Pages

KAPIPI TV

Friday, July 25, 2014

MKUTANO KATI YA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM NA WANAMTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA NA TAMWA

 Doreen E. Maro kutoka TAMPRODA ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba akiwakilisha Wafugaji Akileta Mrejesho wa walichokuwa wakikijadili katika Kundi lao juu ya mapendekezo ya kuimarisha Masuala muhimu ya Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya
 Dkt. Macca A. Mbalwa  Mkurugenzi wa Giyedo Tanzania akiwa anatoa Mrejesho wa kile ambacho walikuwa wamekijadili na kutoa mapendekezo yao ya Kuboresha masuala muhimu katika Rasimu ya pili ya Katiba Mpya.
 Salama Aboud Talib Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba  na Naibu Katibu Mkuu wa UWT akizungumzia makosa mbalimbali ambayo yapo katika Rasimu ya Pili ya Katiba mpya na kutoa mapendekezo kuwa Iboreshwe ili kuweka usawa.
 Executive Director wa  Women Fund Tanzania Mary Rusimbi akizungumza juu ya Majumuisho ya pomoja na Kupanga mikakati ambayo yatasaidia Kuimarisha Masuala Muhimu ya Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya
 Mgeni Hassan Juma Mwenyekiti wa Wawakilishi  Wanawake Zanzibar akitoa neno la Shukurani kwa wote waliohudhuria kwa muda wa siku mbili katika mkutano wa Wajumbe wa Bunge Maalum la  Katiba, Mtandao wa wanawake na TAMWA
 Profesa Ruth Meena  Akitoa Majumuisho pia kutoa Shukurani kwa wale wote waliohudhuria katika Mkutano huo uliochukua siku mbili.
 Valerie Msoka akifunga Rasmi Mkutano huo.
 Fredrick Msigala Mjumbe Bunge Maalum la Katiba ambaye ni Mlemavu wa Miguu akielezea masikitiko yake ya Jinsi watu wenye ulemavu wakiwemo wanawake na wanaume ambavyo wametengwa na kukosa haki zao, amesisitiza Serikali katika Rasimu Mpya ya Pili ya Katiba wawaangalie walemavu kwa umakini na ukaribu maana wanahaki sawa na watu wengine. Pia amesisitiza walemavu wajaliwe katika huduma za Afya mana ni Muhimu kwao. Mwisho amesisitiza kuwa wanawake wenye ulemavu wanahaki ya Kuolewa na kuto nyanyaswa pindi wanapokuwa katika ndoa zao.
 Modesta Mpereme ambaye ni Kiziwi hasikii lakini anaongea vizuri pia ni Mwenyekiti kutoka  Sauti ya Wanawake  wenye Ulemavu Tanzania, Ameiomba serikali iwe na vitendea kazi vya kutosha ambavyo vitawasaidia walemavu katika secta mbalimbali Mfano katika Mabenki kuwe na vifaa maalum vya kuwasaidia walemavu, Katika Upande wa Afya amesisitiza kuwe na hata watu wanaoweza kutoa msaada wa kutafsiri mambo mbalimbali mfano kwa Viziwi, wasio ona na ambao Hawawezi kuongea.
 Siti Ally Mwanasheria na Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutoka Zanzibar akisisitiza umuhimu wa usawa kati ya haki za wanawake na wanaume katika jamii , Pia alisisitiza juu ya mabinti wanaopata Mimba za utotoni wakiwa mashuleni na kusisitiza kuwa wanaruhusiwa kusimama masomo mpaka kipindi mtoto atakapokuwa mkubwa anaruhusiwa kuendelea na masomo,  Mwanaume aliyesababisha Mimba anaweza akashtakiwa .
 Baadhi ya Wajumbe wa Bunge Maalum la katiba pamoja na Wadau mbalimbali waliofika katika Mkutano huo.
 

RAIS KIKWETE AMUAPISHA JAJI KIONGOZI WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA


PIX01
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete akimuapisha Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila leo jijini Dar es Salaam.Picha zote na Frank Shija- MAELEZO
PIX02
Jaji Kiongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jaji Shaban Ally Lila (kulia) akitia saini hati ya Kiapo mbele ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa hafla ya kuapishwa kwake leo jijini Dar es Salaam. Katikati mwenye miwani Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akishuhudia tukio hilo.
PIX03
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini hati ya Kiapo cha Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila wakati wa hafla ya kuapishwa kwa jaji huyo leo jijini Dar es Salaam.
PIX04
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi hati ya Kiapo Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila wakati wa hafla ya kuapishwa kwa jaji huyo leo jijini Dar es Salaam.
PIX05
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue(kushoto) akimpongeza Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila mara baada ya kuapishwa rasmi kushika wadhifa huo katika hafla iliyofanyika Ikulu leo jijini Dar es Salaam.
PIX06
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Majaji wa Mahaka Kuu Tanzania mara baada ya kuapishwa rasmi kushika wadhifa huo katika hafla iliyofanyika Ikulu leo jijini Dar es Salaam.Kushoto kwake ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman

MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA 25 JULAI, 2014

SERIKALI YAPOKEA MABEHEWA 25 YENYE THAMANI YA SH.BILIONI 4.3 KUTOKA INDIA

Waziri wa Uchukuzi Dk.Harrison Mwakyembe (katikati), akifurahia jambo wakati wa kupokea mabehewa hayo. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TRL, Mhandisi Kipalo Kisamfu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk.Shaaban Mwinjaka.
Mkurugenzi Mkuu wa TRL, Mhandisi Kipalo Kisamfu (mwenye tai kushoto),akimuelekeza jambo Waziri Mwakyembe.
Waziri Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari wakati akipokea mabehewa hayo.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (PTA) na wa TRL wakishusha toka katika meli moja ya mabehewa hayo.
Baadhi ya wanahabari waliokuwepo kwenye hafla hiyo.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (PTA) na wa TRL wakishusha toka katika meli moja ya mabehewa hayo.
Waziri Mwakyembe akiangalia moja ya mabehewa hayo.
Baadhi ya mabehewa hayo yakiwa yamepangwa katika njia yake bandarini baada ya kushushwa kutoka katika meli.
Fundi wa Shirika la Reli Tanzania , Ephrahim Joel akikaza nati ya moja ya mabehewa hayo.
Fundi wa Shirika la Reli Tanzania , Francis Mpangala naye akikaza nati katika moja ya mabehewa hayo. (Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com.
………………………………………………………………
Na Dotto Mwaibale
 
SERIKALI imepokea mabehewa 25 mapya ya kubebea kokoto yenye thamani ya sh.bilioni 4.316 kwa ajili ya Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kutoka Kampuni ya M/S Hindusthan Engineering and Industriles Limited ya India.
 
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kupokea mabehewa hayo Dar es Salaam jana, Waziri wa Uchukuzi Dk.Harrison Mwakyembe alisema mabehewa hayo ni sehemu ya mpango kabambe wa Serikali wa kufufua Kampuni ya Reli Tanzania chini ya mapngo wa Tekeleza kwa Matokeo Makubwa sasa (BRN).
 
Alisema mpango wa BRN kwa Kampuni ya Reli Tanzania umelenga kuiwezesha kampuni hiyo kiutendaji ili iweze kusafirisha tani milioni 3.0 ifikapo mwaka 2016 kutoka tani 200,000 zilizosafirishwa mwaka 2012 kupitia Reli ya kati.
 
“Katika harakati za kufikia malengo haya makubwa, Serikali kupitia bajeti zake za mwaka 2012/2013 na 2014, ilitenga fedha kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali iliyolenga kuboresha vitendea kazi vya Kampuni ya Reli Tanzania” alisema Mwakyembe.
 
Alitaja miradi iliyopangwa ni pamoja na kujenga upya vichwa vya Treni 8, kununua vinchwa vya treni vipya 13, mabehewa mapya 274 ya kubebea mizigo na mabehewa ya breki.
 
Mwakyembe alitaja mradi mwingine ni kununua mashine ya kushindilia kokoto, kununua mabehewa 22 mapya ya abiria na kununua mabehewa 25 mapya ya kubebea kokoto ambayo yamepokelewa jana.
 
Katika hatua hiyo Mwakyembe ametumia fursa ?hiyo kuipongeza TRL kwa kupokea mabehewa hayo kwa wakati na kuishukuru Kampuni ya Hindusthan Engineering and Industries Limited ya India kwa utengenezaji wa mabehewa hayo kwa muda uliopangwa.
 
Alisema lengo ni kuiwezesha TRL kufikia malengo ya kusafirisha mizigo tani 3.0 na kutembeza treni za abiria tano kwa wiki ifikapo mwaka 2016.

WANANCHI NA JWTZ WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA TABORA

Baadhi ya askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania wakifyatua risasi hewani kama ishara ya kumbukumbu ya Mashujaa katika maadhimisho yaliyofanyika Tabora mjini kwenye Mnara wa kumbukumbu ya uamuzi wa Busara.
Baadhi ya makamanda wa JWTZ wakitoa heshima wakati wa maadhimisho ya Mashujaa Tabora mjini.

Mkuu wa wilaya ya Sikonge Bi.Hanifa Selengu akiweka Ngao na mkuki kama ishara ya Serikali kukumbuka mchango wa mashujaa waliopambana katika vita mbalimbali.
Baadhi ya makamanda wa JWTZ,Polisi na Magereza walihudhuria katika maadhimisho hayo.

Mkuu wa wilaya ya Sikonge Bi.Hanifa Selengu akihutubia katika maadhimisho hayo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Tabora.
Baadhi ya wananchi wakiwemo wafanyabiashara ambao walilazimika wafunge shughuli zao kushiriki maadhimisho ya Mashujaa.





WAHANGA WA VITA WANENA-KIGOMA

Mkuu wa wilaya ya Kigoma Bw.Ramadhani Maneno  akiweka Ngao na mkuki kama ishara ya kuwakumbuka Mashujaa katika maadhimisho mkoani Kigoma
Mkuu wa wilaya ya Kigoma Bw.Ramadhani Maneno akiingia katika eneo lililotayarishwa kwa ajili ya Maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa mkoani Kigoma.
Baadhi ya makamanda wa JWTZ na wananchi wakiwa tayari katika maadhimisho ya kumbukumbu mkoani Kigoma
Gwaride rasmi katika maadhimisho ya Mashujaa.
 Na Magreth Magosso,Kigoma

WAHANGA waliopigana vita mbalimbali hapa nchini waishio Mkoa wa Kigoma,wamewataka vijana wazingatie nidhamu,uaminifu na kujiepusha kudharau matabaka ya jamii yaliyopo ,kwa lengo la kulinda taifa kwa maslai ya kizazi cha leo na siku zijazo.
 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti  wahanga hao,kigoma ujiji  jana katika  kuenzi  siku ya kurudi nchini hapa kwa mashujaa waliopigana vita  mbalimbali ikiwemo ya  Uganda,msumbiji,Botswana ,vita vya kijadi na nyinginezo walisema walifanikisha hayo kwa kuzingatia nidhamu ,uaminifu kwa kujitolea  kupigania haki za wananchi husika.
 
Inspekta Mstaafu Jeshi la magereza Juliana Stephana na  Kamishna mstaafu Lt.Joseph Nyamkuzwa walisema  wananchi kwa ujumla hawana budi kumcha mungu ili kudumisha  upendo, ambao ni chachu ya kuthubutu kulinda maliasili na kutoa taarifa   za uvunjifu wa amani  iliyopo.
 
Na Lt. kanali mstaafu Raphael  Kakwila alisihi wazazi watoe elimu njema kwa vijana wao,ili waishi kwa nidhamu bora yenye ushawishi wa kuwajengea uwezo wa kizalendo ambao ni tija ya kuzuia uhalifu kwa maslai ya jamii lengwa.
 
Kwa upande wa mgeni rasmiambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya hapa, Ramadhan Maneno kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huoLt.mstaafu Issa Machibya alisema,siku hiyo ni chachu kwa jamii kutambua thamini  ya amani iliyopo.
 
“majirani zetu hawapendi kuona taifa linarithi amani tuliyoachiwa wahanga hawa walitoa damu na jasho kupigania haki za msingi na taifa sasa vijana ni wakati wenu kulinda nchi kwa kujiepusha na matukio ya uvunjifu wa utulivu,amani kwa kuwabainisha wahalifu” alianisha Maneno.
 
Alisema walitumia  zana  duni za kivita  lakini kutokana na uzalendo walionao walijitoa kwa dhati   kupigania maslai ya taifa ili kuipa nchi  heshima .huku awaasa wananchi watoe taarifa kwa vyombo vya usalama ili kudhibiti majanga ya uhalifu.
 
Aidha Shekhe Mkuu  Bakwata wa hapa Hassan Iddi  alisema wanasiasa,wananchi na viongozi wa dini wanajukumu la kuelimisha waumini wao juu ya faida ya amani na athari zake,kwa lengo la kuboresha ustawi wa umaa.
 
Akizungumzia utata Rasimu mpya ya katiba Shekhe Iddi alionya wanasiasa waache utashi wa maslai  binafsi na badala yake wanzingatie  misingi bora  ya wahanga waliothubutu  kufa ili kutetea umaa husika.

Thursday, July 24, 2014

SERIKALI YASAINI MIKATABA MIWILI YA UJENZI WA BARABARA ZA JUU KWA JUU


1 (4)Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada (kulia) wakibadilishana hati ya makubaliano ya mikataba miwili ya ujenzi wa barabara za juu kwa juu katika makutano ya TAZARA na usambazaji umeme jijini Dar es salaam leo zenye thamani ya zaidi ya bilioni 128.
2 (4)Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada (kulia) wakisaini hati ya makubaliano ya mikataba miwili ya ujenzi wa barabara za juu kwa juu katika makutano ya TAZARA na usambazaji umeme jijini Dar es salaam leo zenye thamani ya zaidi ya bilioni 128.
3 (4)Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (kushoto) akionyesha michoro ya itakavyonekana barabara za juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam leo wakati wa kusaini hati ya makubaliano ya miradi miwili zenye thamani ya zaidi ya bilioni 128 na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada (kulia).
Picha na Eleuteri Mangi- MAELEZO -Dar