Pages

KAPIPI TV

Tuesday, October 21, 2014

CHADEMA YAMPA SIKU 14 DC MANENO ZA UWAJIBIKAJI--KIGOMA

 
Na Magreth Magosso,Kigoma

MWENYEKITI wa chama cha (CHADEMA)  Mkoa wa kigoma Ally Kisala ametoa  siku 14  za uwajibikaji kwa  Mkuu wa wilaya ya Kigoma Ramadhan Maneno  endapo hatawadhibiti wanachama wa chama cha Alliance Transparency For Change(ACT)  kwa kitendo cha  utovu wa nidhamu ,madili,kwa mujibu wa  katiba ya Nchi.

Kauli hiyo ilitolewa jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Mwanga urusi uliokuwa ukiwataka wananchama wake waache kulumbana hoja na wanachama wa ACT  na kudai chama hicho kuwa ni SACCOS ya mtu mmoja ambaye analengo la kudhofisha vyama vya upinzani .

Chanzo cha kupewa siku 14 ni kutokana na sintofahamu  dhidi ya mgogoro wa  eneo la urusi ambapo awali kulikuwa na Bango la Chadema lililokuwa na wanachama wapatao 20,hatimaye wote wamejiunga   na ACT  na hivyo bango linatumika na ACT .

Hali iliyochangia Mkuu wa wilaya  hiyo  Ramadhan Maneno kuwapa amri wanachama  wa ACT na Chadema wasitishe huduma zao kutpitia bango hilo la Urusi  hadi suala litakapopatiwa ufumbuzi na vyombo vya dola.

“nitatumia nguvu ya watu ili kutimiza uwajibikaji kwa mkuu wa wilaya  itakuwaje walitumie wao na ndio maana Jeshi la Polisi wametoa bendera ya ACT lakini maneno anawabeba nitatumia nguvu ya umma ,damu itamwagika na wataokota maiti” alidai Kisala.

Katibu wa Chadema wilaya ya Kigoma  Frank Lucas alisema kwa miezi mitatu siasa ya kigoma imegubikwa na lugha chafu ambazo hazina  mashiko katika jamii,ilihali wanakabiliwa na adha mbalimbali na kuwaonya wasilumbane hoja na wananchama wa ACT kuanzia jana na kuendelea.

Akijibia hilo Mwenyekiti wa ACT Kigoma  Ibrahim Sendwe alisema siasa za kumwaga damu ni kawaida ya chadema na kudai suala hilo lipo mahakamani na Octoba ,27,2014 kesi itaanza kusikilizwa ,huku akionya Jeshi la Polisi waache kuingilia hoja za wanasiasa na kudai kitendo cha kuondoa bendera ya ACT ni kuidharau Mahakama.

Mbali na hilo uongozi wa chadema wametumia zaidi y ash.200,000 kwa kununua  katoni za juisi,matunda na sabuni za Gwanji na kuzigawa kwa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya maweni ,Huku Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo Fadhili Kibaya akiwaongoza katika wodi ya kina mama,watoto na kina baba ili kufanikisha ugawaji huo.

Mjumbe wa Uongozi wa Chadema  kanda ya Kati Taifa Alphonce Mbasa alisema wamejipanga kubadili mwelekeo wa siasa kwa kutoa  huduma  zitakazowafikia wananchi moja kwa  moja hasa kusaidia makundi tete likiwemo wagonjwa na yatima.

No comments: