Pages

KAPIPI TV

Tuesday, October 21, 2014

AIRTEL YAZINDUA WIKI YA RASILIMALI WATU KWA WAFANYAKAZI WAKE


DSC_6938
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel  Tanzania Bwn Sunil Colaso akiongea na wafanyazi wakati wa uzinduzi wa wiki ya Rasimali watu uliofanyika katika Ofisi za makao makuu ya  Airtel ambapo wafanyakazi watapata fulsa ya kupata elimu juu ya sera kuhusu mafao mbalimbali na haki yaoza kimsingi  na huduma nyinginezo zinazotolewa na kusimamiwa na kitengo cha Rasilimali  watu, hafla ya uzinduzi huo imefanyika katika ofisi za Airtel Moroko leo HR group photo 2Baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha rasilimali watu cha Airtel Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja  wakati wa uzinduzi wa wiki ya Rasilimali watu iliyozinduliwa  rasmi jana katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar es saalam, IMG_6107wafanyakazi wa Airtel wakifatilia uzinduzi wa  uzinduzi wa wiki ya Rasilimali watu iliyozinduliwa  rasmi jana katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar es saalam
PIC 2Mkurugenzi wa Kitengo cha Rasilimali watu Airtel  Tanzania Patric Foya akiongea wakati wa uzinduzi wa wiki ya Rasimali watu uliofanyika katika Ofisi za makao makuu ya  Airtel ambapo wafanyakazi watapata fulsa ya kupata elimu juu ya sera kuhusu mafao mbalimbali na haki yao
za kimsingi  na huduma nyinginezo zinazotolewa na kusimamiwa na kitengo cha Rasilimali  watu, hafla ya uzinduzi huo imefanyika katika ofisi za Airtel Moroko leo Pic 4Mchekeshaji na mshereheshaji  maarufu kama MC Pilipili  akitoa burdani kwa wafanyakazi wa Airtel wakati wa uzinduzi wa wiki ya Rasimali watu iliyozinduliwa mahususi kwa wafanyakazi wa Airtel kupata elimu juu ya sera na huduma mbalimbali zinazotolewa na kusimamiwa na Kitengo cha Rasilimali watu, hafla ya uzinduzi huo imefanyika katika ofisi za
Airtel Moroko leo
pIC 5Wafanyakazi wa Airtel wakifurahia burdani toka kwa Mchekeshaji na mshereheshaji  maarufu kama MC Pilipili  wakati wa uzinduzi wa wiki ya Rasimali watu iliyozinduliwa mahususi kwa wafanyakazi wa Airtel kupata elimu juu ya sera na huduma mbalimbali zinazotolewa na kusimamiwa na Kitengo cha Rasilimali watu, hafla ya uzinduzi huo imefanyika katika
ofisi za Airtel Moroko leo
…………………………………………………….
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua rasmi wiki ya Rasilimali watu itakayowawezesha wafanyakazi wake kupata elimu kuhusu Sera  na  huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wafanyakazi na kusimamiwa na kitengo cha Rasillimali watu kwa lengo la kuwaongezea wafanyakazi ufanisi zaidi wa kuhudumia wateja

Airtel imeandaa wiki hiyo ya rasilimali watu katika nchini zote Afrika ambapo Airtel inafanya biashara zake na kuzinduliwa rasmi leo nchi Tanzania, airtel imefanya hivyo leo  ikiwa ni muda mfupi tu tangu ilipoadhimisha  wiki ya huduma kwa wateja inayoadhimishwa duniani kote ambapo airtel ilishiriki katika maadhimisho hayo .

Akiongea wakati wa uzinduzi huo Mkurugenzi  wa kitengo cha Rasilimali watu Bwana Patrick Foya alisema”  Tunategemea kuwa na wiki yenye mafanikio ambayo itawawezesha wafanyakazi wetu kupata ufafanuzi juu ya maswala mbalimbali yanayohusu sera na  haki zao za msingi kama wafanyakazi wa Airtel. 

Sambamba na hilo tutakuwa na watoa huduma kutoka kwenye makampuni mengine wakiwemo strategies inayotoa huduma za bima ya afya, NSSF  inayotoa mikopo ya nyumba na mafao kwa wafanyakazi
 na makapuni mengine mengi  ambayo yatatoa fulsa ya wafanyakazi wetu
kupata elimu zaidi kuhusu huduma hizi muhimu na jinsi yakufaidika nazo hii ni fulsa kwa wafanyakazi wetu nasi tuko tayari kuwafikishia wote ili kuongeza ufanisi kazini”.

Natoa wito kwa wafanyakazi kujitokeza katika sehemu maalumu zilizoandaliwa kutoa huduma na kupata mambo mazuri tuliyowaandalia wiki nzima alingoza Foya

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bwana Sunil Colaso aliwashukuru wafanyakazi wa kitengo cha rasilimali watu kwa kujipanga vyema kwa wiki hii na kusisitiza kuwa elimu na mafunzo haya ni mwendelezo wa mpango mkakati wa kuhakikisha kuwa wafanya kazi wote wanajua mambo muhimu yanayotokana na ajira zao, sera mbalimbali kama vile za afya na zile zinazogusa maslahi yao’.
Colaso alisema “ natoa wito kwa wafanyakazi kutumia wiki vyema na kuuliza mswali mengi yatakayo toa ufafanuzi wa maswala wanayohitaji elimu  na uelewa zaidi.

No comments: