Pages

KAPIPI TV

Sunday, August 17, 2014

KIGOGO CCM AKATALIWA NA WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU

Na Allan Ntana,Tabora

WAJUMBE zaidi ya 130 wa halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi
Tabora mjini wamemkataa Katibu wa Chama hicho wilaya ya Tabora mjini
Bakar Luasa kwa madai ya kukigawa na kukichafua.

Hatua hiyo ilifikiwa Agosti 12 mwaka huu baada ya wajumbe hao
kuamua kutoka nje ya ukumbi wa Ali Hassan Mwinyi kwa madai ya kutokuwa
na imani na Katibu huyo wa CCM wilaya.

Chanzo cha taarifa toka kwa wajumbe wa halmashuri kuu ya CCM ndani ya
kikao hicho ambao hawakutaka majina yatajwe walisema kufuatia hali
hiyo kikao kiliahirishwa na kufanyika tena mwezi Agosti 13 mwaka huu.

Wajumbe hao walisema baada ya kuingia ukumbini walitoka
nje na kuongea kwa nyakati tofauti wakidai hawamtaki Katibu wao Bakar
Luasa kwa madai kuwa hawana imani naye na anakigawa chama.

“Huyu Katibu wetu ana kama miezi sita au saba hivi na toka amehamia hapa Tabora
lakini tokea afike amekuwa akikivuruga chama kwa migogoro
isiyoisha…….kwa kujifanya yeye anajua ilani na taratibu za chama kila
kukicha anagombana na Mwenyekiti wake”, waliongeza.

Walisema Mwenyekiti wa CCM Tabora mjini Abrahman Nkonkota aligombea
vipindi viwili na
akashinda kwa kura nyingi hivyo kama Mwenyekiti wetu ana tatizo wapo zaidi
ya Makatibu wanne ambao wamepita hatukuona wanakwaruzana naye.

Walisema Katibu huyo wana taarifa anapokea fedha kila mwisho wa mwezi
ili aendeleze fujo na kugawa chama kwa maslahi yake na kamwe
hawataweza fanya kazi na Katibu Bakar Luasa kutokana na kuendeleza
majungu na fitina.

Walisema alipeleka taarifa Makao Makuu ya chama kuwa hakuna
watendaji, sasa wanachama na wajumbe ambao hawamtaki tunatamka wazi
kuwa tunatoka nje ya ukumbi, hatumtaki.
 
Mwandishi wet alimtafuta Katibu wa CCM Bakar Luasa kuhusiana na madai
hayo ambapo alisema yeye hana tatizo, mwenye tatizo ni Mwenyekiti wake
kwani ndiye anaratibu hayo.

“Mimi nafikiri kila kitu kiko wazi kama mimi ni tatizo kwani katibu
mkuu wa CCM Abdurahaman Kinana alikuja akaelezwa na makamu
mwenyekiti wa CCM Philip Mangula naye alielezwa tunasubiri maamuzi ya
kamati kuu ya CCM” alisema.

Alisema kwa kuwa kamati kuu inataka kuchukua maamuzi dhidi yangu na
Mwenyekiti, sina cha kueleza zaidi tusubiri.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tabora mjini Abdulrahaman Moshi Nkonkota
alijibu kuwa tuhuma hizo si za kweli yeye hana matatizo kwani kila kitu kiko
wazi,..... mimi siwezi kushawishi wajumbe zaidi ya 140 wamkatae Katibu wangu
ili iweje, aliongeza.

Alisema, ukweli ni kwamba anagawa chama,  hapa ofisini haelewani na
watendaji, wanachama na mimi mwenyewe kwani hataki kufanya kazi na mimi.

No comments: