Pages

KAPIPI TV

Saturday, October 25, 2014

NAIBU WAZIRI ELIMU NA MAFUNZO JENISTA MHAGAMA ANENA - KIGOMA

JENISTA MHAGAMA -KIGOMANa Magreth Magosso,Kigoma

Naibu Waziri wa  Elimu  na  Ufundi Jenista Muhagama ashauri Uongozi wa  shule ya Sekondari ya Mwilamvya ifungue kitengo cha ushauri nasaha shuleni hapo, ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa maadili  kwa wanafunzi husika.
 
Kauli hiyo imetokana na risala iliyosomwa jana na Mkuu wa shule Emmanuel  King  katika mahafali ya Darasa la saba na kidato cha Nnne yaliyofanyika  shuleni hapo ambayo ipo katika  kata ya murusi wilayani Kasulu Mkoa wa Kigoma.
 
Akifafanua hilo kwa niaba ya Naibu  husika,Mkaguzi wa shule Kanda magharibi Adriani Mlelwa alisema   utandawazi ni chanzo cha madili kwenda mlama , shida ipo katika mapokeo huku ashauri wafungue kitengo hicho,  ili kudhibiti maadili  na nidhamu kwa wanafunzi.
 
“mawasiliano ni muhimu , wekeni taratibu,kanuni na sheria itasaidia kudhibiti wanafunzi kumiliki simu za mkononi holela,mnaweza mkawa na simu moja ambayo mzazi ataongea na kijana  ” alisema Mlelwa.
Ampongeza mtendaji wa shule Elias Maliyatabu kwa kitendo cha kutumia rasilimali mali na akili katika kuwekeza  elimu mkoani kigoma , ni mtendaji wa kwanza wa hapo mwenye tija ya kufuta ujinga kwa wakazi husika.

Wigo mpana wa kushirikisha  na ushawishi kwa wadau ni chachu ya kuboresha  vitendea kazi  hasa mabara ya kisasa  ni moja ya sifa ya wanafunzi kufuta  alama ya sifuri katika  mtihani wa taifa na kanda  tangu ianzishwe  2005.

Akijibia hilo Mkurugenzi Maliyatabu alisema mafaniko yanatokana na wazazi ambao wanaufahamu  wa tija ya elimu kwa mtoto ,ambapo ni urithi bora wa kushinda adui ujinga na umaskini siku za usoni.
Baadhi ya wanafunzi wahitimu Elimina Segenya na Inocent Batholomeo kwa nyakati tofauti walisema umiliki wa simu kwa wanafunzi chanzo cha kukosa umakini katika masomo.

Waomba wazazi wasiwape simu vijana na kutaka uongozi wa shule uweke utaratibu wa kuweka  watoa huduma ya chakula  zaidi ya mmoja  ili kuboresha uwajibikaji.

Pia Zaidi ya Milioni  Tatu zimetumika katika  ununuzi wa ng`ombe jike moja la maziwa na dume,vitenge doti 10,debe moja la dagaa wa hapa na Lita 20 mafuta ya mawese.

No comments: