Pages

KAPIPI TV

Sunday, December 21, 2014

TIGO YATOA MSAADA HOSPITALI YA WILAYA YA URAMBO

Mkurugenzi wa kampuni ya Simu za mkononi ya Tigo kanda ya Ziwa Bw.Ally Maswanya akikabidhi msaada wa vifaa vya hospitali  kwa  Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Urambo Dr.Heri  Kagya  vifaa hivyo ni pamoja na  magodoro 35,Shuka 35 na Blanketi 35 ikiwa ni sehemu ya Kampuni ya Tigo kurejesha  fadhila kwa wananchi ambao ni watumiaji wa mtandao huo.
Mkurugenzi wa Tigo kanda ya ziwa Bw.Ally Maswanya akizungumza kabla ya kukabidhi msaada huo wa vifaa vya hospitali ambapo aliahidi Kampuni ya Tigo itatoa msaada wa vyandarua zaidi ya mia mbili ili viweze kusaidia katika Wadi mbalimbali husasni ya akina mama wajawazito.
Meneja wa Tigo mkoa wa Tabora Bw.Brite Kisanga akizungumza dhamira ya kampuni ya Tigo kutoa msaada huo kwa hospitali ya wilaya ya Urambo.
Mkurugenzi wa kampuni ya Tigo Bw.Ally Maswanya akikabidhi msaada wa mashuka 35 kwa Mganga Mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Urambo.(Picha na KAPIPIJhabari.COM)




No comments: