Pages

KAPIPI TV

Thursday, March 15, 2012

UWANJA WA KISASA WA ALLY HASSAN MWINYI TABORA"Hivi UNAZEEKA au UNAKOMAA"

 UWANJA WA ALLY HASSAN MWINYI:Eneo la lango wanaloingilia viongozi na watu maarufu.

 Lango kuu la Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi Tabora uwanja ambao umeanza kutumika tangu mwaka 1988 ukiwa unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi mkoa wa Tabora.
                                          Eneo la nyuma la  uwanja wa Ally Hassan Mwinyi
Wakazi wa mkoa wa Tabora hadi leo wanaamini kuwa uwanja wa Ally Hassan Mwinyi ni uwanja wa kisasa tangu walivyoelezwa na viongozi kuwa wanatozwa fedha za michango mbalimbali ili ujengwe uwanja wa kisasa.

Uwanja huo ambao unamilikiwa kihalali na Chama cha Mapinduzi pamoja na wananchi kuchangia nguvu zao kwa hiari na lazima lakini unazidi kuwashangaza wananchi kama unakomaa au unazeeka mbali na kuchakaa siku hadi siku.

Wananchi baadhi yao wamefanikiwa kuongea na mtandao huu wamedai kuwa hawana mtu wa kumuuliza kuhusu hatma ya uendelezaji wa uwanja huo ambao umetumia fedha nyingi za walala hoi. 

No comments: