Pages

KAPIPI TV

Monday, May 7, 2012

WAANDISHI WA HABARI RUKWA WAPATA MAFUNZO YA SIKU NNE KUHUSU UCHUMI NA BIASHARA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na washiriki wa semina hiyo leo wakati akifungua mafunzo hayo rasmi yaliyoandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kuratibiwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Rukwa (Rukwa Press Club). Mafunzo hayo yatadumu kwa muda wa siku nne na jumla ya washiriki 18 kutoka vyombo vya habari tofauti vya Mikoa ya Rukwa na Katavi wanashiriki. Katika maneno yake ya ufunguzi Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka waandishi wa habari wa Rukwa kuhakikisha kuwa wanatumia nafasi yao vizuri kutangaza vivutio na fursa zinazopatikana Mkoani Rukwa kwa wadau ili kuvutia wawekezaji.
Muwezeshaji wa mafunzo hayo Ndugu Mnaku Mbali ambaye ni Muhariri wa gazeti la Business Times la jijini Dar es Salaam. Lengo kubwa la mafunzo hayo alisema ni kuwajengea uwezo zaidi waandishi wa Rukwa waweze kuandika habari za biashara na uchumi katika uelewa chanya kwa maendeleo ya jamii ya Rukwa na Taifa kwa ujumla.
Mkurugenzi na muendeshaji wa Blog ya Pembezoni Kabisa ambaye pia ni mwandishi wa gazeti la Mwanachi Mussa Mwangoka kulia na Joshua Joel wa ITV na Radio One wakifuatilia mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki wengine kutoka Rukwa na Katavi wanaoshiriki mafunzo hayo. Wapili kulia ni mdau Ernest Kibada kutoka Katavi.
Washiriki wa Mafunzo hayo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya leo.

No comments: