Pages

KAPIPI TV

Monday, April 14, 2014

ZANA ZA WAVUVI ZILIZOIBWA NA KUPELEKWA CONGO ZAREJESHWA KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

IMEFAHAMIKA kuwa,baadhi ya mitumbwi inayoibwa katika Ziwa Tanganyika mkoani hapa imekuwa ikitumika kwenye kazi za doria katika mto Lukoga mashariki ya nchi ya Congo-DRC.

Kauli hiyo imekuja baada ya baadhi ya mashine 2,mitumbwi 2 sanjari na karabai kumi za wavuvi  kurudishwa kwa wahanga wa uvuvi kigoma ,kufuatia kamati ya wajumbe maalum kufuatilia mchakato wa kuzipata zana 18 ambazo ziliibwa machi,3,2014 sambamba na kutekwa kwa mvuvi moja katika ziwa hilo.

Ally Mziya ni mmoja wa waliozipata zana hizo alisema  wahalifu wanaoiba zana za uvuvi wanamahusiano ya karibu na baadhi ya askari jeshi wa wilaya ya Kalemi ,hali inayochangia kusuasua kwa zana 16 kurudishwa kigoma,kutokana na sheria ya nchi hiyo ,huku akiomba serikali  zote mbili zishirikiane kwa dhati ili kuondoa changamoto hiyo.
 
Akijibu hilo Ubalozi mdogo wa DRC-Congo Ricky Molema alisema kamati yao ya ulinzi wilaya ya kalemi imebaini kundi hilo la uhalifu  wa ziwani na wapo katika mchakato wa kuwabana waachane na kasumba hiyo, ili kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo,huku akidai si kweli wanatumia zana za wizi za kigoma katika kufanikisha doria zao.
 
Akikabidhi zana hizo kwa baadhi ya wavuvi Mkuu wa wilayani kigoma Ramadhan Maneno alidai jumatatu atakuwa na mkutano na wadau wa uvuvi ili kutambua raia wanaoishi kinyume na sheria ili warudishwe kwao kwa lengo la kupunguza mtandao wa kihalifu unaoathiri uchumi wa wilaya ya kigoma na Uvinza.

Naye mgeni rasmi katika makabidhiano hayo,Mkuu wa MKoa huu Lt.Mstaafu  Issa Machibya alisema wavuvi wawe sehemu ya polisi jamii ili kubaini viashiria vya uhalifu dhidi yao,hali itakayokomesha unafiki miongoni mwao na kuwataka wakuu wa wilaya ya Uvinza na Kigoma wabaini wahamiaji haramu ili kuwadhibiti na waishi kwa taratibu na sheria za idara ya uhamiaji kwa lengo la kukomesha uhalifu mkoani hapo.

Ofisa upelelezi wa Mkoa  Dismas Kisusi na Mwenyekiti wa wavuvi  Ramadhan Kanyongo kwa nyakati tofauti walisema vitendo vya uhalifu ziwani vilianza kushamiri katika ukanda wa mwambao wa ziwa Tanganyika kuanzia mwaka 2011 hadi 2014 hali inayochangiwa na hali halisi ya mipaka ya mkoa huo ,

Sanjari na  bajeti finyu ya ulinzi katika ziwa hilo,lakini leo(jana) Lt.Machibya amedai dolia zipo za kudumu kwa siku 365 na kusisitiza wahalifu watakiona na kukiri zana zilizorudishwa ni chache kulingana na zilizochukuliwa.

No comments: