Pages

KAPIPI TV

Saturday, January 31, 2015

MADIWANI KUMVAA WAZIRI WA UJENZI BUNGENI -KIGOMA

Na Magreth   Magosso,Kigoma

BARAZA la madiwani halmashauri ya wilaya ya kigoma Mkoa wa Kigoma,wameadhimia kwenda Bungeni mkoani Dodoma kuonana na Waziri wa Ujenzi ,ili kutekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya Chankele,Mwamgongo Kagunga kwa nia ya kuondokana na changamoto ya usafiri wa  ziwani( Ziwa Tanganyika ).

Azimio hilo limetokana na sintofahamu ya ukamilishwaji wa barabara hiyo yenye urefu wa km 65  ambapo kupitia bajeti ya mwaka 2013/14 walitumia kiasi cha sh.milioni 194 kukarabati km 20 kutoka mwandiga ,chankele  na kushindwa kufika mwamgongo,ambapo wakazi wa ukanda wa ziwa Tanganyika wanatabika na usafiri wa majini usiokidhi viwango vya usafiri huo.

Awali diwani wa kata ya mwamgongo Kasim Nyamkunga alihoji baraza uhalali wa barabara hiyo kucheleshwa ujenzi wake,ilihali  Rais Jakaya Kikwete na Waziri mkuu Mizengo Pinda waliahidi kujengwa kwake kabla ya mwaka huu,ambapo wameona adha ya wakazi wa vijiji vya kagunga,mgambazi,kaziba kuwa,wana tija ya mradi na  waziri Pinda kudai atachangia sh.milioni 300.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi na mazingira Habibu Hebeye alisema sheria mpya ya mikataba ya miradi ya ujenzi wa miundombinu inachangia uzoreteshaji wa miradi mbalimbali wa huduma za kijamii kwa kuwa mradi unaoanzia kiasi  cha  milioni 50 katika halmashauri zote nchini lazima mkataba upitiwe na mwanasheria mkuu kitendo kinachokwamisha tija kwa wakati.

Akijibia hilo Mwenyekiti wa halmashauri Hamis Betese alisema Februari,10,2015 akishirikiana na mkuu wa wilaya,na mwakilishi kutoka Tanroada watapanda bungeni kuonana na waziri wa ujenzi ili kukamilisha mchakato wa ujenzi huo kwa kushirikiana na Tanroad kutokana na halmashauri kushindwa kukidhi hitaji la mradi husika.

Kwa upande wa Mkuu wa wilaya Ramadhan Maneno aliwaonya wataalam wa humo,waache uongo katika usimamiaji wa miradi mbalimbali ya wananchi,kutokana na baadhi ya watalam kutoa tarifa za uongo hasa katika ujenzi wa mradi wa maabara ,ambao unasuasua baada ya serikali kuu kuongeza muda wa miezi sita ili kila halmashauri ifanikishe hilo.

Ally Kisala ni mfanyabiashara mkongwe wa vitenge alisema kufunguka kwa barabara hiyo ni fursa kwa wananchi kujimiarisha kiuchumi na shughuli za kitalii kwa kuwa hifadhi ya gombe ipo mwambao mwa ziwa husika na jamii kupata huduma ya afya kwa wakati kuliko usafiri wa majini ni hatari  kwa wajawazito na watoto.

Aidha Katibu wa ccm wilaya hiyo Mobutu Malima alisema changamoto za wananchi wa ukanda wa mwambao utakwisha kwa ushirikiano baina ya jamii na viongozi wa serikali ya mkoa haina budi kushinikiza mradi huo uwe chini ya Tanroad ili kuwakwamua umma kiuchumi,afya na elimu.

No comments: