Pages

KAPIPI TV

Friday, August 1, 2014

WANANCHI WAMEASWA KUTOLINDANA KWA VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI-KIGOMA

 
 
Na Magreth  Magosso, Kigoma
 
WITO umetolewa kwa viongozi wa serikali za Vijiji  mkoani hapa,waache hulka ya kulindana dhidi ya wahamiaji haramu ,hali inayochangia jamii kuishi kwa kulipizana visasi.
 
Akizungumzia hilo Kamamda wa Polisi wa hapa Frasser Kashai alibainisha kuwa,Julai ,27 ,2014 saa 12.30 jioni , Elias Balandes (36) ambaye ni muhamiaji haramu wa kijiji cha Nyamidaho wilaya ya kasulu amemua mgambo kwa kile kinachodaiwa kulipa kisasi.
 
“alimuua askari mgambo Shaban Mabad(34) kisa kulipiza kisasi kwa mgambo huyo,kwa sababu zinazodaiwa kuwa alimfikisha kwa mwenyekiti wa kijiji mhamiaji  huyo kutokana na kuishi hapo kinyume cha sheria,lakini aliachiwa katika mazingira tata ” alisema Kashai.
 
Aliongeza kwa kusema siku hiyo wakiwa wanakunywa pombe za kienyeji  kilabuni katika  kijiji hicho,ndipo yalitokea marumbano baina ya marehemu na Balandes akishirikiana na Faustine Phidel(55) walimshambulia  mlengwa kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali chini ya ziwa la kushoto na kiganjani.
 
Kashai alisema marehemu alijikongoja peke yake hadi hospitali ya wilaya hiyo ambapo siku ya tatu aliaga dunia,watuhumiwa wanashikiliwa na Polisi kwa hatua zaidi.Wakati huohuo Mkurugenzi wa idara ya uhamiaji  Ebrosy Mwanguku alisema  changamoto ya uhamiaji haramu  kigoma ni kubwa ambapo baadhi ya  viongozi wa vijiji sio raia halali.
 
Mwanguku alibainisha kuwa,jamii  inalindana  yenyewe kwa yenyewe kutokana na mahusiano ya ukaribu wa kuoleana ,hali inayokwamisha operesheni ya uhamiaji haramu mkoani hapa na kusisitiza wananchi watajihukumu wenyewe kwa kuchezea amani iliyopo.
 
Akichangia hilo Katibu Taifa chama cha NRA Hamis Fadhili  akiri wananchi hutumia fursa za uchaguzi vibaya hasa kuwasimika viongozi  wahamiaji haramu kushika nyadhifa mbalimbali kama udiwani na watendaji wakuu wa vijiji,hali inayochangia kulindana baina ya wahamiaji  wanaoendelea kuja na viongozi husika.
 
Julai 12,mwaka huu  wahamiaji haramu 99 wakiwemo watoto  29 walio chini ya miaka 18 walikamatwa  katika operesheni ya  idara ya uhamiaji  mkoani hapa,ambapo wengi wao hutumiwa kama vibarua katika mashamba ya wananchi wa hapa.
 
Aidha changamoto hiyo inachangiwa na sheria dhaifu za idara hiyo,ambayo jamii huona ni nyepesi na hivyo wengi hushiriki kuwahifadhi na kushika nyadhifa za uwajibikaji katika serikali husika,ili hali idara inakabiliwa na watumishi wachache.

No comments: