Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akiendelea kutembezwa na Meneja wa NHC Mkoa wa Mwanza Bw. Benedict Kilimba katika mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la Buswelu. |
Saturday, January 31, 2015
MKURUGENZI MKUU WA NHC NEHEMIA MCHECHU ATEMBELEA MIRADI GEITA NA MWANZA
MADIWANI KUMVAA WAZIRI WA UJENZI BUNGENI -KIGOMA
Na Magreth Magosso,Kigoma
BARAZA la madiwani halmashauri ya wilaya ya kigoma Mkoa wa
Kigoma,wameadhimia kwenda Bungeni mkoani Dodoma kuonana na Waziri wa Ujenzi
,ili kutekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya Chankele,Mwamgongo Kagunga kwa
nia ya kuondokana na changamoto ya usafiri wa ziwani( Ziwa Tanganyika ).
Azimio hilo limetokana na sintofahamu ya ukamilishwaji wa
barabara hiyo yenye urefu wa km 65 ambapo kupitia bajeti ya mwaka
2013/14 walitumia kiasi cha sh.milioni 194 kukarabati km 20 kutoka mwandiga
,chankele na kushindwa kufika mwamgongo,ambapo wakazi wa ukanda wa ziwa Tanganyika wanatabika na
usafiri wa majini usiokidhi viwango vya usafiri huo.
Awali diwani wa kata ya mwamgongo Kasim Nyamkunga alihoji
baraza uhalali wa barabara hiyo kucheleshwa ujenzi wake,ilihali Rais Jakaya Kikwete na Waziri mkuu Mizengo
Pinda waliahidi kujengwa kwake kabla ya mwaka huu,ambapo wameona adha
ya wakazi wa vijiji vya kagunga,mgambazi,kaziba kuwa,wana tija ya mradi na
waziri Pinda kudai atachangia sh.milioni 300.
Naye Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi na mazingira Habibu
Hebeye alisema sheria mpya ya mikataba ya miradi ya ujenzi wa miundombinu
inachangia uzoreteshaji wa miradi mbalimbali wa huduma za kijamii kwa kuwa mradi unaoanzia kiasi cha
milioni 50 katika halmashauri zote nchini lazima mkataba upitiwe na mwanasheria mkuu kitendo
kinachokwamisha tija kwa wakati.
Akijibia hilo
Mwenyekiti wa halmashauri Hamis Betese alisema
Februari,10,2015 akishirikiana na mkuu wa wilaya,na mwakilishi kutoka
Tanroada watapanda bungeni kuonana na waziri wa ujenzi ili kukamilisha
mchakato wa ujenzi huo kwa kushirikiana na Tanroad kutokana na
halmashauri
kushindwa kukidhi hitaji la mradi husika.
Kwa upande wa Mkuu wa wilaya Ramadhan Maneno aliwaonya
wataalam wa humo,waache uongo katika usimamiaji wa miradi mbalimbali ya
wananchi,kutokana na baadhi ya watalam kutoa tarifa za uongo hasa katika ujenzi
wa mradi wa maabara ,ambao unasuasua baada ya serikali kuu kuongeza muda wa
miezi sita ili kila halmashauri ifanikishe hilo.
Ally Kisala ni mfanyabiashara mkongwe wa vitenge alisema
kufunguka kwa barabara hiyo ni fursa kwa wananchi kujimiarisha kiuchumi na
shughuli za kitalii kwa kuwa hifadhi ya gombe ipo mwambao mwa ziwa husika na
jamii kupata huduma ya afya kwa wakati kuliko usafiri wa majini ni hatari kwa wajawazito na watoto.
Aidha Katibu wa ccm wilaya hiyo Mobutu Malima alisema changamoto
za wananchi wa ukanda wa mwambao utakwisha kwa ushirikiano baina ya jamii na
viongozi wa serikali ya mkoa haina budi kushinikiza mradi huo uwe chini ya
Tanroad ili kuwakwamua umma kiuchumi,afya na elimu.
Friday, January 30, 2015
BARABARA KWENDA OLOLOSOKWAN TISHIO KWA MAGARI MAKUBWA
Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyemtembelea ofisini kwake wakati wa ziara ya kikazi ya siku nne kwenye kijiji cha Ololosokwani na halmashauri ya Ngorongoro kwa ajili ya maandalizi ya mradi wa kijiji cha digitali unaoendeshwa na Unesco kwa kushirikiana na Ki-elektronic ya Samsung unaotarajiwa kuwasili kijijini hapo mwezi februari ukitokea jijini Dar.
Na Mwandishi wetu, Ngorongoro
MKURUGENZI Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues ameonesha mashaka yake juu ya ubora wa barabara ambazo magari mazito yenye vifaa vya kijiji cha digitali Ololosokwan yanaweza kupita.
Alisema hayo kwenye mazungumzo na Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Elias Wawa Lali wakati alipomtembelea ofisini kwake.
Akiwa katika ofisi za mkuu huyo wa wilaya kumwelezea shughuli za Unesco katika wilaya yake, Mkurugenzi Mkazi huyo alipata nafasi ya kuzungumzia haja ya kuboreshwa kwa maaneo kadha ya barabara kuelekea kijiji cha Olosokwan ili kuyawezesha magari hayo makubwa kufika kwa urahisi.
Huku akimuonesha mkuu wa wilaya baadhi ya picha alizopiga akiwa njiani kukagua njia ya kupita magari hayo na kuangalia maandalizi ya mwisho ya mradi huo mkubwa na wa kipekee nchini alisema hali ya barabara si nzuri hata kidogo.
Vifaa kwa ajili ya kijiji hicho vipo bandarini tayari na magari yanayoweza kubeba makontena hayo ni makubwa na barabara za kuelekea kijiji hicho ni mbaya.
Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali (katikati) akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kulia) aliyeambatana na wataalamu wa elimu, afya na mawasiliano pamoja na Mratibu wa Taifa wa tiba asilia na mbadala katika Idara ya Tiba Wizara ya Afya na ustawi wa jamii. Dkt Liggy Vumilia (hayupo pichani) . Kutoka kushoto wa kwanza ni Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias, Afisa mipango ya Elimu wa Shirika la UNESCO, Bi. Jennifer Kotta pamoja na Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph.
Kuwapo kwa kijiji hicho ni matokeo ya mkataba uliotiwa saini kati ya UNESCO na kampuni ya elektroniki ya Samsung mwaka jana.
Katika makubaliano hayo yalitiwa saini na Mwakilishi mkazi Unesco nchini, Zulmira Rodrigues na Mkurugenzi wa Samsung Electronics nchini Tanzania, Mike Seo katika Kijiji hicho kitakuwa na shule yenye Tehama ikiwa na maunganisho ya intaneti, kiliniki ya kisasa ikiwa na kituo cha teknolojia ya mawasiliano yenye kuwezesha utabibu (Telemedicine) na jenereta linalotumia nguvu za jua kwa ajili ya kijiji hicho.
Mradi huo utawezesha UNESCO kuwapatia vijana wa Kimasai elimu kutokana na ukweli kuwa kwa utamaduni na kazi zao za ufugaji wamekuwa wakipata shida ya kupata elimu.
Mkutano huo pia ulihudhuriwa na wataalam wa Elimu, Afya, Utamaduni na Kilimo kutoka Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro jijini Arusha. Kushoto pichani ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Dkt. Peter Kitenyi.
Kupitia kijiji hicho vijana wataendelea na masomo hata kama wanachunga mifugo yao.
Wakati wa utiaji saini Mkurugenzi wa Samsung Electronics nchini Tanzania alitaja miongoni mwa manufaa makubwa yatakayopatikana katika mradi huo wa kijiji cha digitali huko Loliondo ambayo ni pamoja na kuweza kupata nishati rahisi na iliyo rafiki kwa mazingira.
Alisema kwamba Afrika imekuwa mstari wa mbele katika uanzishaji wa vijiji vya digitali. Aidha kwa kitendo hicho Afrika inaonesha dunia ni kwa namna teknolojia inaweza kutumika kuleta mabadikliko chanya yanayotakiwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi waliopo vijijini.
Kijiji hicho cha Loliondo kitakuwa cha nne katika vijiji vya kidigitali barani Afrika.Inatarajiwa kwamba kijiji kingine kitajengwa mjini Zanzibar kwa ushirikiano wa UNESCO na Samsung Electronics mwaka huu.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akifafanua jambo kwa Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali wakati wa mazungumzo na mkuu wa wilaya hiyo kabla ya kuelekea kijiji cha Ololosokwani kwa ajili ya mkutano na wanakijiji wa kijiji hicho kabla ya kuwasili kwa mradi wa kijiji cha kidigitali mapema mwezi februari.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akielezea changamoto za miundo mbinu ya barabara kwa kutumia picha alizopiga akiwa njiani kuelekea kijiji cha Ololosokwan kupitia barabara ya Lake Natron kwa Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali.
Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali akielezea jitihada zitakazofanywa na wilaya yake katika kuhakikisha miundo mbinu ya barabara inarekebishwa kuondoa usumbufu kwa magari mazito yenye vifaa vya kijiji cha digitali cha Ololosokwan yanapita bila kikwazo mapema mwezi februari.
Wataalamu kutoka halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, Unesco pamoja na Wizara ya afya wakitazama picha hizo kwenye kompyuta mpakato ya Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues ofisini kwa Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro.
KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AZURU KABURI LA ALIYEKUWA MAKAMU WA RAIS HAYATI DR.OMAR ALY JUMA
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini kitabu cha
wageni wakati alipozuru kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais Hayati Dr.
Omar Ali Juma aliyefariki mwaka 2001 katika kijiji cha cha Wawi Mchekeni
wilaya ya Chakechako mkoa wa Kusini Pemba leo, katikati ni MNEC wa
wilaya ya Chakechake Bw. Daud Ismail.(PICHA NA KIKOSIKAZI FULLSHANGWE-
KUSINI PEMBA)
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na viongozi
wengine wakiomba dua wakati Katibu Mkuu huyo na msafara wake walipozuru
kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais Hayati Dr. Omar Ali Juma.
Baadhi ya viongozi wanawake nao wakijumuika kuomba dua.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akinywa kahawa na baadhi
ya viongozi kutoka kulia ni Balozi Ali Karume mjumbe wa halmashari kuu
ya Taifa, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai na Mzee Ali
Abdalla Ali.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakichimba msingi wakati
aliposhiriki ujenzi wa madarasa katika skuli ya msingi ya Tumbi
Chambaageni wilaya ya Mkoani.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai akishiriki ujenzi wa
madarasa katika skuli ya msingi ya Tumbi Chumbaageni wilaya ya Mkoani
Kusini Pemba.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakipanda mbogamboga
wakati alipotembelea na kukagua shughuli za kilimo cha mbogamboga
zinazofanwa na kikundi cha ujasiriamali cha Jambo Group Corporation
Society chenye wanachama 15 katika Shehia ya Wambaa kwa Anzani kulia ni
Hafidh Ali Juma Katibu wa kikundi hicho.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua kilimo cha
mbogamboga la kikundi cha Jambo Group Corporation Society kushoto ni
Hafidh Juma Ali Katibu wa kikundi hicho.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutka
kwa Hafidh Juma Ali katibu wa kikundi cha Jambo Group Corporation
Society alipokitembelea kikundi hicho Wambaa kwa Anzania.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia na viongozi
wengine akirejea mara baada ya kukagua kilimo cha mbogamboga katika
kikundi cha Jambo Group Corporation Society
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa tawi la CCM la Milimuni wilaya ya Mkoani Kusini Pemba.
Shamba la migomba la kikundi cha Utandawazi Corporation Group Society kinachojisughulisha na kilimo cha ndizi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda
migomba katika shamba la kikundi cha Utandawazi Corporation Group
Society.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wana CCM wakati alipomtembelea balozi Ame Vuai Shein wa shina namba 1 Kadarani Chokocho. |
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na balozi
mstaafu mzee Makame Bakari Haji alipomtembelea nyumbani kwake na
kumjulia hali kutokana na kuugua maradhi.
Baadhi ya vijana wa CCM wakiimba wakati alipokuwa wakimkaribisha
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kambi yao iliyopo
Chokocho wilaya ya Mkoani Kusini Pemba.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiiimba wimbo na vijana hawapo pichani pamoja na viongozi wengine.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na vijana
wa CCM wakati alipozindua darasa la Itikadi katika kambi yao huko
Chokocha Kusini Pemba.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Vuai Ali Vuai akizungumza katika
mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Mjimbini wilaya
ya Mkoani.
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya wana CCM wakiwa mkutanoni.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi
katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira wa
Mjimbini.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo.
ZIARA YA MKURUGENZI MKUU WA NHC GEITA NA KAGERA YAHAMASISHA MAENDELEO
Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu akiongea
na kikundi cha vijana cha Mshikamano Wilayani Muleba alipokitembelea kuona
namna kinavtumia mashine zilizotolewa na NHC ili kuongeza ajira kwa vijana. Bw.
Mchechu amezitaka Halmashauri za Wilaya nchini kuunga mkono juhudi za NHC kwa
kuwapatia vijana maeneo ya kufanyia kazi zao.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu
ukiwa eneo la Mtukula linapojengwa jingo la kisasa la biashara na NHC ili
kuvutia na kuchochea ukuaji wa biashara katika eneo hilo la mpaka wa Tanzania
na Uganda. Eneo hili ndipo zilipokuwa nyumba ndogondogo zilizojengwa na NHC na
baadaye kuharibiwa na mabomu ya Nduli Iddi Amin alipovamia nchi yetu mwaka
1978. NHC iliiomba Halmashauri ya Wilaya
ya Misenyi kulirejeshea eneo hilo ili kujenga jengo hilo la kibiashara
Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu akikagua
viwanja vya NHC Wilayani Chato vinavyokusudiwa kujengwa nyumba za gharama nafuu
ikiwa ni program ya NHC ya kuzifikia Wilaya zote nchini.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu
ukikagua nyumba za makazi za NHC Wilayani Chato alipotembelea Wilaya hiyo jana.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu akimpa
maelezo Mjumbe wa Bodi ya NHC Bi Subira Mchumo ya juhudi zinazofanywa na NHC katika Halmashauri
mbalimbali za Wilaya nchini za kuwapatia wananchi makazi bora. Ujumbe huo
ulitembelea mradi wa nyumba za gharama nafuu Wilayani Muleba.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu akikagua
mradi wa nyumba za gharama nafuu Wilayani Muleba na kusisitiza matumizi ya malighafi
zinazopatikana katika maeneo husika ili kupunguza gharama za nyumba hizo.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu
ukikagua nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC katika Wilaya ya Muleba
kwa ajili ya kuuzia wananchi. Nyumba hizo ziko katika hatua ya mwisho ya
ukamilishaji.
Msanifu wa Majengo wa NHC Bw. Kintu akitoa maelezo kwa Mkurugenzi
Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu ya jengo linalojengwa na NHC eneo la
Mtukula ili kukuza biashara upande wa Tanzania.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC ulipata pia fursa ya
kutembelea kiwanda cha Sukari cha Mtibwa kujionea juhudi zinazofanywa na
mwekezaji wa kiwanda hicho katika kutoa ajira kwa watanzania.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC BW. Nehemia Kyando Mchechu akipewa
maelezo na Kiongozi wa kikundi cha vijana kilichoko Wilaya ya Bukoba Mjini waliyofadhiliwa
na NHC mashine za kutengezea matofali ili kujipatia ajira