Pages

KAPIPI TV

Monday, January 23, 2017

TTCL YATOA MSAADA WA VIFAA VYA MAABARA KWA SHULE ZA SEKONDARI TABORA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI SABA

Baadhi ya maafisa wa Kampuni ya Simu  Tanzania TTCL katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule za Sekondari ya Tabora Wavulana na Wasichana nje ya Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tabora baada ya hafla fupi ya  TTCL kukabidhi msaada wa vifaa vya Maabara ya Sayansi kwa Shule za Sekondari za mkoa wa Tabora.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Aggrey Mwanry akipokea msaada wa vifaa hivyo vya maabara ya Sayansi kutoka kwa Meneja wa TTCL tawi la Tabora Bw.James Mlaguzi,vifaa hivyo vinathamani ya shilingi milioni saba.
Meneja wa TTCL tawi la Tabora Bw.James Mlaguzi akisoma taarifa fupi ya kukabidhi msaada huo wa vifaa vya maabara vilivyogharimu jumla ya shilingi milioni saba.
Meneja wa TTCL tawi la Tabora Bw.James Mlaguzi akikabidhi taarifa aliyoisoma wakati wa kukabidhi vifaa hivyo vya maabara ya Sayansi kwa Shule za Sekondari kwa Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Aggrey Mwanry.
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Tabora Wasichana wakiwa wamebeba masanduku ya vifaa vya maabara vilivyotolewa msaada na Kampuni ya Simu Tanzania TTCL

Baadhi ya maafisa wa TTCL wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya maabara ya sayansi vilivyokabidhiwa na Kampuni hiyo ya simu Tanzania.












Thursday, January 19, 2017

SERIKALI YAONYA WAWEKEZAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO

Na Woinde Shizza,Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa serikali haitasita
kuwachukulia hatua wawekezaji wanaochochea migogoro katika wilaya ya
Ngorongoro na kusababisha uvunjifu wa amani hivyo kuchangia kuzorota kwa
shughuli za maendeleo.



Gambo ameyasema hayo katika ziara yake wilayani Ngorongoro inayolenga
kutatua migogoro wa pori tengefu lenye ukumbwa wa kilomita za mraba elfu
kumi na tano ambapo amekutana na wadau mbalimbali ikiwemo
wawekezaji,wafugaji pamoja na viongozi wa kiserikali.



Amesema kuwa serikali itawaondoa wawekezaji wanaochochea migogoro na
kuwagombanisha wananchi na serikali yao jambo ambalo halitafumbiwa
macho



Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka amesema kuwa wako baadhi ya watu
wanaonufaika na migogoro hiyo hivyo kumalizika kwa migogoro hiyo kutaleta
manufaa kwa wananchi wengi kuliko kunufaisha kundi la watu
wachache



Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo,Kilimo na Uvuvi  ambaye
pia ni Mbunge wa Ngorongoro Wiliam Ole Nasha na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa
Arusha  Lekule Laizer wamesema kuwa utatuzi wa mgogoro huo utasaidia
kuepusha migongano ya kimaslahi na kuchochea shughuli za kimaendeleo badala
ya kutumia muda mwingi katika usuluhishi wa miigogoro hiyo




Mkuu wa Mkoa ameanza Ziara yake leo Wilayani Ngorongo na kesho atatembelea
katika vijiji mbalimbali ikiwa ni katika juhudi za kutatua mgogoro wa pori
tengefu katika wilaya hiyo.

WAKUU WA MASHIRIKA YA UMEME KUTOKA NCHI KUMI ZA EASTERN AFRICA WAKUTANA ARUSHA


Na Woinde Shizza,Arusha

Wakuu wa  mashirika umeme kutoka katika nchi kumi za Afrika zinazozalisha
umeme(Eastern Africa Power pool(EAPP)          zimekutana  jijini arusha
kwa malengo ya kujadili mfumo wa usafirishaji wa umeme ikiwa ni pamoja na
namna wananchi wao watakavyoweza pata nishati ya umeme kwa uraisi tofauti na sasa

 

Hayo yalisemwa na naibu katibu mkuu wizara ya nishati na madini Dkt.Juliana palangyo alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wakuu wa mashirika ya umeme katika nchi hizo za eastern Africa power
pool(eapp)mapema leo

 

Palangyo alisema kuwa lengo halisi ni kuweza kujadili mambo mbalimbali
yahusuyo nishati ya umeme kwa watumiaji wake kwani  kuna uwezekano  mkubwa wa nchi zote zilizo kwenye umoja huo.

 

Alisema kwa sasa yapo baadhi ya makampuni ambayo yalikuwa yanauza umeme kwa gharama kubwa hasa kwa wananchi ambao hawajapata huduma hiyo ya umeme lakini kupitia umoja huo wataweza kupata nishati hiyo kwa gharama nafuu.
 

"Hizi nchi za eastern tumekutana hapa ili tujadili namna ambayo tunaayo
wanayoweza kutafuta namna ya kuzalisha umeme kwa bei nafuu na kisha nchi
hiyo itaweza kuuza umeme  kwa bei ndogo"aliongeza palangyo.

 

Hata  hivyo kwa upande  kaimu meneja uhusiano wa shirika la tanesco  Leila
Muhaji alisema kuwa katika mkutano huo pia watajadili namna ambavyo
tanzania itajenga njia ya usafirishaji wa umeme wa njia ya maji ambayo
itatoka nchi ya tanzania kwenda kenya,zambia,pamoja na nchi nyingine

Muhaji alisema kuwa tanzania itanufaika na ujenzi wa njia hizo hivyo jamiii
itanufaika kwa kiwango kikubwa sana kama ilivyo kwenye nchi ambazo
zimeeendelea duniani.

 

"Hataivyo mara baada ya huu mkutano wa wakuu wa nchi zinazolisha umeme
tunatarajia pia kuwepo na wadau wengine ambao ni mawaziri kutoka nchi zote ambao nao sasa wataweza kuweka mambo sawa ili huduma iweze kumfikia mlengwa"aliongeza Muhaji

Alimalizia kwa kutaja nchi ambazo zina unda umoja huo kuwa ni  Tanzania ,Kenya,Uganda ,Rwanda ,Burundi ,Sudan , Dr congo, Ethiopia ,Djbout, Libya pamoja na Egypt.

SEMINA YA KUPEANA TAARIFA KUHUSU UTOAJI MIMBA USIO SALAMA

1
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha wanasheria wanawake TAWLA Bi Tike Mwambipile akifungua semina ya kuhamasisha wadau wa Kutetea haki za wanawake na kujadili madhara ya utoaji mimba usio salama hapa Tanzania kwa kushirikishana matokeo ya utafiti uliofanyika hivi karibuni wa matukio ya utoaji mimba usio salama pamoja na huduma za baada ya utoaji mimba usio salama hapa Tanzania.
2
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakifuatilia mada kadhaa zilizokuwa zikitolewa katika semina hiyo.
3
Dk. Pensiens Mapunda Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Afya na Tiba Hurbert Kairuki HKMU akielezea jambo wakati wa semina hiyo.
4
Baadhi ya washiriki wakisikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa katika semina hiyo.
7
5
Washiriki wa semina hiyo wakiwa katika picha ya pamoja.
...........................................................................
Lengo la semina hii ni kujadili swala nyeti linaloigusa jamii yetu ya Kitanzania na wadau muhimu katika kutetea haki za wanawake katika kuhakikisha ustawi wa mwanamke unaendelea vizuri katika jamii yetu
Pamoja na kazi tunazofanya za kutoa huduma ya msaada na ushauri wa kisheria kwa wanawake na watoto, TAWLA imejikita pia katika kupigania haki za wanawake na usawa wa kijinsia hapa nchini ikiwemo Haki ya Afya ya Uzazi. Hii ni kwa sababu, TAWLA inatambua umuhimu wa haki za kijinsia na Afya ya Uzazi katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii na zaidi sana kuondoa imani potofu kuhusu afya ya uzazi.
TAWLA kupitia vituo vyake vya msaada wa kisheria na mijadala ya kijamii (Community Conversation) tulipata taarifa za madhara na vifo vitokanavyo na utoaji mimba usio salama ambazo zilitushtusha na kutugusa sana na ndio maana tukaonelea kuwa ni vyema takafanya utafiti juu ya suala hili ili kuona ni kwa namna gani tunaweza kuisaidia jamii yetu kwa kushirikiana na wadau muhimu katika swala hili, ili kupunguza au kuondoa kabisa vifo vya akina mama na wasichana vitokanavyo na utoaji mimba usio salama.
Takwimu za tafiti ya Guttmacher zinaonyesha kwamba utoaji mimba usio salama ni sababu ya pili ya vifo vya akina mama na wasichana hapa nchini kwa maana kwamba:
(1) Kila mwaka wanawake wa Kitanzania 405,000 hutoa mimba kwa usiri karibu wote na kwamba 40% hupata matatizo ambayo yanahitaji matibabu:
(2) Kila mwaka wanawake wa Kitanzania milioni moja hupata mimba zisizotarajiwa ambazo 39% ya wanawake hao huishia kwenye utoaji mimba:
(3) 60% ya wanawake wa Tanzania wenye matatizo ya utoaji mimba hawapati huduma ya matibabu wanayoihitaji:
(4) Kila mwanamke 1 kati ya wanawake 5 nchini Tanzania ana mahitaji yasiyofikiwa ya uzazi wa mpango
Ni kwa misingi hiyo basi kongamano hili lina malengo makuu yafuatayo:
(1) kuhamasisha washiriki na kujadili madhara ya utoaji mimba usio salama hapa Tanzania kwa kushirikishana matokeo ya utafiti uliofanyika hivi karibuni wa matukio ya utoaji mimba usio salama pamoja na huduma za baada ya utoaji mimba usio salama hapa Tanzania:
(2) Kushirikishana matokeo ya utafiti uliofanyika hivi karibuni wa matukio ya utoaji mimba usio salama pamoja na huduma za baada ya utoaji mimba usio salama hapa Tanzania:
(3) Kubadilishana uzoefu:
(4) Kufanya uchechemuzi wa kuingizwa kwenye Sheria za Tanzania vipengele vinavyohusu haki ya Afya ya Uzazi vilivyopo kwenye Mkataba wa Nyongeza wa Afrika (Maputo Protocol) juu ya Haki za Wanawake:
(5) Kuwakutanisha wadau muhimu juu ya swala hili ili kujadili kuhusu Sheria na Sera zinazohusu Haki ya Afya ya Uzazi na utoaji mimba ulio salama hapa Tanzania.
Pamoja na madhumuni yaliyoiainisha hapo juu, semina hii inakusudia kutambua aina ya michango ambayo wadau mbali mbali waliopo hapa leo wanaweza kutoa katika kupunguza vifo vya akina mama vinavyotokana na utoaji mimba usio salama na madhara yake hapa Tanzania
Chama Cha Wanasheria Wanawake Tanzania kinaamini kwamba, kutambua Haki ya Afya ya Uzazi ni muhimu katika kufikia lengo la kupigania haki za wanawake na usawa wa kijinsia hapa nchini.. Lengo hili linaweza kukamilika endapo tu kila mmoja wetu katika ukumbi huu atajitoa katika kuhakikisha kuwa, wototo wetu wa kike, dada zetu, mama zetu na wanawake wote hapa nchini hawafi kwa sababu ya utoaji mimba usio salama.
Tunatambua kazi za Taasisi/ofisi zenu katika kuletea haki za binadamu, haki za wanawake na usawa wa kijinsia hapa Tanzania, ndio maana tumeomba ushiriki wenu ili kufanikisha lengo hili la kuleta haki katika jamii yetu.
Washiriki wa semina hii ni Baadhi ya wadau kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Wizara ya Katiba na Sheria na baadhi ya Asasi zisizo za kiraia zinazoshughulikia maswala ya haki za wanawake Nchini Tanzania.

SHIRIKA LA UNDER THE SAME SUN LATOA ELIMU KWA WADAU KUHUSU UALIBINO JIJINI MWANZA

Afisa Maendeleo ya Jamii mkoani Mwanza Isaac Ndassa, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, kwenye ufunguzi wa semina kwa wadau wanaosaidia kutokomeza ukatili dhidi ya watu wenye ualibino, inayofanyika kwa siku nne kuanzia leo Jijini Mwanza. 

Semina hiyo imeandaliwa na Shirika la kimataifa la kutetea haki za watu wenye ualibino la Under The Same Sun ambapo imelenga kupanua uelewa kwa wanajamii/ wadau  kuhusu ualibino ili kusaidia kupambana na ukatili kwa watu wenye hali hiyo.
Binagi Media Group
Mwasisi wa Shirika la kimataifa la kutetea haki za watu wenye ualibino la Under The Same Sun, lenye makao yake makuu nchini Canada, Peter Ash, akizungumza na wanahabari kwenye semina hiyo.
Mkurugenzi wa Shirika la kimataifa la kutetea haki za watu wenye ualibino la Under The Same Sun nchini Tanzania, Bi.Vicky Ntetema, akifafanua jambo kwenye semina hiyo.
Mkufunzi Dr.George Rhoades kutoka nchini Marekani, akitoa 
 Shirika la kimataifa la kutetea haki za watu wenye ualibino duniani, Under The Same Sun, limebainisha kwamba vitendo vya ukatili dhidi ya watu wenye ualibino nchini vinaendelea kupungua.

Mkurugenzi wa shirika hilo nchini, Vicky Ntetema, ameyasema hayo leo Jijini Mwanza kwenye semna kwa wadau wanaofanya kazi kwa ukaribu na watu wenye uaribino kutoka taasisi mbalimbali ikiwemo za kijamii, elimu na afya.

Ntetema amesema elimu inayoendelea kutolewa kwa wanajamii imesaidia kupunguza ukatili kwa watu wenye ualibino ikiwemo kukatwa viungo na mauaji licha ya kwamba kumekuwepo taarifa za makaburi ya watu wenye ualibino waliofariki kufukuliwa katika mikoa ya Kagera, Mbeya na Morogoro.

Mwasisi wa shirika hilo lenye makao yake makuu nchini Canada, Peter Ash, ameeleza kufurahishwa na maendeleo ya wanafunzi zaidi ya 300 wenye ualibino wanaosomeshwa na shirika hilo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ambapo amewasihi wanajamii kuondokana imani potofu juu ya watu wenye ualibino ili kutokomeza ukatili dhidi yao.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mwanza, Afisa Maendeleo ya Jamii mkoani Mwanza Isaac Ndassa, amesema serikali imelenga kuhakikisha vitendo vya ukatili kwa watu wenye ualibino vinatokomezwa ambapo amesisitiza elimu zaidi kuendelea kutolewa kwa wananchi ili kufanikisha lengo hilo.

MSIMU WA 15 WA MASHINDANO YA KIMATAIFA YA MBIO ZA KILIMANJARO PREMIUM LAGER MARATHON 2017

Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akizungumza wakati wa uzinduzi wa msimu wa 15 wa mbio za kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2017 ,uzinduzi uliofanyika Kibo Palace Home mjini Moshi.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi huo.
Meneja Mauzo wa Kampuni ya TBL mikoa ya Kilimanjaro na Tanga ,Richard Temba akizungumza wakati wa uzinduzi huo,TBL ndio wadhamini wakuu wa Mbio hizo kupitia Bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za mkononi ya TIGO ,Kanda ya Kaskazini,George Lugata akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2017 ,Tigo wanadhamini mbio hizo kwa upande wa Mbio za Kilometa 21
Baadhi ya wageni waalikwa katika hafla fupi ya uzinduzi wa mbio hizo.
Meneja Masoko wa Kampuni ya GAPCO Tanzania ,Caroline Kakwezi akizingumza wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi wa mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2017,GAPCO wanadhamini mbio za Kilometa 10 kwa upande wa walemavu.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Executive Solution ,Aggrey Mareale ambao ndio waratibu wa mbio hizo akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Mwakiishi wa Kampuni ya Sukari ya TPC,Allen Maro akizungumza wakati wa hafla hiyo,TPC pia ni wadhamini wa mashindano hayo ya kimataifa ambayo hufanyika kila mwaka.
Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya kuchimba Dhahabu ya Geita Gold Mining (GGM) Tenga B Tenga akizungumza wakati wa uzinduzi huo,GGM wakiwa ni wadhamini wapya katika mashindano hayo.
Mwenyekiti wa Chama cha Riadha mkoa wa Kilimanjaro (KAA) Liston Methacha akizungumza kwa niaba ya shirikisho la Riadha Tanzania katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Wildfrontiers,John Hudson ambao ndio waandaaji wa mbio hizo akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Kibo Palace,Vicent Lasway akizungumza katika hafla hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akizungumza katika hafla hiyo.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akiwapongeza wawakilishi wa kampuni zilizojitokeza kudhamini Mbio hizo za kimataifa.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akiwa na wawakilishi wa kampuni zinazodhamini mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Marathoni 2017 pamoja na jeshi la Polisi ,akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mbio hizo.
Mgeni rasmi katika hafla fupi ya uzinduzi wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager Marathoni 2017 akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa Mbio hizo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kaskazini. 

TANZANIA KUANZA KUTUMIA MFUMO WA DIRISHA MOJA LA HUDUMA

Kaimu Kamishna Mkuu TRA, Mary Maganga.
Katika kuhakikisha inaboresha huduma kwa wafanyabiashara ambao wanaingiza mizigo nchini kwa njia ya bandari, mipaka na viwanja vya ndege, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imeeleza mpango wa Serikali wa kuanza kutumia mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System) ambao kwa hakika utamaliza tatizo la mizigo kukaa muda mrefu kwa sababu ya kukosekana vibali. Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika mafunzo ya siku moja kuhusu mfumo wa Dirisha Moja la Huduma kwa taasisi zinazotoa vibali na wafanyabiashara, Meneja Mfumo wa Kieletroniki wa Dirisha Moja la Huduma, Tinka Felix alisema lengo la kuanza kutumia mfumo huo ni kuboresha huduma ambazo wanazitumia sasa ili wafanyabiashara wanaoingiza mizigo nchini waweze kuipata kwa haraka kuliko ilivyo sasa.
Meneja Mfumo wa Kieletroniki wa Dirisha Moja la Huduma, Tinka Felix akizungumza kuhusu mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System). (Picha zote na Rabi Hume - MO DEWJI BLOG)
“Ni mpango wa Serikali kuboresha huduma kwa wateja kwa kupunguza muda wa kutoa mizigo bandarini au mipakani au kwenye viwanja vya ndege, kupitia mfumo huu wateja hawatakuwa wakienda kwenye idara na taasisi za Serikali na badala yake wakiwa hukohuko kwenye ofisi zao wataweza kuomba na kupata vibali na kupata bili za malizo kwenda kulipa benki, mfumo pia utafanya kazi na benki," alisema Felix. Alisema Tanzania haitakuwa nchi ya kwanza kutumia mfumo huo na mataifa mengi yanautumia ili kurahisisha huduma kutolewa kwa haraka kwani mfumo wa sasa wa forodha (tancis system) unashindwa kufanya kazi kwa haraka jambo ambalo linasababisha mizigo kuchelewa kutolewa kutokana na muda mrefu mmiliki kutumia kutafuta vibali.
Mkurugenzi wa Sera Utafiti Na Ushauri wa TPSF, Gili Teri akizungumza faida za kutumia mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System).
“Mfumo wa sasa ili mtu apate kibali anatakiwa atembelee hizo ofisi hata mara 10 na baadhi ya ofisi wanataka vibali zaidi ya kimoja lakini mfumo huu wa sasa muda ambao unatumika kuomba vibali utapungua na tunategemea kuokoa Dola milioni 65 kwa kutumia tu mfumo wa electronic single window system,” alisema Felix. Alisema kwa sasa kuna taasisi za Serikali 47 ambazo zinatoa vibali lakini mfumo wa Dirisha Moja la Huduma utatumiwa na taasisi 32 ambazo kwa pamoja zitakuwa zikitoa vibali 106. Aidha alisema Serikali imeagiza kuwa mfumo huo uanze kutumika baada ya mwaka mmoja hivyo wanategemea kuanzia mwakani mfumo ambao watakuwa wakitumia utakuwa ni wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System) ambao utawezesha wafanyabiashara ambao wanatoa mizigo kupitia bandari, mipaka au viwanja vya ndege kupata vibali kwa haraka. Na Rabi Hume, MO DEWJI BLOG
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo ya siku moja wakiuliza maswali na kutoa maoni kuhusu mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System).