Pages

KAPIPI TV

Thursday, September 20, 2012

LICHA YA KASORO NDOGO MTIHANI WA DARASA LA SABA SINGIDA WAANZA VEMA

Wanafunzi Singida
 Na.Nathaniel Limu-Singida.

Mtihani  wa kumaliza elimu ya msingi unaohusisha wanafunzi 27,749 wa darasa la  saba mkoani Singida umeanza kwa amani na utulivu licha ya  kujitokeza kwa kasoro ndogondogo.
Miongoni mwa kasoro hizo ni pamoja na  utoro, baadhi ya wanafunzi kutojua  kusoma na kuandika na walimu na wasimamizi kulalamikia mfumo wa maswali ya kuchagua na kuweka vivuli.
Katika  shule ya msingi  Mtisi  iliyopo umbali wa zaidi ya kilomita 24 kusini magharibi mwa mji wa Singida, wasimamizi  wa mtihani huo wamesema kati ya 34 watahiniwa nane (8) hawakufanya mtihani kutokana na utoro na wengine sita wameshindwa kusoma wala kuandika.
Hata  hivyo afisa elimu mkoa wa Singida  Yusuf  Kipengele, amesema mbali ya kasoro hizo  hakuna dosari nyingine kubwa iliyojitokeza na kuathiri ufanyaji huo wa mtihani ulioanza leo.
Kipengele ametoa wito kwa wasimamizi  wa mtihani  huo kuwa waadilifu na kutojihusisha na udanganyifu vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria pindi watakapobainika.

No comments: