Tuesday, August 5, 2014
MBUNGE WA JIMBO LA CHALINZE AZINDUA MAKTABA YA KISASA SHULE YA SEKONDARI CHALINZE
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh.
Ridhiwani Kikwete akikata utepe kuzindua maktaba ya shule ya sekondari
ya Chalinze mjini Chalinze jana ambayo imejengwa na Kampuni ya Tanga
Cement kupitia bidhaa yake ya Simba Cement kwa kushirikiana na taasisi
ya Read International kwa gharama ya shilingi milioni 42 za kitanzania
katika kuboresha elimu jimboni humo, Mbunge huyo pia ameahidi kujenga
jiko katika shule hiyo na kuongeza kompyuta ili wanafunzi wajengewe
mzingira mazuri zaidi ya kujisomea lakini pia ameahidi kushughulikia
tatizo la wanafunzi 10 ambao wamefauru kwenda kidato cha ano na sita
lakini hawakupata nafasi ya kuchaguliwa, hivyo ameueleza uongozi wa
shule hiyo pamoja na wazazi kwamba wanafunzi hao lazima watafutiwe
nafasi ya kuendelea na shule hata kama itakuwa siyo ndani ya jimbo la
Chalinze, “Muhimu wapate nafasi ya kuendelea na elimu yao ya kidato cha
tano na sita” Alisema Mh. Ridhiwani Kikwete alimuomba mwenyekiti wa
bodi ya shule hiyo Bw. Mbwana Madeni amkabidhi majina ya wanafunzi wote
kumi ili yaanze kufanyiwa kazi mara moja.(PICHA NA KIKSIKAZI CHA
FULLSHANGWE-CHALINZE)
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh
Ridhiwani Kikweteakipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa bodi ya shule
ya sekondari Chalinze Bw. Mbwana Madeni kabla ya kuzindua rasmi maktaba
ya shule hiyo, Katikati ni Emma Lyu kutoka taasisi ya Read International
na kushoto ni Raquel Araya kutoka Taasisi ya Read International pia.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh
Ridhiwani Kikwete akionyeshwa vitabu mbalimbali vilivyopo katika maktaba
ya shule ya sekondari ya Chalinze na Najma Juma kutoka Chuo Kikuuu cha
Dar es salaam UDSM ambaye anafanya kazi za kujitolea katika taasisi ya
Read Internional.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh
Ridhiwani Kikweteakiangalia kitabu wakati akikagua maktaba hiyo kulia
kwake ni Najma Juma wa Read International.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh
Ridhiwani Kikweteakiweka alama za kiganja chake kama kumbukumbu wakati
alipozindua maktaba hiyo jana kwenye shule ya sekondari ya Chalinze.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh
Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati Mwenyekiti wa bodi ya shule
ya sekondari Chalinze Bw. Mbwana Madeni alipokuwa akisoma risala yake
mbele ya mbunge huyo, kutoka kulia ni Raquel Araya kutoa taasisi ya Read
International na mkuu wa ituo cha polisi cha Chalinze Afande J.S Magomi.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh
Ridhiwani Kikwetea akizungumza na wanafunzi wa sule ya sekondari ya
Chalinze pamoja na walimu mara baada ya kuzindua maktaba katika shule
hiyo jana kushoto ni Mbwana Madeni mwenyekiti wa bodi ya shule, na
kutoka kulia ni Raquel Araya kutoka Read International na mkuu wa ituo cha polisi cha Chalinze Afande J.S Magomi.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh
Ridhiwani Kikwetea akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya
kuzindua maktaba hiyo kushoto ni mdau wa masuala ya habari Dk Fadhil
Kabujanta wa Fadhaget Sanitarium Clinic ya Mbezi Africana jijini dar es
salaam.
Meneja masoko wa Simba Cement
Yasin Hussein akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa
Maktaba ya shule hiyo iliyojengwa na Kampuni hiyo gharama yake ikiwa ni
shilingi milioni 42 za kitanzania.
WAKULIMA MBEYA WANEEMEKA NA ELIMU YA UZALISHAJI WA MBOGA MBOGA KUTOKA TAHA
Mh.
Dr. Christine Ishengoma Mkuu wa Mkoa wa Iringa akipokea taarifa kuhusu
mfumo wa taarifa za masoko kutoka TAHA unavyofanya kazi zake kutoka kwa
Cyrila Antony Afisa wa Masoko
Mkuu
wa mkoa wa Iringa Mh. Dr. Christine Ishengoma akisikiliza maelezo
kutoka kwa Mtaalamu wa kilimo wa TAHA Bw Ringo kuhusu uzalishaji wa zao
la nyanya
Elimu ikiendelea kutolewa
Vitalu na green houses
Aina Mbalimbali za matunda ambazo zimezalishwa na wakulima kutokana na elimu Bora waliyo ipata kutoka TAHA
Mwananchi akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa TAHA
Teknolojia ya umwagiliaji kwa mfumo wa kilimo cha matone ambao pia unaonesha utengenezaji bora wa matuta, nafasi na usafi
Hivi ni Vitalu vya TAHA na Barton Tanzania
Vitalu vya mboga na green house kama zinavyoonekana katika picha
Watangazaji wa Radio Sweet FM ya Mbeya wakishangaa ubora wa karoti ambayo ni daraja la kwanza inapopelekwa sokoni
Zao la chines
Zao la karoti lililopandwa kwenye vitalu vilivyopo ndani ya viwanja vya Nanenane Mbeya kwenye Banda la TAHA
Mwananchi akifurahia maelezo kuhusu zao la karoti daraja la kwanza
Wakulima na wananchi mkoani Mbeya
wameendelea kuneemeka na elimu ya bure ya uzalishaji wa mazao ya mboga, viungo
na matunda inayotolewa na Asasi ya wakulima, wafanyabiashara na watoa huduma ya
mazao ya horticulture nchini Tanzania (TAHA).
wameendelea kuneemeka na elimu ya bure ya uzalishaji wa mazao ya mboga, viungo
na matunda inayotolewa na Asasi ya wakulima, wafanyabiashara na watoa huduma ya
mazao ya horticulture nchini Tanzania (TAHA).
Wakulima hao wameneemeka na elimu
hiyo inayotolewa na maafisa wa ufundi wa kilimo kutoka TAHA kwa ushirikiano na
wale wa Barton Tanzania ambao kwa pamoja wameweka kambi katika viwanja hivyo
ili kuhakikisha jamii ya wakulima wa mboga kutoka ukanda wa Nyanda za Juu
Kusini wanapata elimu ya msingi bora ya uzalishaji wa mboga wenye tija.
hiyo inayotolewa na maafisa wa ufundi wa kilimo kutoka TAHA kwa ushirikiano na
wale wa Barton Tanzania ambao kwa pamoja wameweka kambi katika viwanja hivyo
ili kuhakikisha jamii ya wakulima wa mboga kutoka ukanda wa Nyanda za Juu
Kusini wanapata elimu ya msingi bora ya uzalishaji wa mboga wenye tija.
“Mpaka sasa tumetembelewa na
wananchi na wakulima wasiopungua 460 ambao wamefika katika banda letu hapa
Nanenane kwenye viwanja vya John Mwakangale wakitaka kujifunza mbinu na misingi
ya awali ya uzalishaji wa mazao ya horticulture, hiyo ni ishara njema kwani
inaonesha ni kiasi gani wananchi
wanatafuta mbinu fasaha inayoweza kuwakwamua kutoka katika uzalishaji wa
mboga wa kawaida mpaka uzalishaji wa tija unaozingatia viwango vya kitaifa na
kimataifa” Alisema Likati Thomas afisa Mawasiliano kutoka TAHA.
wananchi na wakulima wasiopungua 460 ambao wamefika katika banda letu hapa
Nanenane kwenye viwanja vya John Mwakangale wakitaka kujifunza mbinu na misingi
ya awali ya uzalishaji wa mazao ya horticulture, hiyo ni ishara njema kwani
inaonesha ni kiasi gani wananchi
wanatafuta mbinu fasaha inayoweza kuwakwamua kutoka katika uzalishaji wa
mboga wa kawaida mpaka uzalishaji wa tija unaozingatia viwango vya kitaifa na
kimataifa” Alisema Likati Thomas afisa Mawasiliano kutoka TAHA.
Akifafanua zaidi kuhusu elimu ya
kilimo cha uzalishaji wa mboga kwenye banda la TAHA afisa mawasiliano huyo
alisema kuwa wamepanda mazao tofauti katika ploti zilizopo kwenye eneo lao
ambapo wakulima na wananchi wanaopata fursa ya kutembelea eneo hilo ujifunza
teknolojia mbalimbali za uzalishaji kama vile uzalishaji unaozingatia Mbegu
bora zenye tija.
kilimo cha uzalishaji wa mboga kwenye banda la TAHA afisa mawasiliano huyo
alisema kuwa wamepanda mazao tofauti katika ploti zilizopo kwenye eneo lao
ambapo wakulima na wananchi wanaopata fursa ya kutembelea eneo hilo ujifunza
teknolojia mbalimbali za uzalishaji kama vile uzalishaji unaozingatia Mbegu
bora zenye tija.
Teknolojia nyingine ni pamoja na
upandaji mazao unaozingatia nafasi kati ya miche na miche, umwagiliaji kwa njia
ya matone(drip irrigation) unaozingatia uhifadhi wa maji na mazingira pamoja na
ulimaji wa matuta yaliyoinuka ili kutoa nafasi kwa mizizi ya mimea kupenyeza
kwenye udongo ili kujitafutia lishe.
upandaji mazao unaozingatia nafasi kati ya miche na miche, umwagiliaji kwa njia
ya matone(drip irrigation) unaozingatia uhifadhi wa maji na mazingira pamoja na
ulimaji wa matuta yaliyoinuka ili kutoa nafasi kwa mizizi ya mimea kupenyeza
kwenye udongo ili kujitafutia lishe.
Mbali na elimu hiyo ya uzalishaji
wa mboga, wananchi wa Mbeya wanaotembelea banda hilo pia wanapata fursa ya
kujifunza elimulishe kutoka kwa mtaalamu wa masuala ya lishe wa TAHA Bi.
Lawrencia …..ambaye amekuwa akiwafundisha wananchi juu ya umuhimu wa ulaji wa
mboga na faida zake kwa afya ya miili yetu.
wa mboga, wananchi wa Mbeya wanaotembelea banda hilo pia wanapata fursa ya
kujifunza elimulishe kutoka kwa mtaalamu wa masuala ya lishe wa TAHA Bi.
Lawrencia …..ambaye amekuwa akiwafundisha wananchi juu ya umuhimu wa ulaji wa
mboga na faida zake kwa afya ya miili yetu.
MZEE YUSUPH AINGIA RASMI KWENYE FILAMU NA HII NDIO TRELA YA MUVI YAKE IITWAYO NITADUMU NAYE
Itaanza Kupatikana Kuanzia Jumatatu ya tarehe 11 August 2014 katika Maduka yote Tanzania. Usikose Nakala Yako.
MAHAKAMA YAFUTILIA MBALI KESI INAYOWAKABILI VIONGOZI WA MSIKITI MKUU WA IJUMAA GONGONI-TABORA
Monday, August 4, 2014
STAR OILS KAMPUNI DADA YA MeTL GROUP YAPATA MKOPO WA BILIONI 100 KUTOKA NBC
Mkurugenzi
Mtendaji wa NBC, Bi. Mizinga Melu akizungumza kwenye hafla ya utiliaji
saini wa mkopo wa bilioni 100 za kitanzania baina ya benki yake na
kampuni ya MeTL mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
.MetTL yajipanga kupanua soko lake la mafuta Afrika Mashariki na Kusini
Na Mwandishi wetu
KAMPUNI
ya Mohammed Enterpries Tanzania Limited (MeTL GROUP) kupitia kampuni
yake dada ya kuingiza, kuhifadhi na kusambaza mafuta nchini ya Star Oils
Ltd. imepata mkopo wa bilioni 100 kutoka kwa Benki ya Taifa ya Biashara
(NBC).
Akizungumza
na waandishi wa habari muda mfupi baada ya hafla ya utiliaji saini wa
mkopo huo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu na
Mbunge wa Singida Mjini, Mhe, Mohammed Dewji (MO) amesema mkopo huo
utafungua mianya zaidi kwa kampuni ya Star Oils kusambaza mafuta nje na
ndani ya nchi.
Amesema
kwamba baada ya majadiliano ya muda mrefu kati ya timu ya wataalamu
kutoka MeTL makao makuu na maafisa wa NBC kutoka nchini na Afrika Kusini
wamefikia makubaliano ya kupata mkopo huo mkubwa na wa aina yake katika
sekta ya mafuta hapa Tanzania.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP, Mhe Mohammed Dewji (MO), akizungumza
kwenye hafla hiyo ya utiliaji saini wa mkopo wa bilioni 100 za
kitanzania.
Amesema
kwamba kampuni ya Star Oils ina mipango ya kusambaza mafuta katika nchi
za Afrika Mashariki na Kusini mwa jangwa la Sahara ikiwa ni sehemu ya
mikakati yake ya kujipanua kibiashara ndani na nje ya Afrika.
“Mpango
huu utaiwezesha Star Oils kupanua malengo yake katika soko la kimataifa
ikiwa ni pamoja na kukuza uzalishaji na usambazaji wake katika ngazi ya
Afrika Mashariki na Kusini mwa jangwa la sahara,” amesema MO.
MO
aliongeza kuwa hatua ambayo kampuni hiyo imefikia ni kubwa kwa kuonyesha
dhamira ya kuwekeza na kufanya biashara ya mafuta Afrika mashariki na
kusini mwa jangwa la sahara.
“Mkopo
huu utasaidia kampuni ya Star Oils kuongeza uzalishaji na usambazaji wa
mafuta ya kwenye soko la Afrika mashariki na kusini mwa Afrika,”
Mkuu
wa Idara- Huduma za Kibenki kwa Wateja wakubwa na Uwekezaji wa NBC,
Andre Potgieter akizungumza na wageni waalikwa kwa kutaja shughuli
mbalimbali na bidhaa huduma za benki hiyo.
“Sisi
tuna mipango ya kuanza kusambaza mafuta na bidhaa za Petroli katika
nchini za Kusini mwa Afrika kama sehemu ya jitihada za kampuni za
kupanua biashara zake katika soko la Afrika,” amesema.
Kwa
upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Star Oils Ltd, Nazir Haji amesema
kwamba mkopo huo utachochea chachu ya uzalishaji, uhifadhi na usambazaji
wa mafuta na kusukuma maendeleo ya sekta mafuta nchini.
Amesema
kwamba kampuni ya Star Oils inajipanga kufanya biashara ya mafuta kuwa
endelevu hapa nchini na Afrika mashariki ili uchumi wa nchi za Afrika
mashariki ziweze kukua kwa kutegemea tija ya uzalishaji wa mafuta.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Bi. Mizinga Melu amesema kuwa
benki hiyo inahitimisha safari ya majadiliano na kampuni mama ya Star
Oils, Mohammed Entrepries Tanzania Limited (MeTL GROUP) ya mkopo wa
bilioni 100.
“Star
Oils ni kampuni dada ya METL ni moja ya makampuni yanayokwenda kasi
katika biashara ya ushindani katika Afrika Mashariki na Kusini mwa
jangwa la sahara na rekodi yao ya mauzo na biashara ni ya kuridhisha,”
amesema.
Mkuu
wa Idara- Huduma za Kibenki kwa Wateja wakubwa na Uwekezaji wa NBC,
Andre Potgieter akionyesha toleo la jarida la “THE AFRICA REPORT”
lilioandika mafanikio ya kampuni ya MeTL GROUP zilizomvutia zaidi na
kupelekea kuwa na imani na kampuni hiyo na kuamua kufanya biashara nao.
Aliongeza
kwamba METL ni moja ya makampuni yalionyesha rekodi nzuri katika
biashara ya viwanda, nguo, vinywaji, bima na mafuta na wanastahili
kuwezesha kwa kupata mikopo mikubwa na ya muda mrefu kupitia taasisi za
kifedha nchini na nje ya nchi,”
“Sisi
kwenye benki ya NBC tunayofuraha kubwa kwa kupata nafasi ya kufanya
biashara na moja ya makampuni yanayokuja kwa kasi katika bara la Afrika
na vile vile NBC ni benki ambayo ipo tayari kusaidia wateja wake,”
aliongeza
Bi.
Melu alisisitiza kuwa baada ya NBC kuridhisha na shughuli za kibiashara
na mzunguko wa fedha wa MeTL wameamua kutoa mkopo huo ili waweze kupanua
biashara yao katika masoko ya kimataifa.
Star
Oils kwa sasa inatekeleza awamu ya pili ya mradi mkubwa wa kuhifadhi
mafuta ya Petroli na baadaye kujenga usambazaji wa mafuta nchi nzima kwa
njia ya mlolongo wa vituo vya karibu 200 vya Petroli nchini.
Mkuu
wa Idara- Huduma za Kibenki kwa Wateja wakubwa na Uwekezaji wa NBC,
Andre Potgieter akipeana mkono wa pongezi na Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL
GROUP, Mhe, Mohammed Dewji.
Uwezo
wa jumla ya uhifadhi wa kituo hiki juu ya kukamilisha mradi itakuwa
lita 68 milioni, kuundwa tu kwa ajili ya kuhifadhi ya Petroli, Gesi
Mafuta na mafuta ya taa. Wingi wa bidhaa hizi kwa sasa ni kuuzwa kwa
misingi ya jumla na mipango ya baadaye soko lao kupitia vituo vya METL
Group vya rejareja vya petroli.
NBC
imetiliana saini ya mkopo wa shilingi za kitanzania bilioni 100 na
kampuni ya kusambaza mafuta ya jijini Dar es Salaam, Star Oils Ltd
katika mpango mkakati wa kuendeleza sekta ya mafuta nchini.
Picha
juu na chini ni Baadhi ya wafanyakazi wa makampuni ya MeTL GROUP na
Benki ya NBC waliouhudhuria hafla hiyo ya utiliaji saini wa mkopo baina
MeTL na NBC.
Mkurugenzi
Mtendaji wa NBC, Bi. Mizinga Melu na Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP,
Mhe Mohammed Dewji wakitiliana saini ya mkopo huo wa bilioni 100 za
kitanzania.
Makamu
wa Rais wa Makampuni ya MeTL GROUP, Vipul Kakad (wa pili kulia
walioketi) na Mkuu wa Idara- Huduma za Kibenki kwa Wateja wakubwa na
Uwekezaji wa NBC, Andre Potgieter wakiweka saini zao kwenye mkataba huo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa NBC, Bi. Mizinga Melu na Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP,
Mhe Mohammed Dewji wakibadilishana hati za mkopo huo katika hafla
iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja baina ya MeTL GROUP na NBC baada ya utiliaji saini wa mkopo huo.
Kutoka
kushoto ni Mkuu wa Idara- Huduma za Kibenki kwa Wateja wakubwa na
Uwekezaji wa NBC, Andre Potgieter, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Bi.
Mizinga Melu, Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP, Mhe Mohammed Dewji,
Makamu wa Rais wa MeTL GROUP, Vipuk Kakad na Afisa Mtendaji Mkuu wa
kampuni dada ya MeTL GROUP Star Oils Ltd, Nazir Haji kwenye picha ya
pamoja.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni dada ya MeTL GROUP Star Oils Ltd, Nazir Haji akitoa shukrani zake kwa NBC.
Makamu
wa Rais wa Makampuni ya MeTL GROUP, Vipul Kakad (katikati) na wasaidizi
wa Mheshimiwa Mohammed Dewji kwenye hafla hiyo iliyofanyika mwishoni
mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP, Mhe Mohammed Dewji akimwonyesha kitu
kwenye simu yake ya kiganjani Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Bi. Mizinga
Melu wakati wa hafla hiyo.
Wafanyakazi wa NBC na MeTL Group wakibadilishana mawazo wakati wa hafla hiyo.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP, Mhe. Mohammed Dewji (wa pili kushoto),
Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Bi. Mizinga Melu (kulia), Mwanasheria Mkuu
wa MeTL GROUP, Zakia Riyaz Ali (wa pili kulia), na Vikash KG wa Star
Oils Ltd wakati wa hafla hiyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP, Mhe Mohammed Dewji akifurahi jambo na mmoja wa wafanyakazi wa NBC wakati wa hafla hiyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP, Mhe Mohammed Dewji akiteta na wafanyakazi wa NBC kwenye hafla hiyo.
KWA NAMNA HII MADEREVA WATAENDELEA KUUA ABIRIA
Basi
la kamwana express likilipita lori kwa mwendo kasi karibu na eneo la
Chalinze mkoani Pwani huku dereva huyo akijua sheria za bararani kuwa ni
marufuku kulipita gari nyingine na anajua wazi kuwa mbele kuna gari
inakuja . Hutua hii inasababisha kukosekana kwa usalama wa abiria na
raia kwa ujumla. Picha na Benjamin Sawe Wizaraya Habari.