Pages

KAPIPI TV

Tuesday, May 8, 2012

WANAKIJIJI WAFUNGA OFISI YA KIJIJI"Washinikiza kusomewa taarifa ya mapato na matumizi"



Na:Robert Kakwesi,Urambo
Wanakijiji wafunga ofisi ya kijiji
WANANCHI wa Kijiji cha kangeme,kata ya Zugimlole,wilayani Urambo wameifunga ofisi ya kijiji wakishinikiza kusomewa Taarifa ya Mapato na matumizi.
Wakizungumzia hatua hiyo wananchi hao walieleza umauzi wao unatokana na uongozi wa kijiji hicho kutowsomea taarifa ya mapato na matumizi kwa muda wa mwaka na mmoja na nusu.
Walisisitiza wataendelea kushikilia msimamo wao kwa vile uongozi wa kijiji umekuwa ukiwapiga chenga wanapowasilisha ombi la kusomewa taarifa ya mapato na matumizi.
Diwani wa kata ya zugimlole.Mh Moshi Kitoboli,alieleza uamuzi huo wa wananchi unatokana na kutokuwa na imani na mwenyekiti wa Kijiji hicho akisema haujasoma taarifa ya mato na matumizi kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
Alieleza uamuzi huo huenda unatokana na kamati ya maendeleo ya kata kupanga ratiba na kuwajulisha wananchi kwa kufuata kalenda ya halmashauri ambapo mkutano wa kusomewa taarifa ya mapato na matumizi ulikuwa ufanyike tarehe 20 mwezi uliopita.
Ili kuweka mambo sawa,Diwani Kitoboli,alisema amemuagiza Mtendaji wa Kata,George maganga,kufuatilia suala hilo na tayari yupo kijijini hapo kupata ufumbuzi wa suala hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Urambo.Bi Anna Magowa,alieleza wiki kadhaa zilizopita kuhimiza viongozi wa vijiji wilayani Urambo kusoma taarifa za mapato na matumizi kwa kufuata kalenda za vikao.
Alisisitiza hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa wote watakaokiuka agizo hilo jambo ambalo pia lilikubaliwa na baraza la madiwani lilioafiki kuchukuliwa kwa hatua kwa watakaoshindwa kusoma taarifa za mapato na matumizi.


No comments: