Pages

KAPIPI TV

Tuesday, December 16, 2014

ACT KUMBURUZA MKURUGENZI MAHAKAMANI -KIGOMA

Na Magreth Magosso Kigoma.

UONGOZI  wa chama cha Alliance for change and Transparency (ACT) mkoa wa Kigoma umeahidi kuifikisha ofisi ya mkurugenzi wa wilaya ya Kigoma mahakamani endapo hatua za maksudi hazita chukuliwa kunusuru  uchaguzi wa Kata ya Kagunga uliositishwa wakati wa uchaguzi.

Kauli hiyo imekuja baada ya  Msimamizi msaidizi aliyejulikana kwa jina moja la Mtisi kuiandikia barua chama cha ACT wametolewa katika uchaguzi huo kutokana na makosa mbalimbali katika kujaza fomu husika.

Akifafanua  hilo nje ya ofisi ya mkuu wa wilaya ya kigoma Ramadhan Maneno alisema hujuma imepangwa baina ya chama tawala na ofisi ya mkurugenzi kwa kushirikiana na mwanasheria wa halmashauri husika kwa mujibu wa barua ya siri walioikamata ndani ya ofisi ya usimamizi wa uchaguzi.

Alisema awali baada ya kupata barua hiyo Novemba 28 mwaka huu uongozi wa chama hicho  ulikata rufaa ambapo kwa mujibu wa kamati ya rufaa ya wilaya ulitupilia mbali rufaa hiyo kwa kuwa ilikuwa nje ya muda wa kupokea rufaa.

Rufaa haikusikilizwa na chama hicho kilitolewa katika orodha ya vyama vitakavyopigiwa kura katika kijiji cha Zashe Kata ya Kagunga wilaya ya Kigoma ambapo kitendo hicho kilizua hamaki kwa wananchi na  uchaguzi kuhairishwa kwa hila za watu wachache.

Kwa nyakati tofauti wakielezea kwa uchache Mkurugenzi wa wilaya Michael Mwandezi na Mwanasheria wake Idd Ndabhona walisema mchakato wa upigaji kura una dosari nyingi na kushauri vyama vya upinzani wachukue hatua za kisheria.

No comments: