Pages

KAPIPI TV

Thursday, May 10, 2012

MAKAMU WA RAIS DR.GHARIB BILALI AZINDUA TAASISI YA WAKURUGENZI TANZANIA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IODT),  wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika leo Mei 10, 2012 kwenye Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo upande wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Mussa Juma (wa pili kulia) ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora) George Mkuchika na (kushoto) ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Pius Maneno. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi ya Tuzo ya Heshima, Ibrahim Mohamed Kaduma,  kwa kuwa Mwanachama wa Heshima wa Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IODT), wakati wa uzinduzi wa Taasisi hiyo uliofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam leo Mei 10, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja kwa kumbukumbu na Viongozi  na baadhi ya wadau walioshiriki katika hafla hiyo ya uzinduzi, baada ya kuzindua rasmi Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IoDT) uliofanyika leo Mei 10 kwenye Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo vya habari mbalimbali, baada ya kuzindua Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IoDT) leo Mei 10, 2012, uzinduzi uliofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma Hotuba yake wakati akizindua rasmi Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IoDT) alioizindua leo Mei 10, 2012, kwenye Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Picha na Muhidin Sufiani-OMR.

 
NA MAGRETH KINABO - MAELEZO
  
Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal  amesema kwamba Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania(IoDT) itasaidia kuboresha utendaji kazi kwa wakurugenzi wa taaasisi na mashirika mbalimbali  na  kuboresha utawala bora .

Aidha amewataka wananachi kuiunga mkono taasisi hiyo kwa kuwa ni chombo muhimu cha kikachosaidia kutoa mafunzo  kwa viongozi hao na kuwaunganisha  ili kuboresha utawala bora.

Kauli hiyo ilitolewa na Dk. Bilal wakati akizindua taasisi hiyo  leo (jana)  kwenye hafla iliyofanyika katika hoteli ya Haytt Regency jijini Dares Salaam.

“Taasisi hii itakuwa inawachukulia hatua baadhi ya wakurugenzi ambao hawatafuata maadili  na kanuni za IoDT ,ikiwemo kubadilishna mwazo na kupata uzoefu,” alisema Dk. Bilal.

Naye Mwenye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania(IoDT), Pius Maneno alisema  taasisi hiyo ina wanachama 19 ambao  kila mmoja amechangia sh. milioni 10 kwa ajili ya uanzishaji.

 Alisema lengo kuwa la  taasisi hiyo ni kutoa mafunzo  kwa ajili ya kuwajengea uwezo viongozi hao , kujenga mtandao na kuandaa mikutano mbalimbali.

 Katika uzinduzi huo , Profesa Geoffrey Mmari kutoka Chuo Kikuu cha Tuamini(TUDARG) na Mwenyekiti  wa African Life Assurance , Ibrahim  Mohamed  walitunikiwa cheti cha uanachama  wa  heshima.

No comments: