Pages

KAPIPI TV

Wednesday, March 26, 2014

TUME YA MACHIBYA YARUDI KICHWA CHINI-KIGOMA

Na Magreth Magosso, Kigoma.

TUME  iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa Kigoma Luten kanali Mstaafu Issa Machibya kufuatilia zana za uvuvi zilizoibiwa na kupelekwa nchi ya kidemocrasia ya Congo haijafanikiwa kurudi na zana hizo kutokana na kuwepo kwa utata baina ya viongozi wa serikali hiyo.
 
Akizungumzia hilo mwakilishi wa wavivu Salumu Shabani ambaye alikuwa katika tume hiyo alisema kuwa jitihada za mkuu wa mkoa wa kigoma  ni kubwa lakini kutokana na mfumo uliopo katika nchi ya Congo imekuwa ngumu kuweze kutimiza yale ambayo analenga kuwasaidia wavuvi mkoani hapa.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana kigoma ujiji, Shabani alisema licha ya kuwepo kwa mikataba ya ujirani mwema baina ya nchi hizo kwa lengo la kuwepo na mahusiano baina yao na viongozi kuhakikisha zana zinazoibiwa na kupatikana katika nchi hizo zirudishwe bila masharti magumu wala urasimu wowote bado mkataba wa ujirani mwema unakiukwa na n chi hiyo.
 
Alisema kuwa, wizi unaofanywa na watu wa nchi hiyo umekuwa ukurudisha nyuma maendeleo ya wavuvi kwa kuwatia umaskini ambapo asilimia 80 ya wakazi wa mkoa huo  wanategemea shughuli za uvuvi ili kulea familia zao na kumudu hali ya maisha.
 
Aidha  mara kadhaa uongozi wa mkoa wa kigoma umekuwa ukituma wawakilishi kufuatilia zana hizo bila mafanikio ambapo fedha za serikali zimekuwa zikitumika kuhakikisha wavuvi wanapatiwa zana zao na wanafanya shughuli za uvuvi kwa amani na utulivu katika ziwa Tanganyika.
 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wa wavuvi Ramadhani Kanyongo na Makamu wake Sendwe Ibrahimu walisema kuwa hadi ifikapo 2025 uvuvi wa mkoa wa Kigoma utakuwa ni ule wa kusonza kwa mitubwi na sio uvuvi uliopo kipindi hiki sambamba na mapato ya mkoa na Halmashauri kuporomoka kwa kasi na uchumi kushuka.
 
Walisema kuwa kutokana na kukidhiri kwa wizi katika mwambao wa ziwa Tanganyika bei ya mazao ya samaki na dagaa imepanda kutokana na wavuvi na wamiliki kuhofia kuingiza vyombo vyao ziwani na wavuvi kuhofia usalama wa maisha yao.
 
Walisema kuwa awali mwaka 2003 kulikuwa na mitubwi 168 katika mwalo wa kibirizi ambapo kwa sasa imebaki 45, huku mwalo wa katonga kulikuwa na mitumbwi 200 na sasa ipo 168 hali inayokatisha tama kuendelea kufanya shughuli za uvuvi katika ziwa hilo.
 
Hivi karibuni Mkuu wa mkoa akizungumza na wavuvi alisema kwa kushirikiana na wananchi, wavuvi na vyombo vya ulinzi na usalama tatizo hilo litapatiwa ufumbuzi ikiwa ni pamoja na kuendesha msako wa kuwakamata wahamiaji wanaoishi kinyume cha sheria na kuwarudisha katika nchi zao.
                                                               
Akijibia hilo ubalozi mdogo wa Nchi ya Congo  Kigoma Balozi Riky Molema   akiri mfumo wa uendeshaji wa serikali ya Tanzania na serikali ya Congo uko tofauti na hivyo kuwa vigumu kupata zana hizo kwa wakati muafaka na kuwataka wavuvi kuwa wavumilivu .
 
Alisema kuwa ili kuondoa tatizo la wizi katika mwambao wa ziwa ni lazima dhati ya kuthubutu kwa viongozi husika wa serikali zote mbili kuunda ulinzi shirikisha ndani ya ziwa hilo kwa kufanya doria ya pamoja na kuhakikisha wimbi la wizi katika ziwa hilo unatokomea.

No comments: