Pages

KAPIPI TV

Saturday, April 12, 2014

KATIBU MKUU WA CCM,AENDELEA NA ZIARA YAKE MKOANI KIGOMA.

Katibu Mkuu wa CCM;Ndugu Kinana na Wananchi wakishiriki ujenzi wa Ghala la kuhifadhi mazao na mashine ya kusaga nafaka katika kijiji cha cha Kidahwe,Kigoma Vijijini.Ghala hilo  linalenga kusaidia katika kuhifadhi mazao ya wakulima na kijiji hicho baada ya kuvuna ili kusubiri soko na bei nzuri ya mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.Usimikaji wa mashine katika ghala hilo utawasaidia  pia wakulima kuchakata mazao yao (hasa mahindi na muhugo) na kuuza unga badala ya mahindi.Gharama za mradi huo ni shiliingi milioni 104,800,000/=.
Katibu wa NEC-CCM wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akishiriki ujenzi wa Ghala la kuhifadhi mazao na mashine ya kusaga nafaka katika kijiji cha cha Kidahwe,Kigoma Vijijini.Ghala hilo  linalenga kusaidia katika kuhifadhi mazao ya wakulima na kijiji hicho baada ya kuvuna ili kusubiri soko na bei nzuri ya mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.Usimikaji wa mashine katika ghala hilo utawasaidia  pia wakulima kuchakata mazao yao (hasa mahindi na muhugo) na kuuza unga badala ya mahindi.Gharama za mradi huo ni shiliingi milioni 104,800,000/=.
Katibu wa NEC-CCM wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye (kulia) akifafanua jambo kwa Wananchi (hawapo pichani) walipokwenda kukagua kushiriki na kukagua ujenzi wa Ghala la kuhifadhi mazao na mashine ya kusaga nafaka katika kijiji cha cha Kidahwe,Kigoma Vijijini.
Baadhi ya Wazee wa kijiji cha Nkungwe wakifuatilia yaliyokuwa yanazungumwa na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana katika kijiji cha Nkungwe,kuhusiana na tatizo la ufumbuzi wa mradi wa maji.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Nkungwe kuhusiana na mradi wa maji unaojengwa,ambao kwa sasa umesimama kutokana na ukosefu wa fedha.
Ujenzi wa tanki hilo la maji kama lionekanavyo pichani.
Katibu Mkuu Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi kuhusiana na ujenzi wa tanki la maji katika kijiji cha Nkungwe,Kigoma vijijini.
Ndugu Kinana (wa tatu kulia),akishiriki kufukia mabomba ya mradi wa maji katika kijiji cha Nkungwe,Kigima vijijini.Mradi huo ukikamilika unatarajiwa kusaidia vijiji zaidi ya 30.
Ndugu Kinana akiwasalimia wananchi mbalimbali (hawapo Pichani),wakati alipokuwa akiwasili katika kijiji cha Nkungwe kukagua mradi wa maji ambao umeshindwa kukamilika kutokana na ukosefu wa fedha. Kinana amewaahidi wananachi kulitafutia ufumbuzi suala hilo ili mradi huo ukamilike na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Mjumbe wa NEC,Balozi Ally Karume akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mara baada ya kukagua mradi mkubwa wa maji katika kijiji cha Nkungwe,Kigoma vijijini.Mradi huo umeshindwa kukamilika kutokana na ukosefu wa fedha,lakini pia Kinana amewahidi wananchi kulitafutia ufumbuzi wa haraka tatizo hilo na hatimaye mradi huo kukamilika na kuwasiadia wananchi mbalimbali wa maeneo hayo.
Katibu wa NEC-CCM wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye (katikati) akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Mahembe, Jimbo la Kigoma Kaskazini.
Baadhi ya Wanakijiji cha Mahembe wakiwa kwenye mkutano huo wa hadhara
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisoma orodha ya vijiji vitakavyopatiwa umeme na maji katika wilaya ya Kigoma Vijijini. Kikiwemo Kijiji cha Mahembe ambacho tayari kimepata umeme.
Mkutano wa hadhara ukiendelea kwenye kijiji cha Mahembe,Kigoma vijiji ambapo wananchi wengi walijitokeza kusikiliza yaliyokuwa yakisemwa kwenye mkutano huo.
Vijana wa bodaboda wakiwa kwenye msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana katika kijiji cha Mwandiga,Kigoma Vijijini 
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipokelewa na wanachama mbalimbali wa CCM,alipokuwa akiwasili kwenye ofisi ya makao makuu ya wilaya ya Kigoma Vijijini,katika kata kijiji cha Mwandiga,Kigoma Vijijini .
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizunguma na baadhi ya Mabalozi mbalimbali wa CCM (hawapo pichani),kwenye kikao chao cha ndani,kilichofanyika katika ofisi ya makao makuu ya wilaya ya Kigoma Vijijini,katika kata kijiji cha Mwandiga,Kigoma Vijijini .

Baadhi ya Mabalozi mbalimbali wa CCM,wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Nduguu Kinana alipozungumza nao kwenye kikao chao cha ndani,kilichofanyika katika ofisi ya makao makuu ya wilaya ya Kigoma Vijijini,katika kata kijiji cha Mwandiga,Kigoma Vijijini .
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwa emeongozana na Viongozi wengine wa CCM,Mkoa na Wilaya katika kukagua mradi wa  wajasiliamali wa Kilimo,ndani ya kijiji cha Kidahwe Kigoma Vijijini mkoani Kigoma.

No comments: