Pages

KAPIPI TV

Thursday, May 26, 2016

BIMA YA AFYA KUANZA HUDUMA YA MAMA NA MWANA

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Bw Bernard Konga, akitoa salamu za Mfuko kwa wajumbe wa baraza hilo lilikofanyika katika ukumbi wa Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wanaohudhuria kikao
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Bw Bernard Konga,(katikati) akizungumza na baadhi ya wajumbe ndugu Gudluck Kirambe, kulia na meneja wa mkoa wa Kilimanjaro ndugu Fidelis Stephen.

Kilimanjaro

MFUKO wa taifa wa bima ya afya (NHIF) utaanzisha huduma mpya ya itakayojulikana kama mama na mwana afya kadi ili kuboresha huduma za bima ya afya kwa kundi hilo ambalo lipo katika uhitaji maalum.

Kauli hiyo imetolewa mjini hapa na kaimu mkurugenzi mkuu wa mfuko huo,bw Bernard Konga alipokuwa akitoa salamu za Mfuko huo kwa wajumbe wa baraza hili linaloanza kikao chake mjini hapa.

Bw konga amesema lengo la huduma hiyo mpya ni kuwawezesha kina Mama Wajawazito na Watoto kupata huduma za matibabu za uhakika zitolewazo na mfuko wa taifa wa Bima ya afya.

Chimbuko la hatua hiyo linafuatia matokeo mazuri na mafanikio makubwa ya mradi unaoendeshwa kwa pamoja kati ya NHIF na benki ya maendeleo ya ujerumani ya KfW katika mikoa ya Tanga na Mbeya. hatua iliyofikiwa kwa sasa ni kupata maoni ya wananchi kabla ya kuanza utekelezaji wake katika mwaka wa fedha wa 2016/17.

Awali, akifungua kikao cha baraza hilo, mkuu wa wilaya ya Siha Dr Charles Mlingwa, aliyemuwakilisha mkuu wa mkoa huo Meck Sadiki,aliushukuru mfuko huo kwa kuwa wabunifu katika utoaji wa huduma kwa
makundi mbalimbali kwa kuzingatia uwezo wao wa kulipa. Ameutaka mfuko huo kutafsiri hotuba za mheshimiwa Rais kuhusu dhana ya afya bora kwa wote kwa kuweka mikakati katika eneo hilo.

Dr Mlingwa pia amesema wilaya ya Siha ni moja ya wilaya zilizofanikiwa sana kuboresha huduma za matibabu ambapo kwa miaka miwili mfululizo imeweza kupunguza sana vifo wa watoto wachanga na kufikia mtoto mmoja kwa kila watoto laki moja.

Wednesday, May 25, 2016

MAONYESHO YA BIDHAA ZA PLASTIKI, MPIRA, KEMIKALI ZA PETROLI NA UJENZI KUFANYIKA MEI 27-29 MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM

Meneja Mkuu wa Expo One,  Ahmed Barakat, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo jioni kuhusu maonyesho hayo.
Balozi wa Tanzania nchini Misri, Balozi Hamza Mohamed Hamza akizungumza katika mkutano huo.
Taswira meza kuu.
Wadau wakiwa kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa Africa-PPB Tanzania, Mohamed Sami akizungumza katika mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Khaled Abu El M karem akizungumza kwenye mkutano huo.
Na Doto Mwaibale

TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa maonesho ya kwanza  ya bidhaa za plastiki, mpira, kemikali za petrol na ujenzi  yanayotarajiwa kufanyika katika  Mei 27 hadi 29 mwaka huu katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Mlimani City jijiniDare s Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Meneja Mkuu wa Expo One,  Ahmed Barakat,  alisema nchi zote za Afrika Mashariki na kati zitashiriki katika maonesho hayo.

Alisema Maonesho ya Afrika –PPB-EXPRO yatakuwa ni jukwaa la kipekee la bidhaa mpya  na yatatoa mwanya wa kuyaelewa  masoko yake ambayo hayafahamiki vizuri.

 “Maonesho haya yamebuniwa kwa lengo la  kukuza umoja miongoni mwa Waafrika kwa kuimarisha mahusiano ya kibiashara  kati ya Misri na Tanzania na hali kadhalika  kuyaweka masoko yake kwenye ramani ya Afrika,kubainisha  kuwa Tanzania ni ya kwanza  katika orodha ya nchi za Afrika ambapo Africa-PBB-EXPO imepanga kushirikiana nayo.

“Aramex Africa ni mshirika rasmi wa usafirishaji wa Africa-PBB-EXPO na itakwua inatoa mchango mkubwa katika kutoa huduma za ugavi na usafirishaji  kutoka Misri hadi Tanzania,” alisema.

Alisema kupitia Aramex na kwa uratibu wa TanTrade na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Africa-PBB-EXPO  inatoa fursa ya kipekee kwa waoneshaji  walio na kanzidata za kina kusajiliwa mara zinapopokelewa.

Alieleza kwamba kanzidata hizo zinajumuisha hali ilivyo ndani ya soko la Tanzania na thamani yake pamoja na takwimu sahihi ya kuuza na kuagiza, hii inatoa  fursa ya uhakika kwa mikutano ya mkakati ya B2B pamoja na ufanisi unaohusiana pindi zinapofika.

Barakat alitoa wito kwa wafanyabiashara kushiriki katika maonesho hayo ili kuweza  ‘kubaini fursa za ushirikiano katika masoko haya mapya pamoja na mtandao ulio na wateja na wenza wa kibiashara. 

“Kwa kushiriki katika maonesho ya Africa-PPB-EXPO, pamoja na mambo mengine washiriki watajifunza jinsi maudhui ya kina ya sekta yanaweza kuathiri biashara zao,  umoja uliopo miongoni mwa viongozi wa sekta, kupata washirika wapya na kulinganisha kiwango chao katika mitazamo ya ubunifu.

“Kampuni ya EXPO ONE ambayo ni mwandaaji, ni taasisi ya kati ya  usimamizi wa mikutano na maonesho ambayo imejikita katika  kuandaa na kutoa huduma kwa maonesho ya  biashara ya kimataifa  pamoja na 
kuyatangaza mabanda ya Misri katika maonesho ya ndani na ya kimataifa.
 Alisema kwamba maonesho mengine  ya Africa-PPB-EXPO yanatarajiwa kufanyika nchini Senegal na baadaye nchini Angola.



MACHINGA, MFUPA ULIOISHINDIKA HALMASHAURI YA JIJI MWANZA

Ipo kauli isemayo "Mfupa Uliomshinda Fisi" ikiashiria jambo gumu mithiri ya mfupa mgumu ambao umemshinda fisi ambae ni mnyaba bingwa wa kutafuna mifupa ya kila aina.

Ndivyo unaweza kusema ukiitazama picha hizi, kwani suala la kuzagaa ovyo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kwa jina la Machinga jijini Mwanza, ni mfano halisi wa mfupa ulioshindikana kutafunwa na halmashauri ya jiji la Mwanza.

Mara kadhaa juhudi mbalimbali zimekuwa zikifanyika ili kuwaweka wafanyabiashara hao katika mpangilio mzuri kwa ajili ya wao kufanya biashara katika maeneo rasmi yaliyotengwa lakini utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua kwani mafanikio yake yakishindwa kuwa ya kudumu licha ya nguvu kubwa kutumika.

Kabla ya kipindi cha kampeni za Uchaguzi mkuu mwaka jana, halmashauri ya jiji la Mwanza ilifanikiwa kuwaondoa machinga katika maeneo yasiyo rasmi lakini baada ya kampeni kuanza, machinga walirejea mitaani kwa kasi ya ajabu na hakuna aliewagusa tena ambapo hivi sasa kila kona ya jiji la mwanza machinga wamezagaa ovyo.

Baadhi  ya Machinga jijini Mwanza wanaomba sekta hiyo kuboreshwa ili kuondokana na changamoto zinazowakabiri ikiwemo kukosa maeneo maalumu kwa ajili ya wao kufanyia biashara hatua ambayo itasaidia kuondokana na kadhia mbalimbali ikiwemo kukabiliana na mgambo wa jiji wanaokuwa wakiwaondoa katika maeneo yasiyo rasmi kufanyia biashara.
Bonyeza HAPA Kwa Picha Zaidi.

WANACHAMA WAPYA 200 WAJIUNGA CHADEMA

Na Allan Ntana, Tabora

ZAIDI ya  watu 200 wamejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo na
kukabidhiwa kadi za uanachama katika mkutano wa hadhara uliofanyika
katika uwanja wa stendi ya mabasi katika kata ya Tutuo wilayani
Sikonge Mkoani Tabora.

Akikabidhi kadi mpya kwa wanachama hao katika mkutano huo
uliohudhuriwa na viongozi wa Mkoa na Wilaya wa chama hicho wakiwemo
madiwani wote wa CHADEMA wilayani humo, Mwenyekiti wa Mkoa wa CHADEMA
Fransis Msuka alisema zama za kulegalega zimeisha kazi yao ni moja tu
ya kuisimamia serikali ya awamu ya tano kwa vitendo ili haki za
wananchi zipatikane kwa wakati.

Alieleza kuwa mara zote umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu
unaochochea umaskini hivyo akawataka wakazi wa kata hiyo kushikamana
na viongozi wao wa serikali ya kijiji na diwani wao ili kuharakisha
maendeleo ya kata hiyo.

'Nawapongeza sana ndugu zangu wa Tutuo kwa kuchagua viongozi wa
CHADEMA kuongoza serikali yenu ya kijiji na udiwani wa kata hii,
hamkufanya makosa, na dhamira yenu ya kutaka maaendeleo tayari diwani
ameshaanza kuitekeleza kwa vitendo', aliongeza.

Aliwahakikishia kuwa viongozi wao wamebeba kauli mbiu ya hapa kazi tu
na hawako tayari kwa namna yoyote ile kuona wananchi hao
wananyanyasika au kunyimwa haki yao ya msingi na kuongeza kuwa kasi
hiyo hakuna atakayeweza kuizuia na wako tayari kuwatumika usiku na
mchana.
 

Kada Mhamasishaji wa CHADEMA mkoani Tabora Elisha Daudi alisema
watendaji wa serikali iliyoko madarakani hawawezi kuleta mafanikio
makubwa kwa kuwa wametokana na CCM na wengi wao hawana moyo wa dhati
wa kuwatumikia wananchi bali kujinufaisha tu ndio maana hata Rais John
Pombe Magufuli anawatumbua majipu.

Alisema ili kata hiyo ipate maendeleo makubwa hawana budi kuachana na
CCM na kujiunga na CHADEMA na washirika wake wote ili kuunganisha
nguvu ya pamoja na kuanza mikakati mipya ya kuibadilisha Tutuo na
maeneo mengineyo.

Aidha alitahadharisha baadhi ya viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa
wilaya hiyo Hanifa Selengu kwa kuendekeza propaganda mbaya za
kukwamisha juhudi za madiwani wanaotokana na chama hicho za kutetea
maslahi ya wananchi kwa kusimamia ukweli na uwazi hasa kunapokuwa na
maamuzi yanayotia shaka.

'Baadhi ya viongozi wa CCM hawapendi kasi ya madiwani wa upinzani ndio
maana wanakuja juu pale wanapoambia ukweli, kama tukio la juzi la DC
kuamua kumwekwa rumande diwani wetu wa kata hii kisa kuhoji suala la
kutowapa nafasi za kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa
vijana wa Sikonge, viongozi wa namna hiyo hawafai hata katika serikali
ya Rais Magufuli, 'aliongeza.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

WAKATI huo huo wananchi wa kata ya Tutuo wilayani Sikonge Mkoani
Tabora wamelalamikia kitendo serikali kuzuia kurushwa LIVE vikao vya
Bunge la bajeti linaloendelea mjini Dodoma.

Wamesema kutooneshwa bunge hilo ni dhuluma kwa Watanzania kwani
mijadala yote inayoendelea imebeba dhamana ya maendeleo ya wananchi
hivyo wakabainisha kuwa Rais John Pombe Magufuli anapaswa kuingilia
kati suala hilo kama
alivyofanya katika Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es salaam.
 

‘Hili bunge ni la wananchi, tuna haki ya kuona jinsi wabunge wetu
wanavyotetea maslahi yetu ya kimaendeleo, sasa wametuzuia, hii sio
sawa, ni kutunyima haki yetu', alihoji Juma Athuman mkazi wa Tutuo.
 

Akizungumza katika mkutano huo ulioandaliwa na Chama cha Demokrasia na
Maendeleo, Mzee Rashid Mzelu alisema wananchi wengi wanafuatilia sana kila
kinachoendelea bungeni tofauti na viongozi wanavyodhani, na hili linasaidia
kuona mbunge wao anavyowatetea na yule anayesubiri posho tu.

‘Kama hatuoni kinachoendelea bungeni tutajuaje kama mwakilishi wetu yuko
bungeni au kaenda kwenye mambo yake, kuna mambo tumemtuma ayalete bungeni,
sasa hatujui kama kayafikisha au la kwa sababu hata bungeni watoro wapo
pia, sasa akirudi tutampongeza kwa lipi’, alihoji.

Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Tutuo Philipo Arcado Kayumba alisema
wakati wa sherehe za kumwaga Mwenyekiti wa Kwanza wa Chama cha Mapinduzi
Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema kwa sasa dunia inahitaji
nuru katika kila jambo ili wananchi waamue wenyewe, bunge ni nuru ya
wananchi.

Kada Mhamasishaji wa CHADEMA mkoani Tabora Elisha Daudi alisema kitendo cha
vikao vya Bunge kutooneshwa LIVE ni dhuluma kubwa kwa Watanzania, hivyo
akamwomba Rais John Pombe Magufuli kuingilia kati suala hilo kama
alivyofanya katika Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es salaam.

Viongozi wengine wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa Mkoa Fransis Msuka,
Mratibu wa Kanda Christopher Nyamwanji na diwani wa kata ya Tutuo Clemence
Msumeno walibainisha wazi kuwa vikao vya bunge ni muhimu sana  kwa
mustakabli wa maendeleo ya Taifa na ni kipimo sahihi kwa mbunge kama kweli
anatekeleza wajibu wake wa kuisimamia na kuishauri serikali ipasavyo au la.

Friday, May 20, 2016

KENYA A SUITABLE COUNTRY FOR A NEWLY WED

wedding14
By Zainul Mzige of Modewjiblog
For newlyweds who want to explore more unexpected territory, Kenya is a place where one will keep the adventure alive long past the walk down the aisle.
Eric Omenda from Kenya Tourism Board says newly-weds who want to explore more unexpected territory during their first few days as a married couple, Kenya is the best place to be.
In Kenya he said one can have surprising romantic spots stretching from the infrastructure, people, beautiful beaches and so forth.
Kenya has a lot to offer in terms of wildlife, beaches and facilities for everybody and that can be achieved hundred percent per budget you pose.
As a touristic destination Kenya offers a reasonable package to fit your budget, what you need to do is to take your phone and tell what kind of a budget you have and they will ensure that you enjoy the best out of your money.
Jacaranda indian ocean beach resort rooms
Jacaranda Indian Ocean Beach Resort rooms.
From the famous panoramic views of the Mountain Kilimanjaro, Maasai Mara to the soothing waters of coastal beach, Kenya has no shortage of romantic areas to go and things to do.
A good history of romance in Kenya starts with The Duke of Cambridge Prince William who proposed to Catherine Middleton while they were at Lewa wildlife reserve run by Ian Craig on 19 October 2010.
Lewa Wildlife Conservancy also known as Lewa Downs is located in northern Kenya is a wildlife sanctuary incorporating the Ngare Ndare Forest, formed in 1995 and covering over 62,000 acres (250 km2).
The Conservancy is home to a wide variety of wildlife including the rare and endangered black rhino, Grevy's zebra and sitatunga. It also includes the big five (Masai lion, African leopard, bush elephant, rhino and African buffalo).
indianoceanbeachresort1
Jacaranda Indian Ocean Beach Resort.
Lewa holds over 12% of Kenya's eastern black rhinoceros population and the largest single population of Grevy's zebras in the world (approximately 350 individuals).
Lewa Wildlife Conservancy is located south of Isiolo town but north of Mount Kenya.
The haunting beauty of Lewa Wildlife Conservancy on the Northern slopes of Mt Kenya in the area which has an abundance of wildlife including endangered species such as black rhino, white rhino and Grevy’s zebra one would not underestimates cheers and joy derived by the view accompanied by fabulous world class gourmet food.
“Looking at the beaches, various wildlife sceneries which are little known to the world, in fact are virgin, will give honeymooners a chance to explore not only nature but be one with it “says Omenda while justifying how lovely the country is for a newlywed.
lewa-wildlife-conservancy
Rhino in the Lewa Wildlife Conservancy in Kenya
He says the hotels and lodges in the country have packages for the honeymooners even if they have very little to spend.
“You can have little money but you want to spend wisely and in fact you want the best out of it, Kenyans will provide what you need” speaks Omenda adding that only in Kenya were you can get what you want for the amount of money you have.
Camren Nibigira from East Africa Tourism Platform (EATP) Regional Coordinator she insisted that the East Africans have no reason to go abroad for such facilities while they have plenty in their regional.
wedding1
She asked people to travel within the country because of the accessibility and the price. She encourages local tourism by adding that, with 7 -8 million people who can go around as a tourist the East Africa has a good domestic market that nosed it can be vibrant.
“If they are coming to see us they should also explore our attractions instead of going to Dubai for the same purpose” said Nibigira.
She commended KTB by show casing Conservancy brands including the snapshots of one newlywed couple saying the branding would encourage local tourism.
East Africa Tourism Platform (EATP) Regional Coordinator Carmen Nibigira
East Africa Tourism Platform (EATP) Regional Coordinator, Carmen Nibigira.
Wausi Walya, Public Relations and Corporate Communications manager of KTB in an interview with this reporter way back during the Kenyans tourism showcase for journalists around the region, spoke also about the success despite of the fear of insecurity.
He however, admitted that security has been reinforced and there is no need to fear and that Kenya is still a place to visit.
He said they were proud to host two key international meetingswhich will serve as an icon and big hope in promoting Kenya as tourist country.
”If you can translate 800 delegates what it means for a country, then you will be in a position to say that we have managed to overcome the fear syndrome”
African-Wedding-Songs
As Kenya Tourism Board is responsible for marketing Kenya abroad they are trying now to get east Africans utilize facilities available in Kenya for different purposes including a place for newlywed to enjoy themselves and make their journey the most memorable one.
“We have a beautiful country, easy to connect, and in fact a very natural destination of choice, we are very proud” he said Walya.
With colleagues, I visited a couple of hotels which have honeymooners package and found Jacaranda Indian Ocean Beach Resort to be the best in Nairobi for the couple to stay with almost everything the couple would want.
This hotel is situated in a Family-friendly place, Westland with 2 restaurants in the entertainment district, within a 10-minute walk of The Sarit Centre and Westgate Shopping Mall, Arboretum and Nairobi National Museum are also within 2 mi (3 km).
Outdoor pool is available in this hotel. A health club and a poolside bar are one among other amenities available to guests.
What a lovely place to be when it comes to enjoy the luxurious party of being together.
Good luck honeymooners.
jacaranda-indian-ocean
Pool side at Jacaranda Indian Ocean Beach Resort.

TRA YAWAPA ELIMU YA MLIPAKODI WAFANYABIASHARA RAIA WA CHINA WAISHIO NCHINI TANZANIA

1Meneja wa Elimu kwa mlipa kodi kutoka TRA Bi. Diana Masalla akitoa elimu ya mlipa kodi na sheria za kodi kwa wafanyabiashara raia wa China wanaoishi hapa nchini na kufanya biashara katika semina ya mlipa kodi iliyofanyika leo kwenye mgahawa wa Tang Ren Chinese jijini Dar es salaam, ambapo kabla semina hiyo imefunguliwa na Bw. Sun Chengfeng Mwakilishi wa masuala ya Kiuchumi na Kibiashara kutoka serikali ya Watu wa China nchini Tanzania, Semina hiyo inalenga kuwapa wafanyabiashara hao elimu na uelewa wa masuala mbalimbali ya kisheria katika kodi na umuhimu wa kulipa kodi.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE)
2 3Baadhi ya wafanyabiashara raia wa China wanaoishi nchini Tanzania na kufanya biashara wakiwa katika semina ya mlipa kodi iliyofanyika leo kwenye mgahawa wa Tang Ren Chinese jijini Dar es salaam
4Bw. Sun Chengfeng Mwakilishi wa masuala ya Kiuchumi na Kibashara kutoka Serikali ya Watu wa China nchini Tanzania akifafanua jambo kwa waandishi wa habari mara baada ya kufungua semina hiyo iliyofanyika kwenye mgahawa wa Tang Ren Chinese jijini Dar es salaam.

"TCRA YAWANOA WADAU WA MAWASILIANO KANDA YA ZIWA KABLA YA KUZIMA SIMU BANDIA."

Wadau wa Mawasiliano Kanda ya Ziwa, wakiwa katika picha ya pamoja katika Semina juu ya utoaji wa elimu juu ya simu bandia (fake) na halali (orginal) ulioandaliwa na TCRA, kabla ya kusitisha matumizi ya simu bandia mwezi ujao.

Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), imeendelea kuwakumbusha watumiaji wa simu za mkononi kuhakiki simu zao kabla mamlaka hiyo haijazima simu bandia ifikapo Juni 16 mwaka huu.
Soma Zaidi HAPA

Thursday, May 19, 2016

MeTL GROUP YATOA MSAADA WA MIL.30.7 KWA CHUO KIKUU CHA SAYANSI NA TIBA MUHIMBILI

Sylvia Kaaya
Mkuu wa Shule ya Tiba katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS), Prof. Slyvia Kaaya (wa nne kulia) akizungumza machache kabla ya kukabidhiwa rasmi viti 200 na uongozi wa kampuni ya MeTL. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Kampuni ya MeTL, Murtaza Dewji.
Kwa kutambua umuhimu wa elimu, kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) imetoa msaada wa Milioni 30.7 kwa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS) ili kusaidia ununuzi wa viti 200 ambavyo vitatumiwa na wanafunzi wa udaktari wa watoto.
Akizungumza na Modewjiblog kuhusu msaada huo, Mkuu wa Shule ya Tiba katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS), Prof. Slyvia Kaaya, amesema kabla ya kupata msaada huo walikuwa wakitumia chumba kidogo ambacho kilikuwa hakiwatoshi wanafunzi wanaosomea udaktari wa watoto hivyo msaada huo umekuwa muhimu kwao ili kupunguza changamoto ambazo zinawakabili.
“Msaada huu utatusaidia sana na hata sasa hivi tuna matarajio tutakuwa na matokeo mazuri kwa kuongezeka kwa watahiniwa, wanafunzi kuhudhuria vipindi na hata kwa walimu uadilifu wa kufundisha utaongezeka,” alisema Prof. Kaaya.
Aidha Prof. Kaaya alisema pamoja na msaada huo lakini bado wanachangamoto ambazo zinawakabili ambazo zinahitaji kutafutiwa ufumbuzi ikiwa ni pamoja na kufunga viyoyozi na kuweka mitambo ya kuzuia mwangwi ili kuwawezesha wanafunzi kusoma bila kuwa na matatizo.
Nae Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Fatema Dewji-Jaffer alisema kampuni yao imekuwa ikitoa misaada mbalimbali kwa jamii ili kusaidiana na serikali kumaliza baadhi ya changamoto zilizopo na wamejipanga kuendelea kuwa wakitoa misaada kwa wahitaji.
“Tunaamini elimu ni muhimu kwa maendeleo ya baadae tunatoa msaada ili wasome na wawasaidie wengine kupitia elimu wanayoipata chuoni,” alisema Fatema Dewji-Jaffer.
Murtaza Dewji
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Kampuni ya MeTL, Murtaza Dewji (kushoto) akitoa salamu za kampuni ya MeTL kabla ya kukabidhi viti 200 kwa uongozi wa MUHAS. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL, Fatema Dewji-Jaffer.
Fatema Dewji - Jaffer at MUHAS
Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL), Fatema Dewji -Jaffer (wa tatu kulia) akimkabidhi moja kati ya viti 200 Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS), Prof. Aporinal Kamuhangwa (wa pili kushoto) vilivyotolewa na kampuni ya MeTL Group. Kushoto ni Mkuu wa Shule ya Tiba katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS), Prof. Slyvia Kaaya. Wengine wanaoshuhudia tukio hilo kulia ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa kampuni ya MeTL Group, Murtaza Dewji na Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Barbara Gonzalez (kulia). Mstari wa nyumba ni watumishi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba (MUHAS).
MeTL and MUHAS
Picha ya pamoja baada ya makabidhiano yaliyofanyika katika jengo la Watoto lililopo Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Murtaza Dewji MeTL
Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS), Prof. Aporinal Kamuhangwa akitoa shukrani kwa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa kampuni ya MeTL Group, Murtaza Dewji baada ya kukabidhiwa viti hivyo.
Barbara Gonzalez
Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Barbara Gonzalez (kulia) akizungumza neno baada ya hafla fupi ya kukabidhi viti hivyo.
Agustine Massawe
Uongozi wa MeTL na MUHAS wakiwa wamekaa kwenye viti hivyo.
Karim Manji
Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL), Fatema Dewji -Jaffer (katikati) akifurahi jambo na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa kampuni ya MeTL Group, Murtaza Dewji. Kushoto ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS), Karim Manji.
Donated to MUHAS by MeTL
Viti 200 vya MUHAS vilivyotolewa na Kampuni MeTL.
Chairs Donate by MeTL MUHAS

DK. MENGI ATOA DARASA KWA WASHIRIKI WA CHUO CHA ULINZI CHA TAIFA

Dk. Reginald Mengi saini
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi akisaini kitabu cha wageni alipowasili kwenye Chuo cha Ulinzi cha Taifa kilichopo Kunduchi, jijini Dar es Salaam Mei 16, 2016 kwa ajili ya kutoa muhadhara kwa washiriki wa kozi ya mbinu za kiusalama katika chuo hicho.(Picha zote na Modewjiblog)
IMELEZWA jukumu la ulinzi na usalama kwa dunia ya sasa halimo kwenye mikono ya polisi na wanajeshi pekee bali ni la kila mtu katika nafasi aliyopo kama amani na demokrasia inatakiwa kuendelea kuwapo.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Meja Jenerali Yacoub Mohamed wakati akizungumza na Modewjiblog ofisini kwake baada ya mhadhahara ulioshirikisha wataalamu wa masuala ya habari kutoka sekta binafsi na umma ambao wanachukua kozi ya mbinu za usalama chuoni hapo.
“Zamani mambo ya usalama yalikuwa ya wanajeshi na Polisi lakini kwasasa mambo ni tofauti, kila mmoja anatakiwa kuhakikisha anakuwa mlinzi ili uwepo usalama wa kutosha kwahiyo tunaamini washiriki wakirudi vituoni kwao watazingatia usalama.
“Wote wanaokuja hapa wanakuwa ni viongozi au viongozi watarajiwa na kama sasa tuna wanafunzi 38, 12 sio Watanzania ni kutoka Kenya, Rwanda, Burundi, Malawi, Namibia, Botswana, Afrika Kusini, Zambia, Nigeria na China,” aliongeza Meja Jenerali Mohamed.
Wataalamu walioendesha mihadhara hiyo ni Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi ambaye amepata nafasi ya kutoa elimu kuhusu habari kwa sekta binafsi na Mkuu wa Shirika la Utangazaji nchini (TBC) na mwanazuoni Dk. Ayoub Rioba ambaye aliwasilisha sekta ya umma.
Akielezea ujio wa Dk. Mengi chuoni hapo, alisema wamekuwa na taratibu wa kukaribisha watu mbalimbali ambao wanawaona wana uwezo wa kuelezea uzoefu wao katika mambo mbalimbali ambayo yanaweza kuwa na faida kwa washirika.
Alisema chuo chao kimekuwa hakina walimu wa kudumu hivyo pamoja na kutumia watu mbalimbali kama walivyofanya kwa Dk. Mengi pia wamekuwa wakiwatumia walimu wa vyuo vikuu ili kutoa elimu ambayo itawasaidia washiriki katika masomo yao ambayo wanayapata chuoni hapo.
“Chuo chetu hakina walimu wa moja kwa moja kwahiyo huwa tunatumia walimu kutoka vyuo vikuu vya hapa nchini lakini pia huwa tunakaribisha watu maarufu wanakuja ku’share’ uwezo wao kwa washiriki ambao wanakuwa wapo masomoni.
“Dk. Mengi ameshafika hapa chuoni mara tatu na sio mtu wa kwanza kuja alishakuja Pius Msekwa, Mawaziri, Katibu Mkuu kiongozi na hata jana tulikuwa na (Dkt. Ayoub) Rioba,” alisema Meja Jenerali Mohamed.
Dk Mengi na Meja Jenerali Yacoub Mohamed
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi akisalimiana Mkuu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Meja Jenerali Yacoub Mohamed (kulia) mara baada ya kuwasili chuoni hapo kutoa muhadhara kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuhakikisha usalama wa taifa kwa washiriki wa kozi ya mbinu za kiusalama Mei 16, 2016 jijini Dar es Salaam.
Alisema chuo hicho hupokea washiriki ambao ni viongozi katika ofisi wanazofanyia kazi na hupokea washiriki kutoka nchi mbalimbali ambapo hupatiwa elimu kuhusu usalama ili wanapotoka chuoni hapo wakafanye kazi kwa umakini ili wasiweze kuwa sababu ya kupoteza usalama katika maeneo yanayowazunguka.
Katika mada yake iliyozungumza kuhusu wajibu wa vyombo vya habari binafsi katika usalama wa Taifa, Dk. Mengi alisema vyombo visipokuwa makini vikawajibika kitaaluma vinaweza kusababisha migogoro itakayohatarisha usalama wa taifa.
Akielezea uzoefu wake kama mmiliki wa vyombo vya habari binafsi alisema usalama ni jambo la muhimu kwa kila mtu bila kujali ana nafasi gani katika nchi hivyo ni wajibu wa kila mtu kushiriki katika kuimarisha usalama.
Alisema vyombo vya habari wanahakikisha habari zinazotolewa zinakuwa hazina madhara ambayo yanaweza kusababisha upotevu wa amani lakini kusimamia misingi na maadili ya uandishi wa habari.
Brigadia Jenerali Yohana Mabongo
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi (kushoto) akisalimiana na Katibu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Brigadia Jenerali Yohano Mabongo mara baada ya kuwasili chuoni hapo.
“Kama kuna utulivu, mshikamano na usalama wa taifa kuna faida kwa taifa na hilo linaweza kusaidia kukuza kwa uchumi wa nchi ambao pia utakuwa na faida kwa kila mwananchi,
“Vyombo vya habari vinatakiwa kufuata maadili ya kazi yake kuupasha umma habari na kutoa elimu bila kuathiri hali ya amani na utulivu kwa sababu tunaelewa kuwa pamoja na kutoa habari lakini pia ni wajibu wetu kuhakikisha kuna usalama nchini,” alisema Dk. Mengi.
Yacoub Mohamed NDC
Mkuu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Meja Jenerali Yacoub Mohamed akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi (hayupo pichani) kutoa muhadhara kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuhakikisha usalama wa taifa kwa washiriki wa kozi ya mbinu za kiusalama chuoni hapo.
Dk. Reginald Mengi 1
Mwenyekiti Mtendaji wa Makapuni ya IPP Ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi akitoa muhadhara kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuhakikisha usalama wa taifa kwa washiriki wa kozi ya mbinu za kiusalama (hawapo pichani) katika Chuo cha Ulinzi cha Taifa kilichopo Kunduchi, jijini Dar es Salaam Mei 16, 2016.
Reginald Mengi NDC
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi akitoa muhadhara kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuhakikisha usalama wa taifa kwa washiriki wa kozi ya mbinu za kiusalama katika Chuo cha Ulinzi cha Taifa kilichopo Kunduchi, jijini Dar es Salaam.
Meja Jenerali Yacoub Mohamed
Mkuu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Meja Jenerali Yacoub Mohamed akitoa historia fupi ya chuo hicho kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).
Dk. Reginald Mengi akiaga
Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP Ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi akiagana na Mkuu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Meja Jenerali Yacoub Mohamed (kulia) mara baada ya kutoa muhadhara kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuhakikisha usalama wa taifa kwa washiriki wa kozi ya mbinu za kiusalama (hawapo pichani) katika chuo hicho kilichopo Kunduchi, jijini Dar es Salaam.
National Defence College
Muonekano wa mbele wa Jengo la Chuo cha Ulinzi cha Taifa kilichopo Kunduchi, jijini Dar es Salaam.

Wednesday, May 18, 2016

RC PAUL MAKONDA ASEMA WANAWAKE NDIO CHANZO CHA UFISADI NCHINI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikagua machinjio ya Vingunguti baada ya kuzungumza na wananchi wa Kata ya Mnyamani Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto.
Wananchi wa Kata ya Mnyamani Vingunguti wakiwa kwenye mkutano huo wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (hayupo pichani)
Makonda (kushoto), akisalimiana na wananchi na viongozi wakati akiwasili kwenye mkutano huo.
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto (wa pili kulia), akizungumza katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuzungumza na wananchi. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Mnyamani, Shukuru Dege, RC. Makonda na Meneja wa Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB), Tawi la Ukonga, Das Ndazi.
Meneja wa Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB), Tawi la Ukonga, Das Ndazi (kushoto), akizungumza katika mkutano huo kuhusu suala zima la utoaji wa mikopo.
RC Makonda akizungumza na wananchi wa Vingunguti.
Wananchi wakimsikiliza RC Makonda.
Safari ya kwenda kukagua machinjia ya Vingunguti.
Sehemu ya machinjio ya Vingunguti.
RC Makonda akipatiwa maelezo kuhusu mitambo ya kuchinjia iliyopo kwenye machinjio hiyo.

Na Dotto Mwaibale

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema wanawake wamekuwa ni chanzo cha ufisadi nchini kutokana na kupokea zawadi zitokanazo na fedha za kifisadi.

Makonda aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnyamani Vingunguti Dar es Salaam jana katika mkutano wa kujadili namna ya kupata mikopo mbalimbali kutoka Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB).

" Ninyi wakina mama mmekuwa chanzo cha ufisadi kwa vile mmekuwa mkipokea fedha na zawadi mbalimbali kutoka kwa watoto wenu lakini mmekuwa hamuwahoji wanako zitoa fedha hizo kwani zingine zinakuwa za kifisadi" aliseama Makonda.

Makonda aliwaambia wanawake hao kuwa hata katika suala zima la usafi linaanzia na malezi ya usafi ya wakina mama kwa watoto wao tangu wakiwa wadogo jambo ambalo lingesaidia kipindi hiki ambapo kunachangamoto kubwa ya kusafisha miji yetu.

Katika hatua nyingine Makonda alitoa pongezi kwa Kaimu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto kwa kuwa jirani na wananchi wa kata yake kwa kufanya maendeleo bila ya kujali itikadi za vyama hasa katika kujipatia mikopo kutoka katika Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB).

"Nimefurahishwa na diwani wenu Kumbilamoto kwa kushirikiana nanyi ili  kujiletea maendeleo ni jambo zuri na wakati huu ni wa kukutana kubuni na kuangalia jambo gani litawakwamua kiuchumi badala ya kuwaza maandamano yasiyo na tija" alisema Makonda.