Pages

KAPIPI TV

Monday, June 23, 2014

ZAIDI YA ROBO TATU YA WANAKIJIJI WARUDISHA KADI ZA CHADEMA,WAJIUNGA NA CCM-NZEGA

Katibu wa Itikadi,Siasa na Uenezi CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Kapama akiangalia kadi zilizorejeshwa na  waliokuwa wanachama wa Chadema katika Kijiji cha Ugembe 2 kata ya Mwakashahala wilayani Nzega ambapo zaidi ya robo tatu ya wakazi wa Kijiji hicho walirudisha kadi wakidai kuchoshwa na Porojo za baadhi ya viongozi wa Chadema ambao wamekuwa wakifika mara chache na kutoa ahadi hewa za matumaini. 
Wakati wanakijiji wa Ugembe wakichangamkia kurejesha Kadi za Chadema baada ya kukosa matumaini
Katibu wa CCM wilaya ya Nzega Bw.Kajoro akisoma majina ya wanachama wapya wa CCM huku Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Ali Ame akigawa kadi kwa wanachama hao waliohama kutoka Chadema katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Ugembe
Wanachama wapya wa CCM wakifanya kiapo cha kujiunga na chama hicho.
Katibu wa CCM Bw.Kajoro akisoma kanuni za mwanachama wa CCM ikiwa ni ishara ya kiapo cha uanachama baada ya kujiunga na chama hicho.
Mwanachama mpya wa CCM akiisoma vizuri kadi yake baada ya kupatiwa na Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Ali Ame. 
Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Ame akizungumza na wananchi katika Kjiji cha Ugembe wilayani Nzega ambapo pamoja na mambo mengine Bw.Ame alisisitiza msimamo wa Chama cha Mapinduzi kuhusu Katiba mpya juu ya umuhimu wa Serikali mbili  zilizoboreshwa kama msingi imara utakaosaidia kuondoa kero wa wananchi.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Bw.Amos Kanuda akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Ugembe 2 ambapo aliwataka kuendelea kukiamini CCM kwa madai kuwa ndio chama pekee chenye muelekeo wa kuleta maendeleo.







No comments: