Pages

KAPIPI TV

Thursday, March 8, 2018

MBUNGE VITIMAALUM MUNDE TAMBWE AMEWASAIDIA WANAWAKE MIAMOJA KADI ZA MATIBABU NA MIFUKO MIAMBILI YA SARUJI KWA AJILI YA UJENZI MABWENI,ZAHANATI

Mbunge wa Vitimaalum mkoa wa Tabora Munde Tambwe akizungumza katika Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wanawake zilizofanyika kimkoa mkoani Tabora,katika maadhimisho hayo Munde aliwalipia  Kadi za matibabu maarufu TIKA Wanawake wasio na uwezo Miamoja wanaoishi manispaa ya Tabora akiwa anakamilisha idadi kama hiyo kwa Wanawake wengine mia moja kwa kila Wilaya za mkoa wa Tabora ambazo ni wilaya saba.
Munde akikabidhi jumla ya shilingi milioni moja kwa Mke wa Rais mstaafu wa awamu ya nne Mama Salma Kikwete kwa ajili ya kulipia Kadi hizo miamoja za matibabu kwa Wanawake wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu Manispaa ya Tabora.
Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete akimpongeza Mbunge wa Vitimaalum mkoa wa Tabora Munde Tambwe baada ya kupokea kiasi cha shilingi milioni moja kwaajili ya TIKA huku Mbunge huyo Munde Tambwe akiahidi mbele Mama Salma Kikwete kuchangia jumla ya mifuko Miambili   ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Mabweni katika Shule za Sekondari za kata manispaa ya Tabora na ujenzi wa uzio Kliniki ya Tabora mjini maarufu Town Clinic.

Mke wa Rais mstaafu wa awamu ya nne Mama Salma Kikwete akizungumza katika maadhimisho hayo ambapo  alisema kuna haja ya kuleta mabadiliko ya kisekta yatakayoharakisha   maendeleo kwa Wanawake kupitia kujenga misingi imara ya kupata elimu bora itakayotoa fursa  kwa  Wanawake  kuajiriwa na hata kujiajiri wenyewe.
Maadhimisho  ya Siku ya wanawake duniani mkoani Tabora ambapo Mama Salma Kikwete alikuwa mgeni rasmi iliyofanyika viwanja vya Chipukizi mjini Tabora.
Mkuu  wa mkoa wa Tabora  Aggrey Mwanry akiungana na Wanawake mkoani Tabora kuadhimisha siku hiyo ya Wanawake duniani
Gwiji na Msanii mkongwe wa muziki wa Taarabu nchini Malkia Khadija Kopa akitumbuiza katika maadhimisho hayo mjini Tabora katika viwanja vya Chipukizi.
Wanawake wajasiliamali wakiadhimisha siku yao wakati muziiki wa taarabu ukitumbuizwa na Malkia Khadija Kopa.






No comments: