WAFUGAJI wanaoishi kijiji cha Minyinya Kata ya
Nyamtukuza wilaya ya Kakonko Mkoa wa Kigoma,wamewashambulia Baba na mtoto kisha kuwachoma moto hadi kufa kwa madai ya kuwaamuru waoneshe walipo majambazi walioua Mfugaji wa ng'ombe katika tukio la Octoba ,15,2014.
Akielezea tukio hilo Mwenyekiti wa kijiji cha Minyinya Justini
Kilegea alisema tukio hilo ni la kulipiza kisasi kwa wakulima ambapo
wafugaji walihisi waliovamia na kuua mwenzao wiki iliyopita alitoka katika
jamii ya wakulima hivyo walitaka waoneshe waliofanya tukio hilo jambo ambalo lilizua tafrani na kuanza kushambuliwa hatimaye kuwaua.
“sasa usiku wa Octoba ,19 kuamkia 20,mwaka huu ndipo
wafugaji walivamia nyumba za wakulima zipo
hukohuko mashambani na kuzichoma moto na hatimae kumuua mtu na mwanae
Kachila Kahegele (48) na Lameck Kahegele (26) .
Baadhi ya wakazi wa kijiji hicho Daniel Paulo ,Jonas Matwa
na Silace Kahebela walidai mwenyekiti wa kijiji hicho ndio chanzo cha mauaji
baina ya wafugaji wageni na wakulima ,ambapo hugawa ardhi kinyemela ,bila kushirikisha
wananchi ,hatua ambayo imekuwa ni chanzo na chokochoko za mapigano baina ya pande hizo mbili.
Kwa upande wa Mkuu wa wilaya ya Kibondo Venance Mwamoto
alisema wafugaji hao walifika hapo wakisaka madini na walipokosa walianzisha
kilimo na ufugaji wa ngombe ukashamiri
na hatimaye wakanzisha kijiji hali iliyowavutia wakazi wa Minyinya kuhamia huko
mashambani na 15,Octoba,2014 miongoni mwa wakulima waliua mfugaji mmoja.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kigoma Jafari Mohamed alipoulizwa juu ya mauwaji hayo ,alisema
yupo nje ya mkoa ,hivyo hajapewa taarifa ya tukio hilo na kusisitiza kuwa kila raia
anawajibu wa kutii sheria bila shuruti hata kama alionewa akithibitika
anawajibika katika vyombo vya dola.
No comments:
Post a Comment