Na Allan Ntana, Tabora
CHAMA
Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Tabora kimepata safu mpya
ya uongozi baada ya kufanya uchaguzi wake mkuu katika ngazi ya mkoa hapo
jana katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Ualimu Tabora.
Katika
mkutano huo wa uchaguzi nafasi zilizokuwa zinagombewa ni Mwenyekiti wa
CHADEMA Mkoa na Katibu wa Mkoa na Mwenyekiti na Katibu wa Baraza la
Vijana Chadema (BAVICHA), Baraza la Wanawake (BAWACHA) na Baraza la
Wazee.
Aliyeibuka
kidedea katika nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Tabora ni Bw.
Francis William Msyuka aliyepata kura 46 na kumshinda mgombea mwenzake
Bw.Hassan Said aliyepata kura 17 kati ya kura zote 66 zilizopigwa huku
kura 3 zikiharibika.
Na
aliyeibuka kidedea katika nafasi ya Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Tabora ni
Bw.Alinanuswe Mwakilima ambaye alipigiwa kura za ndio 57 na hapana 2
kati ya kura zote 61 baada ya kukosa mpinzani katika wajumbe wote
waliohudhuria mkutano huo.
Waliochaguliwa
kuongoza mabaraza ya chama hicho katika ngazi ya mkoa ni, BAVICHA,
Mwenyekiti ni Lazaro Damson na Katibu wake ni Daud Ndelwa, BAWACHA
Mwenyekiti ni Sada Kabezi na Katibu wake ni Anna Nyawacha na Baraza la
WAZEE Mwenyekiti ni Joseph Tanganyika na Katibu wake ni Vicent Ndeuka.
Msimamizi
wa Uchaguzi huo Christopher Nyamwanji ambaye ni Mratibu wa chama hicho
Kanda ya Magharibi aliwapongeza wajumbe wote waliohudhuria mkutano huo
kwa kufanikisha zoezi hilo la kikatiba ndani ya chama kwa utulivu na
amani huku akiwataka kukitumika chama hicho kwa moyo mmoja pasipo
kuruhusu roho za usaliti kama walivyofanya viongozi waliokuwepo.
Naye
diwani wa kata ya Bukene wilaya ya Nzega Omar Shehe kupitia chama hicho
ambaye alikuwa Mwenyekiti wa mkutano huo wa Uchaguzi aliwataka viongozi
hao kudumisha amani, mshikamano na uzalendo ndani ya chama hicho na
kujiepusha na makundi ili kuwaunganisha vizuri wanachama katika mkoa huo
hasa ikizingatiwa kuwa uchaguzi mkuu hauko mbali sana huku akiwaasa
kutogopa changamoto za hapa na pale.
Akitoa
shukrani zake Mwenyekiti mpya wa chama hicho Mkoa wa Tabora Francis
William Msyuka alisema kazi kubwa iliyoko mbele yake ni kutengeneza
mshikamano mzuri kwa viongozi wote na wanachama wa chama hicho kuanzia
ngazi ya shina, wilaya, jimbo na mkoa na kuhamasisha maendeleo katika
kila eneo husika sambamba na kukutana na wananchi ili kusikiliza kero
zao.
No comments:
Post a Comment