Pages

KAPIPI TV

Thursday, August 14, 2014

KIGOMA WAANZISHA BENKI MAALUM YA MATOFALI,NI AGIZO LA RAIS KIKWETE


Na Magreth Magosso,Kigoma
 
IMEELEZWA kuwa,Mkoa wa kigoma umefanikiwa kutimiza agizo la Rais Jakaya Kikwete juu ya kuanzishwa kwa Benki maalum ya matofali kwa ajili ya ujenzi wa majengo mbalimbali katika sekta ya elimu,Afya na Ulinzi kwa lengo la kuboresha huduma hizo.
 
Tamko hilo limefanikiwa kwa asilimia 65 ya nguvu kazi ya wananchi wa wilaya sita ya Kigoma,Kakonko,Buhigwe,Uvinza,Kasulu na Kibondo kwa kuweza kuwa na matanuri ya matofali yapatayo 70 sawa na matofali  milioni tatu,ambapo ifikapo mwishoni mwa mwka huu watakuwa na matofali milioni 5 .
 
Wakizungumza kwa nyakati Tofauti baadhi ya wakazi wa mkoa huo Tumain Fredrick na Juma Hassan  walisema wanachi wapo tayari kutoa nguvu,akili na mali zao katika shuguli za maendeleo ya taifa lao kwa maslai ya kizazi cha leo na siku za usoni kwa kufuata taratibu husika na kuwaasa  viongozi wasimamie kwa dhati ili kufanikisha malengo mtambukwa.
 
 Kwa upande wa mwanafunzi wa shule ya sekondari Manyovu  Juma Nyamgenda alisema ujenzi wa maabara ukifanikiwa katika shule zote itasaidia ufaulu wa masomo michepuo  ya sayansi ambapo  watajifunza kwa vitendo , pia uwepo wa mabweni  ni usalama kwa kutokubughudhiwa na kazi za majumbani na  mimba kwa  wanafunzi wa kike na  kuisihi serikali na jamii watimize  ili  ndoto zao zitimie.
 
Akizindua matanuri hayo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Lt.mstaafu Issa Machibya alisema mradi huo ni moja ya kupunguza changamoto mbalimbali katika jamii husika,hususani ujenzi wa maabara,mabweni,nyumba za watumishi idara ya ulinzi,wauguzi na walimu.
 
 
Machibya aliongeza kwa kubainisha kuwa,viongozi wakishirikiana na wananchi katika agizo hilo ni moja ya kuokoa wanafunzi na matokeoa mabovu ya mtihani wa taifa sanjari na mimba za utotoni kwa wasichana wanaosoma shule za kutwa ambapo ujenzi wa mabweni ni tija kwao kuondokana na vishawishi vya uraiani.
 
 
Aidha  Mpango wa Benki ya Tofali umefikia awamu ya pili baada ya awamu ya kwanza ulikuwa ni mandalizi ya ufyatuaji wa matofali ambapo juzi ulizinduliwa rasmi na mkuu wa mkoa huo katika kijiji cha Mwayaya wilaya ya buhigwe ambapo kupitia wilaya zake sita wamefanikisha agizo la Jakaya Kikwete kwa maslai ya umma  na kuongeza ufanisi wa huduma kwa jamii husika.

No comments: