Pages

KAPIPI TV

Saturday, August 1, 2015

WATANZANIA CALIFORNIA WAMUAGA BALOZI LIBERATA MULAMULA

 Watanzania California wakiongozwa na Balozi wa Heshima Mhe. Ahmed Issa walijumuika pamoja siku ya Ijumaa na kumuaga Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico na kurudi nyumbani kwenda kulitumikia taifa kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Watanzania wa California wakipiga picha ya pamoja na Mhe. Balozi Libarata Mulamula (wapili toka kushoto) siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomuaga rasmi.
 Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi yake Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme mara tu baada ya kukabidhiwa na Watanzania California siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomualika rasmi kwa ajili ya kumuaga.
 Balozi Liberata Mulamula akicheza na kuburudika kwenye moja ya nyimbo zilizopigwa kwenye tafrija hiyo.
 Balozi Liberata akipiga makofi
Moja wa kikundi maarufu cha ngomma ya asili kikitoa burudani

UZINDUZI WA ALBAMU TATU ZA MWAITEGE NI KESHO UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE, WAIMBAJI WATAKAO MSINDIKIZA WATAMBULISHWA

 Boniface Mwaitege, atakaye zindua albamu zake tatu hapo kesho.
 Faustine Munishi, mmoja wa waimbaji wa injili atakayetoa burudani.
Upendo Kilahiro, atatumbuiza.
Jesca Maguba (BN), atatumbiza

Atosha Kissava, atatumbuiza.
 Mwimbaji wa nyimbo za injili, Boniface Mwaitege (katikati), akiimbaji sanjari na waimbaji wenzake wakati wakitambulishwa kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi. Waimbaji hao kesho watatoa burudani wakati wakimsindikiza mwimbaji mwenzao Boniface Mwaitege katika uzinduzi wa albamu zake tatu za Utanitambuaje, Mama ni mama na Tunapendwa na Mungu utakaofanyika kesho ukumbi wa Diamond Jubilee saa nane mchana kesho. Kutoka kulia ni Faustine Mnishi, Upendo Kilahiro, Jesca Magupa (BN) na Atosha Kissava.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion, Alex Msama (kushoto), akizungumza na wanahabari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya uzinduzi huo.
Msama (katikati), akiwa na waimbaji watakaotoa burudani kwenye uzinduzi huo.

Na Dotto Mwaibale

MWANAMUZIKI wa Injili, Boniface Mwaitege kesho mchana anatarajiwa kuzindua albamu zake tatu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam leo mchana Mkurugenzi wa Kapuni ya Msama Promotion alisema kuwa maandalizi yote muhimu ya tamasha hilo litakalofanyika kuanzia saa nane mchana yamekamilika, Mwaitege atatambulisha albamu hizo kwa kusindikizwa na wanamuziki mbalimbali wa muziki wa Injili.

Alisema mashabiki wa muziki wa Injili watarajie burudani ya nguvu kutokana na maandalizi ya nguvu na ya kipekee aliyofanya mwanamuziki huyo ikiwemo kurekodi albamu hizo katika majiji ya Mwanza, Nairobi na Kenya.

"Maandalizi yote ya uzinduzi wa albamu za Mwaitege yamekamilika, mashabiki watarajie burudani ya nguvu, pamoja na ujumbe kutoka katika nyimbo hizo pamoja na mwanamuziki wengine watakamsindikiza," alisema Msama.

Alisema sehemu ya mapato katika uzinduzi huo ambao pia utafanyika katika mikoa mingine, itapelekwa kwa kwenye vitu vya watoto yatima.

Msama alizitaja albamu hizo ni pamoja na 'Tunapendwa na Mungu' yenye nyimbo za 'Tukiimba Mungu anashuka', 'Mtoto wa mwenzio ni wako', 'Safari Bado', 'Tumekuja Kukuchukua (Bibi harusi)', 'Tuko Salama', 'Moyo wa Shukrani', 'Hakuna Ridhiki', albamu nyingine ni Utanitambuaje na Mama ni Mama.

Baadhi ya wanamuziki watakaopanda jukwaani kusindikiza uzinduzi wa albamu za Mwaitege waliotambulishwa kwa waandishi wa habari na baadhi ya nyimbo zao zilizotamba katika mabano ni Upendo Kilahiro (Baba Ninakuabudu), Jesca 
Magupa (Napokea), Mchungaji Faustine Munishi (Malebo) na Atosha Kisava (Umwema).

Akizungumzia utambulisho wa albamu zake tatu, Mwaitege alisema amejiandaa vizuri kwa uzinduzi huo, ambapo mashabiki wataweza kupata burudani nzuri na ujumbe, pia albamu hizo zitakuwepo ukumbini.

Aliwataka mashabiki kufika kwa wingi katika onesho hilo ili kumpa hamasa yeye na waimbaji wengine ambao watamsindikiza.

Awali wasanii wengine waliotajwa kusindikiza uzinduzi huo ni  pamoja na John Lisu, Martha Mwaipaja, Faustine Munishi, Upendo Nkone, Christopher Mwahangila, Eiphraim Sekereti, Atosha Kisava, Mess Chengula,  Eveline Kabwemela, Ambwene Mwasongwe na Joshua Mlelwa.

Onesho hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini.


Kiingilio katika onesho hilo kitakuwa ni sh. 10,000 kwa viti maalumu, sh. 5,000 na sh.2,000 kwa watoto.
 (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA MSIMU WA NNE LAANZA RASMI, WAFANYIWA SHEREHE YA UKARIBISHO KIJIJI CHA MAKUMBUSHO DAR

Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster akiwashukuru wadau mbalimbali ambao wamefanikisha mchakato mzima wa kuendesha shindano la Mama Shujaa wa Chakula, Pia Kipekee Amewashukuru wafanyakazi wa Oxfam akiwepo Eluka Kibona na Suhaila Thawer kwa kuwa Mstari wa mbele kufanikisha Shindano hili na Mwisho kuwatakia kila Laheri , Shindano hili litaruka katika  Runinga ya ITV Kila siku kuanzia 2.08.2015 -21.08.2015 saa 12 Jioni akicheza ngoma ya kwao wakati wakitambulishwa
 Baadhi ya washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 wakiwa katika Sherehe ya kukaribishwa hapo jana katika kijiji cha Makumbusho
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kisalawe Bw. Ellioth Phillemon akiwakaribisha washiriki wa shindano la Mama Shujaa wa Chakula Wilayani Kisalawe.
 Eluka Kibona, Meneja Utetezi na Ushawishi wa Oxfam akielezea kwa ufupi juu ya Mchakato mzima wa Shindano la Mama shujaa wa chakula ambalo linalenga kuwawezesha wakina mama kutambulika katika kilimo na kueleza Matakwa yao juu ya kilimo endelevu. 
  Bi. Mwanaidi Hamza ambaye anatoka katika Programu ya Big Result now akitoa ushuhuda jinsi gani alivyofanikiwa kulingana na Proramu hiyo na sasa anamaisha mazuri, na kuwasihi wakina mama wasikate tamaa katika kilimo.
 Stephen Mfuko aka Zero akitaja namba za washiriki na Jinsi ambavyo wanaweza Pigiwa Kura  ambapo Programu mzima itaoneshwa katika Runinga ya ITV kila Siku kuanzia Tarehe 2.08.2015-21.08.2015 kuanzia saa 12 Jioni
  Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Jackson Samwel akiwapongeza Shirika la Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow kuanzisha shindano la Mama shujaa wa Chakula , kwa kutambua umuhimu wa ardhi katika kuzalisha chakula, ameshauri akinamama wabadilishane uzoefu pindi watakapokuwa kambini ili kuja na mbinu mpya za kilimo, ufugaji na uvuvi.
 Wanao onekana Mbele ni Baadhi ya wenyeji ambao ndio watakuwa wenyeji wa washiriki wa mama shujaa wa chakula pindi watakapokuwa kijijini.
 Baadhi ya wageni waalikwa katika Sherehe hizo
 za kuwakaribisha Washiriki wa shindano la Mama Shujaa wa chakula linalo endeshwa na Shirika la Oxfam katika Kampeni yao ya Grow.

Friday, July 31, 2015

ALEX MSAMA:MAANDALIZI YA UZINDUZI WA ALBAM YA BONNY MWAITEJE YAMEKAMILIKA

????????????????????????????????????
Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu Uzinduzi wa albam ya muimbaji wa nyimbo za injili Bonny Mwaiteje utakaofanyika jumapili kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, uzinduzi huo utashirikisha mwimbaji wa nyimbo za kutoka Zambia Ephraim Sekereti Faustine Munishi pia atashiriki kwenye uzinduzi huo na waimbaji wengine wengi kutoka hapa nchini
Fedha zitakazopatikana katika uzinduzi huo zitanunua baiskeli kwa ajili ya kuwapatia walemavu katika mikoa ya Ruvuma na Morogoro ambayo haikupata katika mgao wa kwanza na pia zitanunua Chakula kwa ajili ya vituo vya watoto yatima.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
????????????????????????????????????
Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam.
???????????????????????????????????? ???????????????????????????????????? ????????????????????????????????????

RAIS YOWERI MUSEVEN AFUNGUA MKUTANO WA MARAIS WASTAAFU KATIKA HOTELI YA SERENA JIJINI DAR-ES-SALAAM

????????????????????????????????????
Mh. Rais Yoweri Museveni wa Uganda akifungua rasmi mkutano wa Marais wastaafu wa Afrka AFRICA LEADERSHIP FORUM unaofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Mkutano huo unaojumuisha marais wastaafu Benjamin Mkapa wa Tanzania , Olusegun Obasanjo wa Nigeria, Hifikepunye Lucas Pohamba wa Namibia, Festus Mogaye wa Botswana, Bakili Muluzi wa Malawi na Jerry Rowlings wa Ghana unajadili masuala mbalimbali ya maendeleo katika bara la Afrika na Changamoto zinazokabili barahilo na umeandaliwa na Taasisi ya Uongozi Institute.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
????????????????????????????????????
Marais wastaafu Bakili Muluzi wa Malawi kulia na Jerry Rawlings wa Ghana wakiwa katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Rais Mstaafu wa Nigeria Olusegun Obasanjo kushoto na Salim Ahmed Salim Katibu Mkuu Mstaafu wa AU na Waziri mkuu Mstaafu wa Tanzania wakiwa katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya waalikwa kutoka taasisi mbalimbali wakiwa katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Gavana wa Benki KuuProf. Beno Ndulu wa tatu kutoka kulia na wageni mbalimbali wakihudhuria katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Marais wastaafu kutoka kushoto ni Hifikepunye Lucas Pohamba wa Namibia,Benjamin Mkapa wa Tanzania na Festus Mogaye wa Botswana wakifuatilia mkutano huo.
????????????????????????????????????
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel wa pili kutoka kulia pamoja na watendaji wa taasisi mbalimbali wakifuatilia mkutano huo.
????????????????????????????????????
Rais Mstaafu wa Tanzania Mh. Benjamin Mkapa akitoa mada katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Mh. Rais Yoweri Museveni wa Uganda kulia akiwa katika mkutano huo pamoja na marais wastaafu kushoto ni Rais Mstaafu wa Nigeria Mh. Olusegun Obasanjo.

GARI LA KUBEBEA MAJENEZA LA KIPEKEE LAINGIA NCHINI

IMG_0469
Pichani juu na chini ni muonekano wa Gari maalum la kukodisha kwa ajili ya shughuli za kubebea majeneza katika misiba limeingia nchini.
Kwa wanaohitaji kukodi kwa shughuli za misiba wanaweza kuwasiliana kupitia barua pepe kiwiaadavidson@hotmail.com au simu namba +255 715 213213, +255 713 616606 na +255 784616606
IMG_0459 IMG_0481
Muonekano wa ndani sehemu maalum linapowekwa jeneza.
IMG_0477

MSIMU MPYA WA KANDANDA NDANI YA DSTV KUTIMUA VUMBI WIKI IJAYO

IMG_0388
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa msimu mpya wa kandanda kwa wateja wa DStv jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia ni Meneja Mwendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).
IMG_0397
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo, akijibu maswali ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na huduma za DStv. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi.
IMG_0422
Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu, akielezea huduma za kuunganishwa kwa wateja wapya wa DStv, ambapo ving'amuzi pamoja na dishi vinapatikana kwa gharama nafuu kabisa ya Sh.99,000/- kwa mawakala wote wa DStv nchini.
IMG_0443
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi (wa pili kushoto) akikabidhi zawadi ya begi kwa mwandishi wa habari, Joseph Michael baada ya kuchezesha droo kwa waandishi waliohudhuria mkutano huo. Wanaoshuhudia kushoto ni Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia ni Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
IMG_0454
Furaha Samalu na Barbara Kambogi wakikabidhi zawadi ya begi Super Sport kwa mpiga picha wa ITV, Abdallah Kaniki aliyeibuka mshindi katika droo iliyochezeshwa na Multichoice Tanzania wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kulia Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
IMG_0458
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi akikabidhi zawadi ya T-shirts kwa mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Imani Makongoro.
IMG_0419
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Na Andrew Chale, modewjiblog
Msimu mpya wa Soka 2015/16, unatarajia kuanza rasmi Jumapili ijayo kwa kushuhudia ligi mbalimbali Duniani zikichezwa na kurushwa moja kwa moja kupitia SuperSport ambayo imejipanga kukuletea burudani kabambe kwa mashabiki wa soka barani Afrika.
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania , Ronald Baraka Shelukindo mapema jana akizungumza na vyombo vya habari amebainisha kuwa, Wateja wa DStv wakae tayari msimu huu kwenye Ulimwengu wa Mabingwa ambapo timu mbalimbali zimejiimalisha katika kuakikisha zinatwaa ubingwa.
“Ligi ya mwaka zitakuwa za kasi na kuvutia kwa kila timu. Barcelona wanajiandaa kutawala dunia kwa mara nyingine, huku Manchester United wanahitaji kurudisha kiti chao cha Ubingwa Uingereza. Jose Mourinho analenga kuhakikisha Chelsea inabaki juu, wakati huo huo , Hispania inajiandaa kuhakikisha wanashinda kwa mara ya tatu kombe la Euro 2016.” Ameeleza Baraka Shelukindo.
Ameogeza kuwa, Watazamaji wa SuperSport watakuwa na nafasi ya kipekee kushuhudia mechi kwenye ubora wa HD, ikiwa ni pamoja na michuano ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) , Ligi ya Hispania (La Liga) , Ligi ya Mabingwa wa Ulaya(UEFA) na Ligi ndogo ya Ulaya ( Europa) ,mechi za FIFA za kirafiki za kimataifa na Klabu Bingwa ya Dunia , Kombe la Ujerumani , Kombe la Mfalme Hispania (Copa Del Rey) , Kombe la FA na zaidi.
Kwa upande wake, Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi anaeleza kuwa, Katika msimu huu , Ulimwengu wa Mabingwa itakuwa ikionyesha mechi zaidi ya 900 za kimataifa. Wateja wa DStv Compact Plus wataweza kufurahia baadhi ya mechi zaidi ya 450 ‘live’, huku Wateja wa DStv Premium watazawadiwa mechi zote ‘Live’ zitakazorushwa katika chaneli zote za SuperSport .
“Kuanzia msimu huu na kuendelea, vituko vyote vya Ligi Kuu ya Uingereza vitakuwa vikiletwa kwenu kupitia SuperSport 5 ( SS5 ) inayopatikana kwenye kifurushi cha Premium. SS5 sasa itakuwa ni nyumba ya soka la Afrika kwa ligi kuu ya Uingereza huku ikijumuisha mechi 3 ‘Live’ kila Jumamosi na Jumapili. Kuambatana na mechi kutakuwa na vipindi maalum vya soka kama PLTV Kick Off, Match Day Live, Fan Zone, Saturday/Sunday Review, Football Today, Classic Matches, Netbusters na Mech za Wiki” Amebainisha Barbara Kambogi.
Moto wa La Liga utawashwa ndani ya SuperSport 3 ( SS3 ). Chaneli hii itakuwa inakuletea mechi hadi tatu za ligi ya Hispania ‘ Live’ kwa siku ya Jumamosi na Jumapili . Wateja wa DStv Premium na Compact Plus watapata nafasi ya kuangalia mechi za michuano ya Kombe la mashindano Uingereza ndani ya SS3 sambamba na mechi za Jumamosi mchana za Ligi kuu ya Uingereza , mbadala wa mechi inayorushwa ndani ya SS5, pamoja na Ratiba zote za Jumatatu usiku na vipindi vya mahojiano vya studio.
Pamoja na Mechi za ‘Live’ ndani ya SS3 , itakuwa inakuonyesha vipindi muhimu vya shoo za magazeti , yanayojiri ndani ya La Liga, pamoja na vipindi maalum vya ligi za soka . Makombe yote ya mpira wa miguu, Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya Europa, Kombe la FA , Kombe la Mfalme Hispania (Copa Del Rey), Kombe la Ujerumani , Euro 2016 na mechi za kirafiki za kimataifa zitaendelea kutapatikana kwenye SS3 .
Kwa habari zaidi za michezo na ratiba za mechi kwenye SS5 na SS3, tafadhali tembelea www.supersport.com