Pages

KAPIPI TV

Tuesday, October 4, 2016

NHC YAKABIDHI MARARASA SHULE YA MSINGI SAKU WILAYA YA TEMEKE

1
Meya wa Halmashauri ya Temeke Abdallah Chaurembo akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa madarasa ya shule ya msingi Saku wilayani Temeke wakati wa makabidhiano yaliyofanyika shuleni hapo jana, Madarasa hayo yamejengwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC kwa gharama ya shilingi milioni 32 , makabidhiano hayo yamefanyika shuleni hapo mwishoni mwa wiki kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Nassib Mmbaga , Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari na Mkuu wa wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaviva.
2
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akifungua mlango mara baada ya makabidhiano hayo kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw. Nassib Mmbaga na kushoto ni Meya wa Halmashauri ya Temeke Abdallah Chaurembo.
3
Haya ndiyo madarasa yaliyojengwa na Shirika la Nyumba NHC kwa gharama ya shilingi Milioni 32 katika shule ya msingi Saku.
5
Baadhi ya wanafunzi wakikokotoa hesabu walizopewa na Mh. Meya wa Manispaa ya Temeke Halmashauri ya wilaya ya Mh. Temeke Abdallah Chaurembo.
6
Mh. Meya wa Halmashauri ya wilaya ya Temeke Abdallah Chaurembo akiwafundisha hesabu wanafunzi wa darasa la sita katika shule ya ya msingi Saku.
7
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi wenzake mara baada ya makabidhiano ya madarasa hayo.
8
Mh. Meya wa Manispaa ya Temeke Halmashauri ya wilaya ya Mh. Temeke Abdallah Chaurembo akikabidhi vitabu kwa mwanafunzi Leokadia Projestus wa darasa la sita shule ya msingi Saku katikati ni Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari
9
Mkuu wa wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaviva. akizungumza na wanafunzi.
10 11
mwanafunzi Leokadia Projestus wa darasa la sita shule ya msingi Saku akitoa hotuba kwa niaba ya wanafuzni wenzake.
12
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akizungumza neno katika makabidhiano hayo.
13
Wanafunzi wakiimba kwaya wakati wa makabidhiano hao

Friday, September 23, 2016

WANAFUNZI KISARAWE NA TABORA KUNUFAINIKA NA MSAADA WA MADAWATI KUPITIA KAMPENI YA SIMAMA KAA INAYOFANYWA NA DR.AMON MKONGA FOUNDATION

Stella Pius Afisa Mawasiliano wa Kampuni ya simu za mkononi ya Halotel(Kulia) akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo kuhusu kampeni ya Madawati mkoani Tabora , katikati ni Mwenyekiti wa Dr. Amon Foundation Bw. Amon Mkoga na kushoto ni Ngo Duy Truong Meneja Masoko Halotel
Mwenyekiti wa Dr. Amon Foundation Bw. Amon Mkoga katikati ,  Ngo Duy Truong Meneja Masoko Halotel, Kushoto na Stella Pius  Meneja Mawasiliano wa Halotel wakionyesha kwa waandishi wa habari mfano wa Madawati ambayo watakuwa wanayagawa kupitia kampeni ya Simama Kaa Desk  itakayofanyika mkoani Tabora na Pwani.
 
Mwenyekiti wa Dr. Amon Foundation Bw. Amon Mkoga  ametoa mchango wa madawati  katika kampeni ya uchangiaji madawati  kwa udhamini wa mtandao wa simu za mkononi wa Halotel hii leo katika ukumbi wa Idara ya Habari  Maelezo jijini Dar-es-Salaam.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Amon Mkoga amesema kuwa ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ,wameandaa kampeni ya “Simama Kaa Desk” Kampeni.,  itakayosaidia kupunguza uhaba wa madawati ikidhaminiwa na Kampuni ya Simu ya  Halotel.
 
“Lengo kubwa la kampeni hii ya “Simma Kaa Desk”   ni kuchangia na kupunguza upungufu  wa madawati katika shule za msingi na sekondari  ili kumuunga mkono rais wa  Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, Kampeni hiyo  itaanzia katika mkoa wa Tabora na Pwani tukiwa pamoja na Kampuni ya Halotel.”
 
Aidha afisa mawasiliano wa Halotel Stella Pius amesema kuwa Halotel itakuwa pamoja na Dr Mkoga Foundation kuhakikisha kwamba watakuwa bega kwa bega ili kuwasilisha mchango wa madawati katika elimu.
 
“Ikiwa ni pamoja na kuunga mkono uchangiaji wa madawati Haloteli tutahakikisha katika kampeni hii ya Simama Kaa Desk kampeni,  tunawakilisha mchango wetu tukishirikiana na Dr Amoni Foundation kupitia kampeni hii ambapo  tunaamini kuwa ni njia pekee ya kupunguza uhaba wa madawati mashuleni.”
 
Licha ya hayo pia kutakuwa na burudani ya mziki wakati wa kukabidhi madawati hayo ambayo italetwa na  kundi la muziki wa kizazi kipya la Mabaga Fresh la jijini Dar es salaam.
 

AMON MKOGA
MANAGING DIRECTOR
CHIEF PROMOTIONS
P.O BOX 78566
MOBILE 0755 638 004/0784 772628/0655 638 004
EMAIL dramontz2002@yahoo.com
WEBSITE www.chiefpromotions.or.tz
WEBSITE www.mtemimilambofestival.blogspot.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA

MTAA WA MASAKI JIJINI DAR ES SALAAM WAANZISHA TOVUTI YAKE KWA AJILI YA MAENDELEO

 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita (kulia), akizungumza katika na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa Tovuti ya mtaa huo iliyofanyika Hoteli ya Best Western Plus Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta. 
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita, akitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya tovuti hiyo.
 Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (katikati), akikata utepe kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kionondoni, aliyekuwa mgeni rasmi, kuashiria uzinduzi rasmi wa tovuti hiyo. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta, Mwenyekiti wa mtaa huo, Kimweri Mhita, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Masaki, Richard Mwakyulu na Mjumbe wa Kamati ya Mtaa huo, Rose Mkisi.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea kabla ya uzinduzi huo.
 Wajumbe wa kamati ya mtaa huo wakishiriki kwenye uzinduzi huo.
 Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo,  Peter Mkongereze akizungumza kwenye hafla hiyo.
 Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta (kulia), akizungumza katika hafla hiyo.
 Mmoja wa waendeshaji wa tovuti hiyo, Benjamin Chaula (kulia), akielezea jinsi itakavyokuwa ikifanya kazi.Kushoto ni Norbert Baranyikwa.
 Makofi yakipigwa baada ya uzinduzi wa tovuti hiyo.
Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.


Na Dotto Mwaibale

SERIKALI ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam imezindua tovuti yake ili kurahisisha mawasiliano na shughuli za maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tovuti hiyo Dar es Salaam leo asubuhi Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Masaki, Kimweri Mhita alisema tovuti hiyo imeanzishwa kwa lengo la  kuwasiliana na kuwashirikisha katika shughuli za maendeleo raia wa kigeni wanaoishi katika mtaa huo.

"Kutokana na jiografia ya eneo letu kulikuwa na changamoto kuwa ya kuwashirikisha wenzetu katika masuala mbalimbali kutokana na kutokuwa na mawasiliano tukaona tuanzishe tovuti yetu itakayosaidia kuondoa changamoto hiyo" alisema Mhita.

Alisema kupitia tovuti hiyo itasaidia kuwatambua wafanyabiashara waliopo katika mtaa huo ambao wameanza kujisajili pamoja na wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, Katibu Tarafa wa Kata ya Magomeni, Fullgence Sakafu alisema kuanzishwa kwa tovuti hiyo katika wilaya hoyo wilaya hiyo mtaa huo umeonesha njia hivyo akaomba mitaa mingine kuiga mfano huo.


Alisema tovuti hiyo itasaidia kuweka wazi mipango ya maendeleo katika mtaa huo pamoja na kuhimizana kwenye kampeni ya kufanya usafi inayoendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuwa.

Wednesday, September 21, 2016

MADEREVA 10 WA TANZANIA WALIOTEKWA NCHINI CONGO WAREJEA NCHINI NA KUSEMA WALIPONEA TUNDU LA SINDANO KUUAWA

 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba (katikati), akizungumza na madereva 10 wa Tanzania waliotekwa na watu wanaodaiwa kuwa ni waasi Jamhuri ya Demokrasia ya Conco (DRC), wakati wa hafla fupi ya kuwapokea iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam leo jioni. Kulia ni Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba na kushoto ni Mkurugenzi  Idara ya Afrika katika wizara hiyo, Balozi Samweli Shelukindo.
 Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.
 Mmiliki wa Kampuni ya Simba Logistic ambayo magari yake na madereva walitekwa, Azim Dewj (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo ya kuwapokea madereva hao.
 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakisubiri kuchukua taarifa za kuwapokea madereva hao.
 Madereva hao wakipokelewa uwanjani hapo.
 Madereva hao wakiwa chumba cha mkutano cha uwanja huo wakati wa mapokezi yao.
Dereva  Mbwana Said (kulia), akielezea jinsi walivyotekwa.
 Dereva Kumbuka Seleman (kulia), akisimulia jinsi alivyotoroka na kutoa taarifa ya kutekwa kwao.
Dereva  Athuman Fadhili (kulia), akisimulia walivyookolewa na majeshi ya Congo na jinsi walivyojificha porini na kutembea umbali mrefu kwa kutambaa ambapo ilifika wakati waliomba bora wafe kuliko mateso waliyokuwa wakipata.
 Hapa ni furaha ya kukutana na ndugu jamaa na wafanyakazi wenzao.
 Picha ya pamoja na viongozi waliowapokea.
 Ndugu, Jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzao wakiwa nje ya jengo la VIP uwanjani hapo wakisubiri kuwapokea.
 Mapokezi yakiendelea.
Ni furaha ya kukutana na wapendwa wao.
Hapa Dereva Mbwana Said akikumbatia na mjomba wake Kassim Salim katika hafla hiyo kwa Mbwana ilikuwa ni furaha na majonzi. 
Mbwana Said (katikati), aamini macho yake baada ya kukutana na mke wake Mariam pamoja na mtoto wake Kauzari.

Na Dotto Mwaibale

MADEREVA 10 wa Tanzania waliotekwa na watu  wanaodhaniwa ni waasi Jamhuri ya Demokraia ya Congo (DRC) wamesema waliponea tundu la sindano kuuawa.

Kauli hiyo imetolewa na madereva hao katika hafla ya kuwapokelewa iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam leo jioni.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Mbwana Said alisema analishukuru jeshi la Congo kwa jitihada kubwa walioifanya kwa ajili ya kuokoa maisha yao." 

" Tunaishukuru serikali ya Congo kwa kutuokoa kwani tulikuwa katika wakati mgumu na leo kuungana tena na ndugu zetu" alisema Said.

Alisema walilazimia kutembea kwa muda mrefu huku risasi zikirindima kati ya majeshi ya serikali na waasi hao hadi walipofanikiwa kutuokowa kutoka kwenye mikono ya waasi hao. 

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba aliishukuru serikali ya Congo kwa jitihada iliyoifanya na kufanikiwa kuwaokoa madereva hao.

Balozi wa Congo nchini Jean Mutamba aliwataka madereva hao kuacha viza na nyaraka zao ubalozini pindi wanapo safiri na kurudi ili iwe rahisi kuwatambua pale wanapopata matatizo.

"Tukio hilo limetokea kwa bahati mbaya na kutoa wito kuwa waendelee kusafiri kwa kufuata taratibu zilizopo," alisema Mutamba.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712727062)



WATANZANIA WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA


Na Rabi Hume, MO BLOG

Kutokana na kuwepo na shughuli nyingi za kibinadamu ambazo zinaharibu mazingira, watanzania nchini kote wametakiwa kuwa makini kwa kutunza mazingira yanayowazunguka ili kuepusha matatizo ambayo yanaweza kutokea kutokana na kushindwa kudhibiti vitendo vya uharibifu mazingira.

Rai hio imetolewa na Balozi Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa Geneva, Uswisi, Modest Mero katika warsha ya kujadili kuhusu kilimo na biashara iliyoandaliwa na Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF).

Balozi Mero alisema kuwa nchi nyingi duniani zimekuwa na shughuli nyingi ambazo zinaharibu mazingira hali ambayo inatishia maisha ya vizazi vijavyo na hivyo ni vyema watanzania wakaanza kuchukua hatua kwa kutunza mazingira ili kuepeusha athari ambazo zitajitokeza kwa miaka ijayo.

"Dunia nzima watu wanakata miti, wanachoma majani mashambani lakini hawajui kama kuna vitu vya muhimu wanaua ardhini, na mimi niwambie watanzania wawe makini wasikate miti ambayo inawazunguka huo ni uharibifu wa mazingira," alisema Balozi Mero.
Balozi Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa Geneva, Uswisi, Modest Mero akizungumza na washiriki wa warsha iliyoandaliwa na Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), ikizungumza kuhusu kilimo na biashara. (Picha zote na Rabi Hume - MO BLOG)

Aidha alisema kuwa kwa sehemu kubwa watu ambao wanachangia vitendo hivyo ni wafanyabiashara na hivyo kuwataka wafanyabiashara kuacha vitendo vya kukata miti ikiwa bado haijafika katika muda sahihi ambao wanaruhusiwa kuikata.

"Wafanyabiashara wanakata sana miti, lakini wajue kuwa wakikata hovyo baadae wataikosa hiyo miti, ili mazingira yanayotuzunguka yawe mazuri inabidi kuyatunza ila tukitumia vibaya hata vyanzo vya maji vitakauka," alisema Mero.
Mtafiti Mshiriki wa ESRF, Dkt. Osward Mashindano akizungumzia malengo ya warsha hiyo.

Nae Mtafiti Mshiriki wa ESRF, Dkt. Osward Mashindano alisema warsha hiyo ina lengo la kuzungumzia jinsi gani kilimo, biashara, usalama wa chakula na mabadiliko ya hali ya nchi jinsi ambavyo vinaweza kutoa matokeo mazuri au mabaya.

Alisema kuwa pamoja na matokeo hayo, pia wanazungumzia ni hatua gani inafaa kuchukuliwa iwapo matokeo yanakuwa ni mazuri au mabaya ili kumsaidia mkulima mdogo kwa jinsi gani anaweza kufaidika na kilimo chake na kuepuka kupata hasara.

"Bidhaa kwa sasa zinatakiwa kuongezwa thamani, bidhaa kama haijaboreshwa haiwezi kuwa na soko zuri la ndani na hata nje ya nchi, tunataka kujua matokeo yake yanakuwaje maana biashara inavutia kutokana na soko lake lilivyo,

"Watu wanatakiwa kujua matokeo kama ni mazuri wafanyaje kama wengine wanaweza wanachangamkia fursa au kama ni mabaya wajue jinsi gani wanaweza kupunguza athari hizo ... tunatazama hilo maana hata sera zilizopo sasa hazisemi hatua gani ichukuliwe kama matokeo ni mabaya au mazuri," alisema Dkt. Mashindano.

Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wakihangia mada zilizokuwa zikijadiliwa.



Baadhi ya washiriki wa warsha ya kujadili kuhusu kilimo na biashara iliyoandaliwa na Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF).



Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.