Mwenyekiti wa Dr. Amon
Foundation Bw. Amon Mkoga ametoa mchango wa madawati katika kampeni
ya uchangiaji madawati kwa udhamini wa mtandao wa simu za mkononi wa
Halotel hii leo katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini
Dar-es-Salaam.
Akizungumza na waandishi wa
habari Amon Mkoga amesema kuwa ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano
ya Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ,wameandaa kampeni ya “Simama Kaa Desk”
Kampeni., itakayosaidia kupunguza uhaba wa madawati ikidhaminiwa na
Kampuni ya Simu ya Halotel.
“Lengo kubwa la kampeni hii
ya “Simma Kaa Desk” ni kuchangia na kupunguza upungufu wa
madawati katika shule za msingi na sekondari ili kumuunga mkono rais
wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, Kampeni hiyo itaanzia katika
mkoa wa Tabora na Pwani tukiwa pamoja na Kampuni ya Halotel.”
Aidha afisa mawasiliano wa
Halotel Stella Pius amesema kuwa Halotel itakuwa pamoja na Dr Mkoga Foundation
kuhakikisha kwamba watakuwa bega kwa bega ili kuwasilisha mchango wa madawati
katika elimu.
“Ikiwa ni pamoja na kuunga
mkono uchangiaji wa madawati Haloteli tutahakikisha katika kampeni hii ya
Simama Kaa Desk kampeni, tunawakilisha mchango wetu tukishirikiana na Dr
Amoni Foundation kupitia kampeni hii ambapo tunaamini kuwa ni njia pekee
ya kupunguza uhaba wa madawati mashuleni.”
Licha ya hayo pia kutakuwa na
burudani ya mziki wakati wa kukabidhi madawati hayo ambayo italetwa na
kundi la muziki wa kizazi kipya la Mabaga Fresh la jijini Dar es salaam.
MANAGING DIRECTOR
CHIEF PROMOTIONS
P.O BOX 78566
MOBILE 0755 638 004/0784 772628/0655 638 004
EMAIL dramontz2002@yahoo.com
WEBSITE www.chiefpromotions.or.tz
WEBSITE www.mtemimilambofestival.blogspot.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
CHIEF PROMOTIONS
P.O BOX 78566
MOBILE 0755 638 004/0784 772628/0655 638 004
EMAIL dramontz2002@yahoo.com
WEBSITE www.chiefpromotions.or.tz
WEBSITE www.mtemimilambofestival.blogspot.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
No comments:
Post a Comment