Pages

KAPIPI TV

Wednesday, August 13, 2014

WANAFUNZI WATUMIA MIFUKO YA RAMBO KUJISAIDIA-KIGOMA

 
Na Magreth Magosso,Kigoma


WANAFUNZI wa  Shule ya Msingi Airport  iliyopo wilaya ya Kigoma   Manispaa  ya Kigoma Ujiji, wanadaiwa kutumia mifuko ya Rambo kujisaidia haja zao ,baada ya kukosa choo  zaidi ya miaka miwili,  ili  hali  uongozi husika  wanalifumbia  macho changamoto hiyo.


Pia shule hiyo  inakabiliwa na adha ya ukosefu wa maji sambamba na madawati 600 ,ili kukidhi hitaji la wanafunzi wapatao 1408 pamoja na  vyumba vya madarasa ,ambapo kila darasa lina wanafunzi  173, hali inayochangia uelewa finyu kwa wanafunzi husika.


Jamboleo lilipiga hodi katika shule hiyo,baada ya kubaini Diwani wa kata ya Mwanga mjini Moses  Bilantanye Kuahidi kupeleka  Mifuko ya Rambo shuleni hapo,ili kuokoa jahazi la vifo kwa wahanga hao kutokana na choo chao kutitia.


shule ilitaka kufungwa kitambo lakini wamezibaziba  tundu mbili tu tena kwa shida ,wanafunzi hutumia sasa mimi napeleka mifuko  wiki ijayo ,ili wajisaidie humo,” alianisha Bilantanye.


Kwa upande wa Mwalimu Mkuu Yustus Fundi alipohojiwa  mifuko ya Rambo kutumika  kwa wanafunzi hao ili kujisitiri na maumbile  ya mwili alisema ni kweli hali inayochangiwa na ubovu wa matundu saba ya choo  sambamba na ukosefu wa maji.


Alisema aliyekuwa mkurugenzi wa awali Alfred  Luanda na ofisa elimu Shomari Bane walifika katika shule hiyo na kutaka ujenzi ufanyike ndani ya wiki moja kuokoa janga hilo, kabla ya utekelezaji  walihamishwa  mkoani hapo.


Mratibu  elimu kata ya husika  Edes  Ibrahim  na  kaimu mwalimu mkuu Deogratius Rulakuze  kwa nyakati tofauti walisema Novemba,23,2012 walipeleka barua kwa wakuu wa idara na hakuna jipya zaidi ya kila mwanafunzi anajua njia ya kujisitiri kwa namna yake.


Walisema  walijaribu kuomba msada kwa BayPort na  mkuu wa uwanja wa ndege mkoani hapo lakini jitihada za kuwapatia  hitaji hilo hakuna  zaidi ya ahadi ya maneno .


Aidha Mtandao huu umeshuhudia baadhi ya wanafunzi Matilda Zephine na Neema Samweli wakinyata kwa tahadhari kuingia katika choo hicho ambacho wakati wowote kitazama chini kutokana na shimo kubwa lililotoboa  tundu za choo hicho.


Walipoulizwa sababu ya kunyata wakati wa kuingia chooni walidai wanaogopa kutumbukiwa na kukiri hali hiyo inashawishi baadhi kuwa watoro hasa wakishikwa na haja wakienda nyumbani nadra kurudi darasani kuendelea na vipindi vingine.


Akijibia hilo  Mwenyekiti  kamati ya uchumi  afya na elimu  manispaa hiyo Moshi Said  alisema  changamoto ya vyoo katika shule za manispaa kigoma ujiji ni makubwa hivyo  katika kikao cha Octoba mwaka huu 2014  watatenga   bajeti ya  kujenga matundu ya vyoo 200 kwenye shule  zote zenye changamoto hiyo .

No comments: