Pages

KAPIPI TV

Friday, July 24, 2015

RAIS KIKWETE AIFARIJI FAMILIA YA MAREHEMU JOHN EDWARD MCHECHU.

1
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) Bw. Nehemia Mchechu. Rais Kikwete alikwenda nyumbani kwa Mkurugenzi huyo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam julai 23, 2015 kumpa pole kufuatia kifo cha Baba yake aliyekuwa anaugua ugonjwa wa kiharusi.
Marehemu atasafirishwa kuelekea Muheza, Tanga kwa ajili ya Mazishi. Mazishi yatafanyika Kijiji cha Enzi, Muheza – Tanga siku ya Jumamosi tarehe 25/07/2015.
PICHA ZOTE NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM
2
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Marehemu John Edward Mchechu ambaye ni baba wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) Bw. Nehemia Mchechu. Rais Kikwete alikwenda nyumbani kwa Mkurugenzi huyo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam julai 23, 2015 kumpa pole kufuatia kifo cha Baba yake aliyekuwa anaugua ugonjwa wa kiharusi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiifariji familia ya marehemu John Edward Mchechu Mbezi beach jijini Dar es Salaam julai 23, 2015. (wapili kushoto) mtoto wa Marehemu ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchechu.
4
Familia ya marehemu John Edward Mchechu.
5 6
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiondoka mara baada ya kuifariji familia ya marehemu John Edward Mchechu (katika) mtoto wa Marehemu ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchechu.
7
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiagana viongozi mara baada ya kuifariji familia ya marehemu John Edward Mchechu (katika) mtoto wa Marehemu ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchech.
8
Waombolezaji.
9
????????????????????????????????????

"NITASHUGHULIKIA IPASAVYO KERO NA MATATIZO YA WANANCHI WA JIMBO LA TABORA MJINI"-BANDORA MIRAMBO

NA LUCAS RAPHAEL,TABORA

Kazi ya uwakilishi wa wananchi kwenye vyombo vya maamuzi sio kukaa ofisini na kutembelea  gari lenye  kiyoyozi bali ni kuyajua  matatizo na changamoto zinazowakabili na kisha kuzipatia ufumbuzi.


Imekuwa mazoea mara baada ya uchaguzi wabunge na madiwani wa vyama vyote kusahau  wajibu wao kwa wananchi jambo linalowafanya kuhaha unapokaribia wakati wa uchaguzi.



Hebu jaribu kukumbuka nyakati za mwisho wa Bunge hili lililopita la mwisho lililokuwa na bajeti,lilikuwa halina wawakilishi wa kutosha  kwa kuwa wengi wao walijaribu kujirudisha majimboni kwao ili kuanza kujenga upya  imani ya wananchi kuelekea uchaguzi mkuu baada ya kushindwa kufanya hivyo kwa miaka minne na nusu.



Tabia ya kutowajali wananchi imegharimu kwa kiasi kikubwa kasi ya maendeleo kuwa ndogo, Miradi kutokukamilika kwa wakati, Miradi kutekelezwa kwa viwango duni na matumizi mabaya ya fedha za umma na madaraka.



Mmoja kati ya vijana mahili anayeteka kuwani nafasi ya ubunge jimbo la Tabora mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi, Bandora Salum Mirambo (40) ambaye ni mkurungezi wa kampuni ya Salu Security Services Ltd ya Tabora imemkera sana hali hiyo na hata kufikia hatua ya kutoa kauli hiyo.



Anasema wabunge wengi kwa makusudi wamekuwa hawawatumikii wananchi waliowachagua ipasavyo jambo ambalo limekuwa likirudisha nyuma maendeleo ya maeneo husika.



Anasema, “Mimi  nikipewa ridhaa ya kuwa mbunge wa jimbo la Tabora mjini nitahakikisha navitumia vizuri vyombo vya maamuzi kwa maana ya baraza la madiwani na bunge la Jamhuri ya Muungano kutatua matatizo na kero mbalimbali  za wananchi.”



Anasema vyombo hivyo vya maamuzi vikitumiwa vizuri vinaweza kuleta matokeo chanya na kuharakisha maendeleo ya wananchi kwa kuwa ndipo maamuzi ya kibajeti ufanyika.



Anasema wabunge wengi wanaomaliza muda wao wameshindwa kuwatetea wananchi wao bungeni na wala hawakuonekana kwenye vikao vya mabaraza ya madiwani na hivyo kushindwa kujua kinachoendelea kwenye ngazi ya halmashauri.





Anasema ubunge au udiwani unahitaji kiongozi ambaye ni mbunifu, mwenye maono na dira ya kuwavusha watu wake kutoka kwenye umasikini kwa kuzibadili changamoto kuwa fursa.





Bandora anasema suala hilo limekuwa gumu kwa wabunge wengi ambao wamekuwa wakisubiri fedha za kibajeti au za mfuko wa jimbo ambazo zinaukomo na hivyo kushindwa kutatua matatizo na changamoto zinazowakabili wananchi.



Kazi ya uwakilishi inahitaji mtu mwenye upeo wa kupambanua na kuchambua mambo mbalimbali kuanzia ngazi ya kitongoji hadi ngazi ya vikao vya kamati za maendeleo za mitaa, vijiji na kata.



Aidha anasema mtu huyo anapaswa kuutumia upeo wake kuchambua mambo kwenye vikao vya ushauri vya wilaya DCC na mkoa RCC ili kushawishi mwelekeo wa kuzipatia ufumbuzi kero za wananchi wa jimbo lake.



Vikao hivyo muhimu vimekuwa vikipuuzwa na wabunge wengi na hata wanapohudhuria wamekuwa hawatoi mchango chanya au kutoongea kabisa.



Anabainisha kuwa kwa muda mrefu wabunge wengi wameshindwa kuonekana majimboni sio kwa sababu ya vikao vya bunge au vya kamati za kudumu za bunge bali wanaogopa kuombwa misaada na wapiga kura wao.



Jambo hili la kihekima linapaswa kutatuliwa na mbunge kwa kuwaonesha wapiga kura wake fursa zinazowazunguka ili waanzishe shughuli za uzalishaji mali badala ya kuwakimbia kwa hofu ya kuombwa.



Anasema, “Nikifanyikiwa kuwa mbunge nitasimamia upatikanaji wa mikopo ya fedha ,zana za kazi pamoja na maarifa ambayo yatawafanya wananchi kuziona fursa za uzalishaji mali na kuzitumia.”





Anasema kwa kuwashirikisha wananchi wa kada zote tutaimarisha shughuli za VICOBA uanzishwaji wa SACCOS zenye nguvu ambazo zitapambana na masharti ya dhamana yanayotolewa na taasisi za kifedha.



Bandora anasema jambo lingine atakalo lifanya ni kuibana halmashauri ya Manispaa ya Tabora kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana na wanawake.



Anasema endapo halmashauri hiyo ingekuwa ikitenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa mujibu wa sheria ingesaidia kubadili maisha ya wananchi wake kwa kiwango kikubwa.



Anabainisha jambo lingine atakalolipa kipaumbele ni uwazi katika kutekeleza majukumu yake ya kibunge kwa maana ya wapiga kura kujua utaratibu na ratiba ya mikutano ya kibunge, na vikao vya kamati za bunge ili kuondoa visingizio vya kutowajibika kwao.



Jambo lingine atafanya mikutano ya hadhara na wananchi na makundi mbalimbali ya kisekta ili kujua matatizo na changamoto zinazowakabili kabla ya kwenda bungeni tofauti na ilivyosasa ambapo mbunge anakwenda Bungeni kuwasilisha mambo anayoyawaza kutoka kichwani kwake.



Anasema wananchi wa Manispaa ya Tabora wamekabiliwa na migogoro ya ardhi kwa muda mrefu ambayo imedhoofisha shughuli zao za uzalishaji mali na uwekezaji wa makazi na mambo mengine.



Anasema, “Jambo hili nitalisimamia kwa kuwakosoa na kuwakemea waziwazi watu wanaotumia madaraka yao ya utumishi wa umma au ya kisiasa kutengeneza migogoro ya ardhi kwa manufaa yao.”



Kwa kuwa njia nyingine bora ya kukabiliana na vitendo vya dhuluma kwenye ardhi ni kuwawezesha wananchi kuzijua sheria za ardhi za mwaka 1999 na sheria ya mipango miji ya mwaka 2007.



”nitahakikisha wakazi wa mji wa Tabora wanarasimisha shughuli zao pamoja na makazi kwa kupata hati zitakazowawezesha kupata mikopo kwenye taasisi za fedha.”



Anabainisha kuwa atahakikisha vyombo vya kisheria vinavyoshughulikia migogoro ya ardhi vinawezeshwa kwa kupatiwa wataalamu,vitendea kazi na kutekeleza majukumu yake kwa uwazi na haki.



Anavitaja vyombo hivyo  kwa mujibu wa sheria kuwa ni mabaraza ya Ardhi ya kijiji, kata, mabaraza ya Ardhi na nyumba ya wilaya , mahakama kuu kitengo cha Ardhi na mahakama ya Rufaa.



Bandora anaweka wazi kuwa akiwa mbunge ataweka daraja la wazi kati yake na asasi za kiraia, makundi maalumu ya watu wenye ulemavu ambayo yamesahauliwa na wabunge na madiwani.



Aidha anaeleza kuwa ataimarisha misingi ya utawala bora kwa kujenga ofisi za wenyeviti wa mitaa kila kata kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji kwa wananchi.



 Anasema kwa kufanya hivyo kutapunguza malalamiko ya rushwa na kwamba atawawezesha kupata posho na vitendea kazi kila mwezi.



Anasema atasimamia kikamilifu sekta za maji, elimu na afya ambazo zinagusa na kuchochea ustawi wa sekta nyingine.

Bandora anasema atahakikisha zahanati zinakuwa na watumishi wa afya, dawa, vifaa tiba ili kupunguza msongamano kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete.


Aidha atahakikisha mpango wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Tabora unaanza mara moja kwa fedha kutengwa na pia kutafuta misaada kwa wadau wa sekta ya afya.


Mkakati huo anasema ni wa makusudi utasaidia kupunguza vifo vya watoto wenye umri chini ya miaka mitano na akinamama wajawazito.


Atahimiza uimarishwaji wa mpango wa damu salama ambao umepuuzwa na wabunge na madiwani wengi huku wahitaji wakubwa ni watoto na akinamama wajawazito.



Bandora anasema kama wanawake ni jeshi kubwa linalotumika kwenye uchaguzi kwanini limekuwa likisahaulika mara baada ya uchaguzi kwa kuruhusu vifo vyao wakiwa wajawazito?.



Anasema atasimamia mipango ya uboreshaji wa huduma ya maji kutoka mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira TUWASA pamoja na kuhimiza serikali kulipa madeni ya taasisi zake ambayo ni zaidi ya shilingi bilioni moja.

Atahimiza pia utekelezaji wa mradi wa maji ya ziwa Victoria kutokea kijiji cha Solwa Shinyanga kupitia Nzega kuja Tabora na wilaya nyingine za mkoa wa Tabora.


Aidha kwenye elimu atahakikisha hakuna mtoto anayekaa chini katika shule za msingi za manispaa ya Tabora ambako kuna miti ya mbao na mbao za kutosha.



Akizungumzia michezo anasema kwamba atashirikiana na vyama vyote vya michezo kuinua michezo kuanzia ngazi za mitaa, vijiji na kata tofauti na ilivyosasa nguvu  zisizo na utaratibu zimewekwa kwenye soka la wanaume pekee.



Anasema ameamua kufanya hivyo ili kurudisha hadhi ya michezo ya mkoa wa Tabora iliyokuwepo miaka ya nyuma.



“Kukosekana kwa mikakati madhubuti katika michezo kumefanya vipaji vingi vya vijana wa Tabora  kupotea  jambo ambalo limesababisha kupoteza ajira kupitia michezo.”anasema Bandora.



Anasisitiza kukitumikia Chama Cha Mapinduzi na kukifanya kuwakomboa wananchi na wanachama wake kwa kuwaletea maendeleo halisi.

LISTEN TO ERICA LULAKWA’S BRAND NEW SONG “DUNDIKA”

maxresdefault
Debut Album "Piga Moyo Konde" is out! On Itunes http://itunes.apple.com/album/id10046...
Dundika is the 2nd Song released from this Album. Listen free on Spotify and Tidal. If you like the music, I would truly appreciate your support in writing a review or sharing links to iTunes or Google Play on social media.
Listen to her music on you tube below here.

BHALALUSESA ASISITIZA UMUHIMU WA UMAHIRI KATIKA TEHAMA

IMG_8834
Kiongozi wa kitaifa wa mradi wa CFIT, Prof. Ralph Masenge akimkaribisha mgeni rasmi Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa (hayupo pichani) kufungua kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu linalofanyika mjini Bagamoyo.
IMG_8915
Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa akisoma hotuba kwa niaba ya Kamishina wa Elimu, Profesa Eustella Bhalusesa wakati akifungua rasmi kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu linalofanyika mjini Bagamoyo. Kulia ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.
Na Mwandishi wetu, Bagamoyo
KAMISHINA wa Elimu, Profesa Eustella Bhalalusesa amesisitiza haja ya kuhakikisha kwamba viwango vya umahiri vya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu nchini vinakua vya juu kukidhi haja ya matumizi ya kufundishia na kujifunza nchini.
Alitoa kauli hiyo mjini hapa wakati akifungua kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu.
Katika hotuba yake iliyosomwa na Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa alisema kwamba changamoto ya Tehama inaonekana wazi katika matumizi yake na hivyo wakufunzi lazima wawe mahiri.
"Duniani kote, sekta ya uchumi, fani mbalimbali, taasisi na hata mifumo ya maisha yanategemea sana matumizi ya Tehama kwa sasa. Kadhalika, maendeleo makubwa katika Tehama yamebadili namna mambo yanavyofanyika,” alisema.
Alisema kwa kuhakikisha kwamba kuna maendeleo ya kutosha ni vyema walimu kuwa na umahiri unaotakiwa kwani Tehama inachangamoto nyingi zinazotakiwa kuangaliwa ili kuweza kuitumia ipasavyo kuleta mabadiliko katika jamiii.
Aliwataka washiriki kuhakikisha kwamba wanapitia muswada huo kwa makini na kujazia maeneo yote ambayo wataalamu wameshindwa kumaliza na kusaidia kuweka mtaala huo vyema kwa mafunzo.
Kongamano hilo ambalo ni sehemu ya mradi wa kuimarisha uelewa kwa wanafunzi na wakufunzi vyuo vya walimu ili kuboresha matumizi ya Tehama katika mafunzo hasa masomo ya sayansi limeshirikisha wataalamu mbalimbali na kuendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kushirikiana na watu wa China.
Alisema kwamba serikali inatambua kuwa Tehama inaweza kutumika vyema katika kubadili na kuboresha mfumo wa elimu Tanzania.
Aidha alisema Sera mpya ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 inatambua umuhimu wa Tehama katika kuboresha viwango vya elimu nchini Tanzania.
Alisema moja ya malengo ya sera ni kuonesha mahitaji halisi ya Tehama nchini katika upande wa wataalamu na vifaa ili kufanikisha utoaji wa elimu hata ya masafa katika ngazi zote.
Kongamano hilo ni moja ya mradi wa China Funds in Trust Project (CFIT) wa UNESCO na serikali ya China wenye lengo la kusaidia serikali ya Tanzania kuimarisha umahiri wa wakufunzi na walimu kwa kuwawezesha kujua tehama na kuitumia.
Mradi huo umelenga kuongeza uwezo wa vyuo vya walimu na teknolojia ya kisasa ya Tehama na vifaa vyake ili kusaidia kujifunza na kufunza.
Ingawa kwa sasa vyuo vinavyofanyiwa kazi na mradi huo vipo viwili vipo vingine vinane vinavyofunza walimu wa sayansi na hesabu vitaingizwa.
IMG_8909 IMG_8842
Pichani juu na chini ni washiriki wa kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu wakati kongamano hilo likiendelea mjini Bagamoyo.
IMG_8843 IMG_8831
Kiongozi wa kitaifa wa mradi wa CFIT, Prof. Ralph Masenge (kushoto) akijadili jambo na mgeni rasmi Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa (katikati). Kulia ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.
IMG_8826
Kiongozi wa kitaifa wa mradi wa CFIT, Prof. Ralph Masenge (kulia), akifurahi jambo na Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph (katikati) pamoja na Mratibu wa kitaifa wa mradi wa CFIT kutoka UNESCO, Faith Shayo (kushoto) mara baada ya kufunguliwa rasmi kwa kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu.
IMG_8928
Mgeni rasmi Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa (walioketi wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha hiyo inayomalizika leo mjini Bagamoyo.

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA (PTA), YATOA SHILINGI MILIONI MBILI KUSAIDIA WANAHABARI WANAOPAMBANA NA UJANGILI NCHINI

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (PTA), Awadh Massawe akizungumza na wanahabari wakati akikabidhi hundi ya sh.milioni mbili kwa Taasisi ya Habari Development Association Dar es Salaam jana asubuhi. 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (PTA), Awadh Massawe (kushoto), akikabidhi mfano wa hundi ya sh.milioni mbili kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Habari Development Association (HDA), Kunze Mswanyama (kulia), Dar es Salaam jana asubuhi kwa ajili ya kuandaa mafunzo ya kuwawezesha waandishi wa habari kujenga weledi wa kufanya tafiti na kuandika habari za kupambana na ujangili. Wa pili kushoto ni Ofisa Mwandamizi wa Mawasiliano wa TPA, Focus Mauki na Katibu Mkuu wa Taasisi hiyo, Benard James.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Habari Development Association (HDA), Kunze Mswanyama (kulia), akizungumzia kuhusu mafunzo na umuhimu wa wanahabari katika kupambana na ujangili wa rasilimali za taifa kabla ya kukabidhiwa msaada wa sh.milioni 2 kutoka PTA. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa PTA, Awadh Massawe.


Kaimu Mkurugenzi wa PTA, Awadhi Massawe (katikati), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana. Kushoto ni Ofisa Mwandamizi wa Mawasiliano wa TPA, Focus Mauki na Mkurugenzi wa Taasisi ya Habari Development Association (HDA), Kunze Mswanyama.

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imetoa sh. milioni 2 kwa Taasisi ya Habari Development Association kwa ajili kuandaa mafunzo ya kuwawezesha waandishi wa habari kujenga weledi wa kufanya tafiti na kuandika habari za kupambana na ujangili.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Awadh Massawe alikabidhi hundi ya thamani ya fedha hizo kwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Kunze Mswanyama jijini Dar es Salaam jana.“Tunaunga mkono juhudi hizi za kupambana na ujangili,” alisema Massawe. 

Alisema TPA imefanya hivyo kwa kuwa nchi ina tatizo la uwindaji haramu hasa wa ndovu na usafirishaji wa pembe za ndovu na kulisababishia hasara taifa kupitia mipaka yake.

Alifafanua kuwa bandari ya Dar es Salaam ni sehemu ya mpaka wa taifa, hivyo lazima TPA iunge mkono juhudi za kuelimisha jamii na kuzuia uhalifu huo.

Massawe alisema kwa sasa wanatarajia kufunga kamera 400 za CCTV ili kuimarisha ulinzi na kuwa skana tatu zimeletwa bandarini kwa ajili yakuziongezea nguvu skana mbili zilizopo.

Pia, alisema wanatarajia kupata msaada wa mbwa maalumu wa ulinzi watakaotolewa na Serikali ya Marekani. Alisema TPA inaendelea kuwajengea uwezo wafanyakazi kimaadili ili kuendelea kufanya kazi kwa weledi na uaminifu kwa faida ya taifa.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Mswanyama alisema fedha walizopewa watazitumia kwa kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari 54  kwa masuala ya ujangili kupata weledi na kutafiti na kufichua ujangili. “Tunahitaji kujenga uwezo wa kupambana na ujangili  ili taifa liweze kunufaika nazo,” alisema. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)




TAKUKURU YAMKINGIA KIFUA MKURUGENZI WA MANISPAA YA TABORA MBELE YA BARAZA LA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA


Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora, Sipora Liana, akijieleza mbele ya Baraza la  Maadili kwa Viongozi wa Umma Dar es Salaam leo, alipofikishwa kwa tuhuma za kukiuka maadili ya viongozi wa umma alipokuwa Halmshauri ya Manispaa ya Mkuranga mkoani Pwani kabla ya kuhamishiwa Tabora.

Jaji Msumi (katikati), akiwa na wenzake akisikiliza shauri hilo.


Na Dotto Mwaibale

KAMANDA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Wilaya ya Mkuranga, Damas Pasalau, amemkingia kifua aliyekuwa Mkurugenzi wa Halamashauri ya Manispaa ya Mkuranga Sipora Liana kwa tuhuma zinazomkabili katika Baraza la Maadili ya Utumishi wa Umma.


Kwa mujibu wa hati ya mashitaka iliyosomwa katika vikao vya baraza a maadili vilivyoanza jana jijini Dar es Salaam, Sipora ambaye kwa sasa Mkurugenzi wa Manispaa ya Arusha  anakabiliwa na tuhuma za kukiuka maadili.


Inadaiwa kuwa mnamo mwaka 2009/2010 Sipora alimchukulia hatua za kinidhamu bila sababu za msingi kwa kumsimamisha kazi aliyekuwa Ofisa Kilimo, Mifugo na Ushirika Wilaya ya Mkuranga Dk. Fransis Mallya kinyume na sheria ya maadili ya utumishi wa umma.


Pasalaus alitoa utetezi kwa muda wa dakika 30 ambapo kati ya hizo 10 alizitumia kutoa utetezi wakati akiulizwa maswali na Mwanasheria wa Serikali Getrude Cyriacus.


Pasalau ambaye mara kwa mara alibanwa na mwanasheria huyo kwaajiri ya kutoa ushahidi sahihi aliendelea kumtetea huku akitoa mifano mbalimbali na utendaji kazi wake uliofanyika katika Wilaya aliyotoka Sipora huku akidai kuwa ni kitendo hichop ni chuki binafsi hivyo zisiruhusiwe kushika nafasi kwenye mali za umma.


Wakati akitoa ushahidi huo alimtaka Jaji Hamis Msumi kutenda haki na kudai kuwa Mkurugenzi huyo hana kosa bali ni hujuma za baadhi ya watu ambao walikuwa kwa maslahi yao binafsi katika ofisi za Manispaa hiyo.


Alisema awali katika Manispaa hiyo kulikuwa na msuguano kati ya Madiwani, watumishi wa umma na wakurugenzi jambo ambalo baada ya kufanyika kwa uchunguzi na taasisi hiyo ilibainika uwepo wa ubadhilifu wa mali za umma.


"Baada ya Sipora kuwasili katika halmashauri hiyo ambapo katika utendaji kazi wake mzuri watu wengi hawakumpenda kwani wengi wao walikuwa wakifanya shughuli zao kwa maslahi binafsi," alisema.


Alidai baada ya Mkurugenzi huyo kufika na kuonekana utendaji wake unawabana baadhi ya watu akiwemo Mallya na wenzie waliunda kundi ambalo lilikuwa ni kwaajili ya kupambana nae.


"Watu hawa walitumia vyombo vya udhibiti wa maadili kutunga hoja za uwongo ili kuweza kufanikisha malengo yao.


" Ila kiukweli mwenyekiti huyu mama amethubutu na ameweza kulingana na hali ya mazingira yaliyoko katika halmashauri ile kwatu watendaji wengi hawakupenda watu wa aina hii," alisema.


Akifafanua zaidi kuhusu tatizo lililotokea hadi hatua za kusimamishwa kazi zilipotokea alidai kuwa baada ya Mkurugenzi huyo kuwasili katika halmashauri hiyo alianza kufuatilia idara ya Mallya katika kukamilisha miradi ya Mabwawa ya Mkwalia pamoja na ununuzi wa vitotozi visivyofanyakazi na kuweka mashamba hewa ambapo hakuwa amefanya kazi yeyote.


Hata hivyo shauri hilo liliahirishwa kutokana na anaedaiwa kuwa ni mlalamikiwa Sipora, kutofika na mashahidi wake kama alivyowasilisha idadi yao katika baraza la hilo.


Akihairisha kikao cha baraza hilo, Jaji Msumi alisema shauri hilo litasikilizwa hadi pale itakapotolewa hati maalum ya wito kwa mashahidi wa Mkurugenzi huyo. 

.


UZINDUZI RASMI WA KAMPENI YA WAZAZI NIPENDENI NI KESHO VIWANJA VYA MWEMBE YANGA JIJINI DAR ES SALAAM MAANDALIZI YAMEKAMILIKA WANA MUZIKI LULUKI KUTOA BURUDANI

 Mshauri wa masuala ya Malaria kutoka Taasisi ya Jhpiego, Jasmin Chadewa (kushoto), akitoa huduma ya kumpa dawa ya vitamini A, mtoto Rahim Simai,  viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam leo asubuhi ikiwa ni utoaji huduma wa elimu ya afya kwa wajawazito na matumizi ya dawa aina ya SP, upimaji wa malaria pamoja na matumizi ya vyandarua kama muendelezo wa huduma za afya ya mama mjamzito na mtoto kuelekea uzinduzi wa awamu ya pili wa Kampeni ya Wazazi Nipendeni utakaofanyika kesho katika viwanja hivyo.
 Wakina mama wakisubiri kupata huduma katika moja ya banda yaliyopo viwanja vya Mwembe Yanga.
 Maofisa Taasisi ya Center for Comminication Programs Johnns HopKins University wakifunga kitanda cha kujifungulia wajawazito wakati wakitoa huduma mbalimbali viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam leo asubuhi tayari kwa uzinduzi wa Kampeni ya Wazazi Nipendeni utakaofanyika katika viwanja hivyo kesho.
Mtaalamu wa Maabara Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, Mbwana Mohamed (katikati), akimtoa damu, Juma Bakari mkazi wa Yombo Kilakala ikiwa ni utoaji huduma kuelekea uzinduzi wa Kampeni ya Wazazi Nipendeni utakaofanyika kesho. Katikati ni Maida Millanzi wa Hospitali hiyo.
Maofisa Taasisi ya Center for Comminication Programs Johnns HopKins University wakifunga chandarua katika utoaji wa huduma mbalimbali za afya kwa wananchi.

Msimamizi wa masuala ya Malaria  Kata ya Kurasini Hondo Mwindeni (wa pili kulia), akiwaelekeza wananchi waliotembelea moja ya banda jinsi ya kujikinga na vidudu vya malaria.
Mtaalamu wa Maabara Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, Mbwana Mohamed akimtoa damu mpiga picha wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Abdallah Kaniki kwa ajili ya kumpima malaria.
Burudabni mbalimbali zikiendelea. Lakini kesho katika viwanja hivyo itakuwa ni zaidi ya burudani.

Dotto Mwaibale

BENDI ya muziki wa dansi nchini, FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma'
wanatarajia kutoa burudani  ya nguvu wakati wa uzinduzi wa kampeni ya 'Wazazi Nipendeni', itakayofanyika leo kwenye viwanja vya
Mwembe Yanga wilayani Temeke jijini , Dar es Salaam.

Mbali na bendi hiyo kutumbuiza leo, pia kutakuwa na uhondo
mwingine utakaotolewa na wasanii wa kizazi kipya nchini Chegge
Chegunda, Mh Temba na Juma Nature. 

Akizungumza Dar es Salaam jana kiongozi wa FM Academia, Nyoshi el Sadaat alisema watanzania wanatakiwa kujitokeza kwa wingi, ili kujua jinsi ya kujikinga na maambukizi pamoja na kumlinda mama na mtoto huku  wakipata burudani kali toka kwetu bure.

Alisema kuwa nyimbo zote zitakazoimbwa katika viwanja hivyo, zitakuwa na ujumbe utakaogusa watu wa rika zote.

Kiongozi huyo alisema licha ya kupiga nyimbo hizo zitakazokuwa na
ujumbe utakaowagusa wa watu rika zote kutokana na maambukizi, pia
watapiga nyimbo zao zilizowahi kutamba na zinazotamba sasa.

"Tutaporomosha nyimbo zetu zote kali zikiwemo Heshima kwa wanawake, Anna, Sumbungengi, Prison, Kazi ni kazi na nyingine nyingi ambazo tunaamini zitakuwa burudani tosha kwa mashabiki wa dansi watakaofika viwanja vya Mwembe Yanga," alisema Nyoshi

Nyoshi alisema hii itakuwa ni mara ya pili kushiriki kampeni yenye
maudhui kama hayo, hivyo hatowaangusha katika upande wa
burudani."Kundi letu limejipanga vizuri na tutahakikisha ujumbe
tutakaoutoa siku hiyo utabadilisha mwenendo wa jamii ya Tanzania na
kujua thamani zaidi ya kumlinda mama na mtoto," alisema Nyoshi.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi huo wa Wazazi Nipendeni, Waziri Nyoni  alisema kila kitu kimekamilika kuhusiana na tamasha hilo na pia utoaji wa elimu kuhusu Afya ya mama na Mtoto inaendelea kwa siku zote mbili jana na leo.

“Elimu ya afya ya mama na mtoto ni muhimu hivyo tunawakaribisha
watanzania wote mje kupata burudani na elimu ya afya ya mama na mtoto.

Alisema kufayika kwa Kampeni ya Wazazi Nipendeni ni ya awamu ya pili kwa udhamini wa  shirika la Maendeleo ya Kimataifa la watu wa Marekani (USAID),  ikiwa kwa lengo la kumwezesha mjamzito na mwenza wake kuchukua hatua muhimu kuwa na maendeleo mazuri ya ujauzito, kujifungua salama na kuwa na mtoto mwenye afya njema, hadi anapofika mwaka mmoja,” alisema. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712727062)

Thursday, July 23, 2015

JUMUIYA YA WATANZANIA WA DMV NA WASHIRIKA WAO WATOA HUDUMA YA MATIBABU

Mkurugenzi wa Taasisi ya kinamama wa Kiafika inayohusika na ugonjwa wa Saratani ya matiti Bi. Ify Nwabuku(kushoto) akizungumza na wakina mama (hawapo picha) wakati wa utoaji wa matibabu bure kwa wakina mama katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar. Kushoto ni Bi Asha Nyang'anyi ambaye ni mwanakamati wa ustawi wa jamii na maendeleo ya kiuchumiwa jumuiya ya Watanzania DMV.

 Wakina mama wakimsikiliza kwa makini Bi. Ify Nwabuku wakati akitoa maelezo juu ya upimaji wa Saratani kwa wakina mama waliofika kupima afya zao katika hospitali ya Mwananyamala zilizokuwa zikitolewa na Jumuiya ya Watanzania DMV pamoja na  washirika wao walioamua kutoa huduma za kitabibu na madawa bure.
 Dk. George Quintero(kushoto) kutoka Marekani akimtibu meno mtoto Living Andrew aliyeshikwa na mama yake huku akisaidiana na Dk. Emilton Ndashau(kulia) wakatia wa utoaji wa uduma bure iliyodhaminiwa na Jumuiya ya Watanzania DMV pamoja na  washirika wao katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar.