Pages

KAPIPI TV

Monday, July 21, 2014

MWIGAMBA ATAKA ACT WATUMIE FURSA CHAGUZI SERIKALI ZA MITAA-KIGOMA

Na Magreth Magosso, Kigoma.

KATIBU mkuu wa chama cha Alliance for change and Transparency(ACT)  taifa  Samson Mwigamba amewataka viongozi wa chama hicho  kuanzia ngazi ya kata na majimbo kuhakiki viongozi  watakaogombea katika uchaguzi ujao 2014 wa serikali za mitaa kwa kuwasimika viongozi wenye upeo wa  mambo na wanaokubalika katika jamii.

Akitoa kauli hiyo  kigoma Ujiji jana katika kikao cha viongozi na wanachama wa chama hicho kutoka jimbo la Kigoma Kaskazini, Kusini na kigoma mjini alisema watumie fursa ya hiyo kuwapa nafasi viongozi wenye sifa na vigezo  kwa lengo la kuboresha mfumo wa utawala.

Alisema ili chama kiweze kupata nyadhifa mbalimbali za uongozi ni lazima kila kiongozi katika jimbo alilopo ahakikishe kunakuwa na uongozi kamili katika vijiji ,ili kunyakua majimbo katika nafasi za udiwani, ubunge na urais.

Hata hivyo aliwataka viongozi na wanachama kuacha siasa za matusi katika majukwaa na badala yake watumie lugha za hekima,busara na kizalendo kwa hoja zenye mashiko ya kuelimisha umma na kufanya kazi kwa uwazi na uwajibikaji.

Mwigamba alisema lengo la chama hicho kurekebisha siasa ya nchi kupitia vyama pinzani kwa kuondoa tofauti zilizopo pamoja na kuondoa utashi wa mwasisi wa chama katika vyama vilivyopo, kuwa na demokrasia ya kweli ambapo vyama vingine havizingatii hilo.

Naye katibu wa mawasiliano na habari Muhamedi Masaga alisema kuanzishwa kwa chama sio kwa lengo la kudhohofisha vyama vingine ni kuwa na chama chenye mshikamano, umoja na kulinda uzalendo wa   n chi ili kushika dola ya nchi katika chaguzi zijazo.

Alisema katika ziara walizozifanya katika mikoa mitatu, mkoa wa kigoma umekuwa kinara  wa wanachama waanzilishi ambao wamefikia 570 ikifuatiwa na Katavi 400 pamoja na Tabora 150 ambapo ni mwanzo unaoleta matumaini katika kukiendeleza chama.

No comments: