Pages

KAPIPI TV

Tuesday, December 12, 2017

TIGO YAZINDUA DUKA LA KISASA URAMBO IKIWA NI MUENDELEZO WA KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA WAKE

Mgeni rasmi  Katibu Tawala Wilaya  ya Urambo  Bw.Paschal  Byemelwa  akikata  utepe  ikiwa  ni  Uzinduzi wa Duka la Kisasa la Kampuni ya Simu za kiganjani ya Tigo wilayani Urambo katika kutekeleza adhma ya kusogeza karibu huduma za mawasiliano kwa wananchi wilayani humo,Kutoka kulia ni Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Urambo Bi.Margareth Nakainga,wapili kulia ni Meneja wa Tigo kanda ya Ziwa Bw.Gwamaka Mwakilembe,na wa kwanza kushoto ni Meneja wa Tigo mkoa wa Tabora  Bw.Bright Kisanga.

Duka la kisasa la Huduma kwa Wateja wa Tigo Wilayani Urambo

Mgeni Rasmi  Paschal  Byemelwa,kulia ni Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Urambo Bi.Margareth Nakainga,wapili kutoka  kulia ni Meneja wa Tigo kanda ya Ziwa Bw.Gwamaka Mwakilembe,na wa kwanza kushoto ni Meneja wa Tigo mkoa wa Tabora  Bw.Bright Kisanga wakipiga makofi kushangilia tukio la kutaka utepe kama ishara ya Uzinduzi wa Duka hilo la Kisasa wilayani Urambo.

Picha ya pamoja baada ya Uzinduzi wa Duka hilo
Mmoja kati ya maafisa wa Tigo  Bi.Tunu Kazinja  akitoa maelezo kwa huduma ambazo wanazitoa mara baada ya uzinduzi wa Duka hilo la Kisasa wilayani Urambo.

Mgeni Rasmi  Katibu Tawala wilaya ya Urambo Paschal Byemelwa pamoja na wageni wengine waalikwa katika hafla fupi ya uzinduzi wa Duka hilo la kisasa,walipata fursa ya kuangalia bidhaa mbalimbali za Tigo ambazo zilikuwa zikioneshwa nje ya Duka hilo la Kisasa.
Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Urambo wakipata maelezo ya huduma zinazotolewa na Kampuni ya Tigo katika moja ya Banda la maonesho wakati wa hafla fupi ya Uzinduzi wa duka la Kisasa wilayani Urambo.

Katibu Tawala wilaya ya Urambo Bw.Paschal Byemelwa akihutubia wakati wa Uzinduzi wa duka la Tigo  wilayani Urambo ambapo ameishukuru kampuni ya Tigo kwa kufungua Duka hilo la Kisasa ambalo amesema litasaidia kuwapunguzia adha kubwa wananchi wa Urambo ambao walikuwa wanalazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma. 
Baadhi ya wananchi wa Urambo wakimsikiliza katibu tawala wilaya ya Urambo Bw.Paschal Byemelwa wakati akiwahutubia katika hafla fupi ya uzinduzi wa duka hilo la kisasa.
Meneja wa kanda ya ziwa wa Tigo Bw.Gwamaka Mwakilembe akizungumza na wananchi wa Urambo wakati wa uzinduzi wa Duka la kisasa wilayani humo ambapo alieleza kuwa kampuni ya Tigo  ambayo inaongoza kwa mageuzi ya kidigital nchini imeamua kuzindua duka hilo ikiwa ni muendelezo wa juhudi zake kuboresha huduma kwa wateja wake.




No comments: