Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na washiriki wa
semina hiyo leo wakati akifungua mafunzo hayo rasmi yaliyoandaliwa na
Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kuratibiwa na
Klabu ya Waandishi wa Habari ya Rukwa (Rukwa Press Club). Mafunzo hayo
yatadumu kwa muda wa siku nne na jumla ya washiriki 18 kutoka vyombo vya
habari tofauti vya Mikoa ya Rukwa na Katavi wanashiriki. Katika maneno
yake ya ufunguzi Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka waandishi wa habari wa
Rukwa kuhakikisha kuwa wanatumia nafasi yao vizuri kutangaza vivutio na
fursa zinazopatikana Mkoani Rukwa kwa wadau ili kuvutia wawekezaji.
Muwezeshaji
wa mafunzo hayo Ndugu Mnaku Mbali ambaye ni Muhariri wa gazeti la
Business Times la jijini Dar es Salaam. Lengo kubwa la mafunzo hayo
alisema ni kuwajengea uwezo zaidi waandishi wa Rukwa waweze kuandika
habari za biashara na uchumi katika uelewa chanya kwa maendeleo ya jamii
ya Rukwa na Taifa kwa ujumla.
Mkurugenzi
na muendeshaji wa Blog ya Pembezoni Kabisa ambaye pia ni mwandishi wa
gazeti la Mwanachi Mussa Mwangoka kulia na Joshua Joel wa ITV na Radio
One wakifuatilia mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki wengine kutoka Rukwa na Katavi wanaoshiriki mafunzo hayo. Wapili kulia ni mdau Ernest Kibada kutoka Katavi.
Washiriki wa Mafunzo hayo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya leo.







No comments:
Post a Comment