Pages

KAPIPI TV

Saturday, August 2, 2014

VIONGOZI WAASWA KUENDELEZA UZALENDO


ELE1
Kamishina wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda akikata utepe kuashilia uzinduzi rasmi wa Filamu ya The Minister katika hafla iliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam, anayeshuhudia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo
ELE2
Kamishina wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda akifurahia mara baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Filamu ya The Minister katika hafla iliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaa,. Filamu hiyo imetengenezwa na Kampuni ya Equity Link Enterpreses ya jijini Dar es Salaam ambapo inaelezea namna viongozi wa umma wanavo ishi katika muktadha wa maadili miongoni mwa jamii zao.
ELE3
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzaia Bibi Joyce Fissoo akimpongeza Jaji Mstaafu Salome Kaganda mara baada ya kuzindua rasmi Filamu ya “The Minister” Filamu hiyo ilimetengenezwa na Kampuni ya Equity Link Enterpreses ya jijini Dar es Salaam inaelezea namna viongozi wa umma ambavyo utumia nyadhifa zao bila kuzingatia maadili.Katika ni Muongozaji Mkuu wa Filamu hiyo na Mkurugenzi wa Kampuni iliyotengeneza Filamu hii Bibi. Deborah Nyakirang’ani.
ELE4
Msaani wa Filamu mbaye ameigiza kama Mhe. Waziri katika filamu hiyo Bw. Julius Busee (Mr.Kakula) akifanya mahojihano na waandishi wa Habari wakati wa hafla ya uzinduzi wa Filamu ya “The Minister” ambapo yeye ndiyo muhusika mkuu.
ELE5
Katikati Kamishina wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda akiangalia ngoma mara baada ya kuzindua rasmi Filamu ya The Minister jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo na kulia ni Muongozaji Mkuu wa Filamu hiyo na Mkurugenzi wa Kampuni iliyotengeneza Filamu hii Bibi. Deborah Nyakirang’ani.
ELE6
Wa kwanza kutoka kulia Mkurugenzi wa Msaidizi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Leah Kihumbi akiwa na baadhi ya wadau wa Filamu wakiangalia Filamu The Minsiter ilipoonyeshwa kwa mara ya kwanza wakati wa hafla za uzinduzi wake hivi karibuni katika Ukumbi wa Century Cinemax jijini Dar es Salaam.
ELE7
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzaia Bibi Joyce Fissoo akiwa katika picha ya pamaoja na wasanii walioigiza akatika Filamu ya The Minsiter mara baada ya uzinduzi kukamilika, Filamu hiyo imetengenezwa na Kampuni ya Equity Link Enterpreses ya jijini Dar es Salaam ambapo inaelezea namna viongozi wa umma wanavo ishi katika muktadha wa maadili miongoni mwa jamii zao. Picha zote na Frank Shija Afisa Mawasiliano Serikalini, WHVUM
…………………………………………………………………………………
 
Na Frank Shija, WHVUM
Viongozi wa umma wametakiwa kuendeleza uzalendo ambao muasisi wa Taifa hili Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere alituachia.
 
Rai hiyo himetolewa na Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda alipokuwa akizindua Filamu ya “The Minister” mapema hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
 
Jaji Kaganda alisema kuwa viongozi wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha uzalendo unakua hapa nchini ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma kwa mujibu wa sheria badala ya kuendelea kupiga kelele bila vitendo.
 
Aidha Jaji Kaganda aliongeza kuwa watumishi wa umma wanaongozwa na kanuni za maadi ya utendaji ambapo alitaja sheria ya maadili ya viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995 na kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma za mwaka 2005 ambapo alisema mtumishi akizingatia ni dhahiri kwamba atakuwa mzalendo wa kweli.
 
 Aliongeza kuwa amefarijika kuona wasaniisasa wameamua kutumia vipaji vyao kutoa Elimu ya maadili ambapo kupitia Filamu ya The Minister viongozi wengi watajifunza ana kujisahihisha pale walipoteleza. Alisema Jaji Kaganda
Jaji amesema kuwa maadili ni suala nyetu kwani bila maadili haki haipatikani hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu kwa nafasi yake kuhakikisha kunajenga jamii yenye maadili.
 
Katika hali ya kuonyesha amevutiwa na Filamu hiyo Jaji Kaganga ametangaza rasmi kuwa Ofisi yake itatumia Filamu hiyo kama kielelezo rasmi wakati wa utekelezaji wa shughuli za uelimishaji kwa umma.
 
” Nimefurahishwa sana na maudhui ya Filamu hii naomba nipatiwe nakala angalau tano hili nami niweze kuwa na vielezo vya kutumia pindi tunapotekeleza majukumu yetu ya kuelemisha umma juu ya maadili ya viongozi” Alisema Jaji Kaganda.
 
Kwa upande wake Muongozaji wa Filamu hiyo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Equity Link Enterprises Bibi. Debora Nyakirang’ani amesema kuwa wazo hilo la Filamu  ya The Minister baada ya kubaini kuwa wasanii wengi ujikita zaidi katika kucheza filamu zenye mafundisho tofauti na kusahau eneo nyeti la maadili.
 
Kushuka kwa maadili miongoni mwa jamii imekuwa ni chachu ya vijana wengi kutokuwa wazalendo wa nchini yao tena badala yake watu wamebaki kuwa wabinafsi zaidi.Hivyo nimatarajia yangu kwamba kupitia Filamu hii wwatu watabadilika na kurudu katika mstari ulionyooka. Alisema Bibi. Nyakarang’ani.
 
Filamu ya The Minister ni filamu ya kitanzania iliyoandaliwa na kutengenezwa na Kampuni ya Equity Link Enterprises,katika Filamu hiyo inaelezea namna mhusika mkuu alivyobadilika ghafla mara baada ya kupata wadhifa wa Uwaziri, na jinsi ambavyo alikuwa akiishi katika maisha yake binafsi yakionyesha azingatii maadili yake ya kazi ipasavyo

No comments: