Pages

KAPIPI TV

Sunday, May 25, 2014

MGONJWA WA HOMA YA DENGUE APATIKANA KIGOMA



Na Magreth Magosso,Kigoma
WANANCHI wa Mkoa wa Kigoma wametakiwa wafanye usafi wa mazingira maradufu katika kaya  zao ili waepukane na ugonjwa wa Dengue,ambapo kwa sasa  mkazi mmoja amekutwa  na ugonjwa huo.

Akifafanua kauli hiyo Mganga wa Mkoa Leonard Subi kwenye kikao cha kamati ya ushauri  ya  Mkoa  alisema, kwa sasa  kuna mgonjwa mmoja wilaya ya Buhigwe  na anapatiwa matibabu katika hospitali ya misheni ya Heru,baada ya kuambuki zwa  kirusi cha  mmbu aina ya Edesi ambaye anaambukiza ugonjwa huo.

Alisema  awali mkazi huyo alitoka jijini Dar-es-salaam na kuja hapa kwa lengo la kusalimia jamaa zake ndipo  akapatwa na homa ya ghafla na baada ya kuchukuliwa vipimo vyote akagundulika na ugonjwa wa dengue.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Issa Machibya aliwaonya wananchi  waache kupokea taarifa zisizo na utafiti wa uhakiki toka wizara husika juu ya tiba zinazotolewa katika mitandao ya kijamii kwa kubainisha tiba  feki ya ugonjwa huo.

Alisema jamii ikubali maelekezo ya wataalamu wa afya juu ya dalili husika hasa ya kutoka damu sehemu za wazi,kuchoka kwa viungo vya mwili,na waende kwenye vituo vya afya kwa uchunguzi zaidi kabla mgonjwa ajazidiwa.

N aye Katibu tawala wa mkoani hapa,Eng.John Ndunguru alisema bora kinga kuliko tiba,usafi unaondoa magonjwa kwa asilimia 55,hivyo jamii haina budi kuzingatia utunzaji  na usafi wa mazingira kwa manufaa yao na mkoa kwa ujumla lengo kuepukana na magonjwa ya mlipuko ukiwemo dengue.

No comments: