Pages

KAPIPI TV

Monday, April 14, 2014

SAMSUNG YAZINDUA SIMU MPYA GALAXY S5 IKILENGA MAMBO MUHIMU YA WATEJA WAKE


heart rate
Meneja wa Simu za mkononi wa Samsung Tanzania , Bw. Silvester Manyara, akiwaonyesha waandishi wa habari jinsi simu mpya inavyopima mapigo yake ya moyo. Pembeni yake ni Bw. Kishor Kumar, Meneja wa kitengo cha simu na mambo ya teknohama wa Samsung Tanzania.
samsung team
Team ya Samsung Tanznia Bw. Silvester Manyara, Bw. Jang na Bw. Kishor Kumar kwenye picha ya pamoja wakionyesha Simu mpya ya Galaxy S% iliyozinduliwa rasmi hapa Dar es Salaam.
waandishi wa hbr pamoja na wananchi
Waandishi wa habari pamoja na wateja wakishuhudia uzinduzi wa simu mpya ya Samsung Galaxy S5.

“Teknolojia ya kisasa duniani, camera iliyobora zaidi sokoni, na unmatched support for fitness na kusaidia kufanya maisha ya kila siku ya wateja wa Samsung kuwa na maana zaidi”

Kampuni inayoongoza kwa kutengeneza vifaa vya umeme ya Samsung imeungana na nchi nyingine duniani kuzindua simu ya mkononi mpya ya Galaxy inayojulikana kama Galaxy S5 ; simu ya kisasa na bora zaidi ya mkononi ilitengenezwa kwa matakwa ya mtumiaji

Simu mpya ya Galaxy S5,nyepesi, inayofanya kazi kwa haraka na imezinduliwa rasmi siku ya leo tarehe 11/4/2014 kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Dar es salaam. Simu mpya ya Galaxy S5 inamrahisishia vitu vingi mtumiaji na kumpa ujuzi kupitia features maalum anavyoweza kutumia katika shughuli zake za kila siku

Akiongea na waandishi wa habari Meneja wa kitengo cha simu na teknohama wa vifaa kampuni ya Samsung Tanzania Bwn.Kishor Kumar alikua na haya ya kusema “Kupitia Galaxy S5,Samsung imevuka matarajio yetu kwa kutuletea bidhaa inayolenga zaidi matakwa ya wateja wake.” Bw. Kishor Kumar aliendelea kwa kusema “ Wateja wanataka bidhaa na simu ambazo zitawarahisishia kwa njia moja au nyingine maisha yao ya kila siku. Simu ya Galaxy S5 imetengenezwa na ubunifu wa kipekee wa hali ya juu ikiwa na vigezo vyote zinazotegemewa na watu”

Bw.Kishor alienda mbali zaidi kwa kuongeza kua simu ya  Galaxy S5 imeboreshwa maradufu; rahisi kwenye utumiaji na imuongezwa  ubora wa kamerayake pamoja na vipimo vya kulinda usalama wa simu (security feature).

Galaxy S5 ina umbile jembamba la kuvutia, kioo kikubwa cha simu, fremu ya metalic, chaguo kubwa la rangi za kisasa, finishing choices ambazo zinaonyesha muundo mpya wa simu duniani. Simu hii inajumuisha kamera ya kisasa,muunganiko wa kasi wa mtandao, vifaa vya kuangalia ubora wa hali yako and vifaa vilivyoboreshwa vya ulinzi (protection and security feature) ambavyo vinakufanya uwe na mawasiliano in style.

No comments: