Pages

KAPIPI TV

Saturday, August 23, 2014

ACT WADAI KUMLINDA ZITTO KABWE -KIGOMA

Baadhi ya wanachama wapya wakivamia jukwaa la ACT  katika kiwanja cha cine atlasi  manispaa ya kigoma ujiji wakitaka wapewe kadi za chama hicho .
kaimu mwenyekiti akihutubu madhira yaliyochangia kukihama chama cha chadema katika kiwanja cha cine atlas manispaa ya kigoma ujiji.

walioshika bendera za chama katikati aliyevaa flana ya bluu na njano ni katibu ACT wilaya ya kigoma Anzoluni Kibela akiwa ameshika bendera za chadema kutoka kwa wanachama wapya pembeni yake ambao wamekihama Chadema jana katika kiwanja cha cine atlas manispaa ya  kigoma ujiji na hapo chini ni baadhi ya kadi za chadema.

Na Magreth Magosso,Kigoma

Chama  cha  Alliance Transiparency For Change(Act) Mkoa wa Kigoma, kimeahidi kumlinda  Mbunge  wa  Jimbo la Kigoma Kaskazini  Zitto Kabwe kwa gharama zote kutokana na hila zinazofanywa na mahasimu wachache wa chama cha chadema za kutaka kumwangusha kisiasa.
 
Pia wamemshauri afute kesi yake dhidi ya uongozi wa Chadema na kumtaka arudi Kigoma aungane na ACT kwa ajili ya kukusanya  wanachama katika vijiji   vilivyopo hapa kwa lengo la kukuza demokrasia  ya uwazi,uwajibikaji  wenye tija kwa wananchi .
 
Akitoa kauli hiyo kigoma ujiji jana  Mjumbe  Kamati  Kuu  Taifa  Jaffar Kasisiko   katika mkutano wa hadhara uliofanyika  kiwanja cha Cine Atlas uliokuwa ukiwakabidhi  kadi wanachama  wapya  kutoka  vyama mbalimbali  ambapo   wanachama hao  walichana kadi ,bendera na katiba ya chadema wakidai  wameshindwa kukihudumia chadema mkoani hapa.
 
Alisema uongozi wa chadema una hila ya kusambaza maneno hasi dhidi ya Zitto Kabwe  kwa umma kwa lengo la kulinda maslai yao binafsi ,badala ya kutetea haki za wanyonge ili kuboresha changamoto zilizopo kwa tija ya kuondoa fujo na vurugu zinazolinyemelea  taifa husika.
 
“Zitto ni wa hapa,tutamlinda kwa njia zote na huyu Sabrina Sungura achunge ndimi yake,ni mwanetu lakini aache fitna asome alama za nyakati ,akumbuke aliyemuweka katika kiti alichokalia” alibainisha  Kasisiko.
 
Mjumbe halmashauri kuu Taifa Msafiri Wamalwa alisema ,Mbunge huyo asipoteze muda wa kulumbana na uongozi wa chadema,badala yake akaifute kesi katika mahakama husika na aje hapa ili kukijenga chama  hicho.
 
Katibu mwenezi wilaya ya kigoma Anzoluni Kibela alisema hadi sasa kadi  ya kiongozi huyo ipo tayari na kuna wabunge wapatao 18 wapo tayari kujiunga na chama kwenye uzinduzi ,ambao utafanyika mkoani hapo mwanzoni mwa mwezi ujao.
 
Kwa upande wa Kaimu mwenyekiti Taifa Shaban Mambo aliwasihi wananchi wamuunge mkono mbunge huyo atakapojiunga na chama hicho, ili aboreshe adha ya usafiri wa njia ya reli ya kati kwa kuwaletea treni inayotumia umeme kwa gharama zake.
 
Baadhi ya wanachama wapya wa ACT aliyekuwa mweka hazina  Chadema kigoma ujiji, Hamidu Hamis na Katibu wilaya Haji  Idd  kwa nyakati tofauti walisema wamejiunga na ACT kwa nia ya kuleta mabadiliko  ya umoja,uwazi na uwajibikaji kwa mujibu wa dira ya chama hicho.
 

No comments: