Pages

KAPIPI TV

Tuesday, September 17, 2013

NGELEJA ACHANGISHA SHILINGI MIL.18 KANISA LA MORAVIAN SIKONGE

Na  Mwandishi wetu,Sikonge

WATANZANIA wameaswa kuishi maisha ya kupendana,kusaidiana na kuvumiliana na bila kufanya hivyo Tanzania haitakuwa kisiwa cha amani.

Mbunge wa jimbo la Sengerema mkoani Mwanza Williamu Ngeleja alisema hayo wakati wa ibada katika kanisa Moravian jimbo la Magharibi wakati akifanya harambee ya kuchangia kwaya ya Upendo ya Sikonge.

Mbunge huyo alichangisha kupitia harambee hiyo kiasi cha milioni 18 ambapo yeye binafsi alitoa sh milioni 6,335,000,mbunge wa Sikonge Said Nkumba alitoa sh milioni 2,mbunge wa jimbo la Igunga 500,000,mbunge viti maalumu Munde Tambwe sh 500,000 na mwenyekiti wa halmashauri Uyui sh 500,000 na waumini wengine zikiwemo taasisi za serikali.

Ngeleja alisema hivi sasa Tanzania tumefikia mahali kumekuwa na chokochoko kadhaa ikiwemo watu wachache kutaka kutugawa kwa misingi ya dini,ukabila na ukanda na kutaka watu hao wapuuzwe.

Alisema dalili mbaya za nchi yetu kuingia kwenye mifarakano ziko wazi tunapaswa kukemea hali hiyo kwa nguvu kubwa kwani imefikia mahali sasa watu wanakamatwa na madawa ya kulevya na wengine wanamwagiwa tindikali.

“Sisi kama wanakondoo wa bwana tunapaswa kukemea kwa nguvu zote na wachache hawa wafikie mahali watambue sisi kama watanzania tuko imara hatuatkubali kuharibiwa amani yetu kwa tamaa za wachache.” alisema.

Amesema anaumia sana kusikia Tanzania ya leo imekuwa ni sehemu ya biashara na kuingiza dawa za kulevya na kumwagiana tindikali kwa viongozi wa dini.

Mbunge huyo alisema haya yote ymekuja kutokana na kutoishi kwa hofu ya bwana na kutokubali kuishi na mwenyezi Mungu lakini tunapaswa kuombena.
Alisema anapenda kushirikiana katika shughuli za kijamii ili kuleta maendeleo tarajiwa na kwamba mali,utajiri na akiba vyote vinatoka kwa Mungu sote tutambue hilo.

“Ni jambo la kufurahisha na kushirikiana na bwana kwa kuliimbia jinalake na ndiyo maana leo tuko hapa tunazindua albamu ya “Kanisa la Mungu na kufikka kwake Sikonge kanisani ni mpango wa Mungu” alisema.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Sikonge Said Nkumba awali aliwapongeza viongozi wa kanisa Moravian kwani mafanikio yao ni kutokana na malezi na uongozi bora.

Alisema Yesu anaondoa pazia la ubaguzi,dini na dini ukabila, ukabila undugu na undugu tuachea hayo ni dhambi kwa mwenyezi Mungu.
Msomaji wa risala ya kwaya ya upendo Aneth Masanja alisema kikundi kinahitaji kurekodi na vifaa vingine vinavyogharimu kiasi cha sh milioni 23.

No comments: