Pages

KAPIPI TV

Tuesday, April 15, 2014

JOTI MSANII AMBAYE ANAZIDI KUPATA UMAARUFU NCHINI NA NJE YA NCHI BILA KUWA NA MAJIGAMBO

Msanii wa vichekesho nchini maarufu JOTI anazidi kuendelea kujipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi huku idadi ya watu wanaomkubali ikizidi pia kuongezeka....JOTI ambaye anaonesha kujali watu wanaomkubali katika tasnia hiyo ya uchekeshaji na amekuwa hana unyanyapaa kwa watu wote jambo ambalo linazidi kumpa nafasi kwa mashabiki wake na kuonekana kuwa ni msanii ambaye kwa hali ya kawaida bado ataendelea kuwa nyota mbele ya watu...Nimemsikia na kumuona mara kadhaa msanii huyu nguli ambaye karibu kila kona amekuwa mtu wa watu na pia hasikiki kuwa na mtazamo wa kujitengenezea  umaarufu  kupitia mfumo wa kuandaa  kashfa za ajabu ajabu kwenye magazeti  kama walivyo wasanii wengine nchini ambao hujipandisha chati kwa mfumo huo...JOTI nimekutananae tena hapa Dodoma akiwa anazungumza na baadhi ya watu ambao walikuwa na hamu kubwa ya kumsikiliza.

No comments: