Pages

KAPIPI TV

Tuesday, September 1, 2015

MULTICHOICE AFRICA CONTENT SHOWCASE...ONLY THE BEST

bty
Modewjiblog Operations Manager, Zainul Mzige taking a 'selfie' with the Nigerian Artist Mr. Flavour at Sir Seerwoosagur Ramgoolan International Airport upon our arrival in Mauritius.
IMG_5901
Head of delegation from Tanzania, Public Relations Manager at MultiChoice Tanzania Ltd, Barbara Kambogi pose for a photo with Tanzanian Journalists who have been invited to Mauritius to experience the biggest week in Africa's video entertainment, hosted by MultiChoice Africa.
IMG_5906
Invited guests from Botswana poses for a group photo.
IMG_5912
Comedian from Nigeria, Basket Mouth (left) pose for a photo with award winning singer and songwriter Mr.Flavour
IMG_5913  
The Guardian Newspaper Senior Reporter Sylivester Domasa with Nigerian Comedian Basket-Mouth (right) and award wining singer and song writer Mr.Flavour
dav
Invited guests mingle at the VIP Lounge upon their arrival.
Dear readers
We are in Mauritius to experience the biggest week in Africa’s video entertainment, hosted by MultiChoice Africa.
We have arrived at Sir Seerwoosagur Ramgoolan International Airport just some hours ago and the fun has already started.
For the next five days, we will be treated to ‘ONLY THE BEST’ in video entertainment on the DStv and GOtv.
We are here, and the only thing we have been encouraged, is to open our mind to experience television like we had never before and also to grab the opportunity to interact with various exciting channels that will engage with us and give an exclusive, in-depth and VIP experience of their content.
I trust that throughout this event, I will have plenty of material to share with you.
I look forward to give you an amazing Africa-inspired content live-in action.
While am here definitely I will touch and rubbed shoulders with the stars of Hollywood, Nollywood, Bollywood and so much more. I am truly looking forward to sharing with you this exciting journey of television content discovery.
Be part of the conversation on social media with the hashtag: #OnlyTheBest. And please follow us on social media via Twitter: @MCAShowcase; Instagram: @MultiChoice_Africa and Facebook Group: #OnlyTheBest

MO DEWJI FOUNDATION YAKABIDHI MATUNDU NANE YA CHOO BORA KWENYE SHULE YA MSINGI KIBAONI MKOANI SINGIDA

DSC01579
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kibaoni mjini Singida, Sundi Samike, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane chenye thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni zilizotolewa na MO Dewji Foundation (shilingi 14 milioni) na Doris Mollel Foundation shilingi 2.3 milioni).
DSC01583
Mwakilishi wa Mo Dewji Foundation mkoani Singida, Duda Mughenyi, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane shule ya msingi Kibaoni mjini Singida, chenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 16. Duda amewataka wakazi wa manispaa ya Singida, kujenga utamaduni wa kuchangia kwa hali na mali, uboreshaji wa mazingira ya shule, ili kuvutia wanafunzi kupenda shule.
DSC01592
Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation ya jijini Dar-es-sa-laam, Doris Mollel, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane ya shule ya msingi Kibaoni mjini Singida chenye thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni, kati ya fedha hizo, Mo Dewji Foundation imetoa shilingi 14 milioni na Doris Foundation shilingi 2.3 milioni.
DSC01596
Mwakilishi wa Mo Dewji Foundation mkoani Singida, Duda Mughenyi, (wa tatu kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation, Doris Mollel (wa pili kulia) wakielekea kuzindua choo bora kipya cha shule ya msingi Kibaoni.
DSC01600
Mwakilishi wa MO Dewji mkoani Singida, Duda Mughenyi, (wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundatin, Doris Mollel (wa tatu kushoto) kwa pamoja wakizindua choo bora kipya cha shule ya msingi Kibaoni chenye thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni. MO Dweji Foundation imechangia shilingi 14 milioni na Doris Mollel, shilingi 2.3 milioni.
DSC01603
Jengo la choo bora chenye matundu nane kilichojengwa kwa thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni kwa ushirikiano wa MO Dewji Foundation na Doris Mollel Foundation kitakachotumiwa na wanafunzi 842 wa shule ya msingi Kibaoni mjini Singida. (Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
WAZAZI/WALEZI wakazi wa halmashauri ya manispaa ya Singida, wamehimizwa kujenga utamaduni wa kuchangia kwa hali na mali uboreshaji wa mazingira ya shule, kama njia moja wapo ya kuwavutia wanafunzi kuhudhuria shule.
Wito huo umetolewa na Mwakilishi wa MO Dewji Foundation mkoa wa Singida, Duda Mughenyi, wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane chenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 16 kwa shule ya msingi Kibaoni mjini hapa, yenye jumla ya wanafunzi 842, kati yao wavulana ni 377 na wasichana ni 465.
Alisema uzoefu unaonyesha kwamba mazingira ya shule yakiwa safi, vifaa vya kufundishia na kujifunzia viwepo vya kutosha , maji safi na salama yawepo na vyoo bora vinavyokidhi mahitaji, hatua hiyo huwajengea mazingira mazuri wanafunzi , kujiendeleza kielimu.
Akifafanua, alisema shule ya msingi ya Kibaoni ilikaribia kufungwa kutokana na kukosa vyoo kwa ajili ya wanafunzi na wanafunzi,lakini Dewji Foundation na Doris Mollel Foundation, ilinusuru shule hiyo isifungwe baada ya MO Dewji Foundation kutoa shilingi 14 milioni na Doris Mollel kutoa shilingi 2,300,000.
Duda alitumia nafasi hiyo kuwataka wanafunzi wakitunze na kudumisha usafi wa choo hicho ili kiweze kutumika kwa muda mrefu.
Kwa upande wake Doris Mollel (Miss Singida 2014), alisema Foundation yake itaendelea kufadhili sekta ya elimu mkoani Singida kama njia ya kuwashukuru wakazi mkoani hapa kwa kumsapoti na kufanikisha kushinda nafasi ya Miss Singida mwaka jana.
Awali Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kindai tarafa ya Mungumaji iliyoanzishwa mwaka 1975,Sundi Samike,alishukuru uongozi wa Mo Dweji Foundation na Doris Mollel Foundation, kwa kuifadhili shule hiyo ujenzi wa choo na kuinusuru kufungiwa.
“Nitumie nafasi hii pia kulipongeza shirika la WaterAid Tanzania kwa uamuzi wake wa kufadhili ujenzi wa vyoo bora ambao ujenzi wake tayari umeishaanza.Aidha,nitoe wito kwa wazazi,wasaidie kwa hali na mali kuharakisha ujenzi huu”,alisema.

UN YAFANYA USAFI SOKO LA TEMEKE STEREO KUADHIMISHA MIAKA 70

IMG_5298
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (katikati) kabla ya kuanza zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Na Mwandishi wetu
KATIKA kuadhimisho miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa (UN) wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Kimataifa walijumuika na wakazi wa Temeke katika kufanya usafi kwenye soko la Temeke Stereo.

Shughuli hiyo wameifanya baada ya wiki iliyopita kufanya shughuli za upandaji miti katika miteremko ya mlima Kilimanjaro. Wakiwa katika miteremko ya milima Kilimanjaro walipanda miti 2,000.

Shughuli hizo za kufanya usafi ambazo ziliongozwa na Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez, zilifanyika katika juhudi za kuleta uhalisia wa utunzaji wa mazingira kama umoja huo unavyofanya.

Akizungumza katika shughuli hizo Mkuu wa wilaya ya Temeke, Sophia Mjema, ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa aliupongeza Umoja wa Mataifa kwa kusherehekea miaka 70.

“Nachukua nafasi hii kupongeza watu wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kufanya shughuli mbalimbali kuelekea maadhimisho ya miaka 70 kwa kupanda miti 2,070 kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro na hili tendo la leo la usafi kama mwendelezo wa kaulimbiu inayohimiza utunzaji wa mazingira ya“ Sayari moja, watu bilioni 7: Ulinzi wa mazingira ni wajibu wetu,” alisema.

Akisisitiza umuhimu wa kutunza mazingira na usafi, Mkuu huyo wa wilaya alisema wajibu wa kutunza mazingira ni wa kila mtu.
IMG_5365
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa ikiwemo kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii kwa wananchi na wafanyabiashara wa soko la Temeke Stereo mwishoni mwa juma. Kushoto ni Kaimu Mwakilishi Mkazi wa FAO nchini, Patric Otto. 
Wa tatu kulia ni mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Temeke, Sophia Mjema, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (wa pili kulia) na Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira manispaa ya Temeke, Ally Hatibu.

“Kutunza mazingira si wajibu wa mtu mmoja. Ni wajibu wako kama ilivyo kwa jirani yako. Kunapokuwepo na watu wengi mara nyingi hutokea watu ambao hawajali wala kuona umuhimu wa kutunza mazingira, umuhimu wa kufanya haya.

“ Nawaomba wote mlioshiriki katika shughuli hii leo kuwa watu wa kuchunga mazingira katika maeneo yenu mnayofanyia kazi na majumbani kwenu.Hakikisheni mnafundishana na majirani zako katika suala hili na kuhakikisha kwamba kila mmoja anayekuzunguka anawajibika katika kutunza mazingira.”

Akisisitiza menejimenti ya mazingira, Rodriguez, alizungumza kwamba mabadiliko ya tabia nchi na mazingira endelevu ndio ajenda kuu katika malengo endelevu ya maendeleo (SDG’s).

“Mwaka huu jumuiya ya kimataifa itakubaliana kuhusu SDGs na kukamilishwa kwa malengo ya milenia (MDGs). Malengo ya milenia yamewezesha kupatikana kwa mabadiliko makubwa katika kukabiliana na umaskini, afya bora na kiwango kikubwa cha watu wanaojiunga na shule. Mataifa ya Umoja wa Mataifa kwa kupendezwa na mafanikio ya MDGs sasa wanataka kukubaliana kuhusu SDGs.

“ SDG itakuwa na vipengele 17 kikiwamo cha mabadiliko ya tabia nchi. Umoja wa Mataifa umechagua suala la mabadiliko ya tabia nchi kuwa ndio kipaumbele cha mwanzo kwani imebaini kwamba ni tishio kwa maendeleo endelevu. Hii inatokana na ukweli kuwa mabadiliko ya tabia nchi ni ya kweli na ni vyema kila mtu kuwajibika ili kuhakikisha mazingira yetu yanaendelea kuwa mazuri-tukianzia na mazingira yetu yanayotuzunguka” alisisitiza.

Rodriguez alizitaka jamii mbalimbali kutoa kiipaumbele katika kusafisha mazingira na usafi binafsi hasa kipindi hiki ambapo kumezuka ugonjwa wa Kipindupindu kwa mikoa ya Dar es salaam na Morogoro.

“Usafi wa soko hili ni muhimu kwa ajili ya afya yako na uhai mrefu. Afya njema inatuwezesha kuendelea kufanya shughuli zetu mbalimbali za kuchangia ukuaji wa uchumi.

Hebu angalia pembeni mwako imetuchukua saa chache kusafisha soko la Temeke na je hamuoni tofauti? Nawaomba wakazi wa Temeke na wafanyakazi wa soko hili kufanya shughuli hizi kila siku kwani maisha yao, afya yao na uchumi unategemea soko hili.”

Pia aliwaalika wananchi wote katika sherehe za miaka 70 za Umoja wa Mataifa zitakazofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja Oktoba 13 ili kushiriki kikamilifu katika kuadhimisha siku hiyo ya Umoja wa Mataifa.

Pia alihimiza serikali kuendelea kuelimisha wananchi juu ya utunzaji wa mazingira na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
IMG_5475
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Temeke, Sophia Mjema akitoa nasaha zake kwa wananchi na wafanyabiashara wa soko la Temeke Stereo, ambapo aliwataka kuzingatia usafi wa maeneo yao ya biashara pamoja na majumbani ili kuepeukana na mlipuko wa Kipundupindu.

Katika hafla hiyo ya kusafisha soko la Temeke, Umoja wa Mataifa na serikali ya Tanzania kwa pamoja walitoa vifaa vya kufanyia usafi vyenye thamani ya shilingi milioni 10. Vifaa hivyo vilikabidhiwa kwa menejimenti ya soko la Temeke.

Watu wengine walioshiriki katika shughuli hiyo ni pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy; mkuu wa wilaya ya Temeke Mheshimiwa Sophia Mjema, akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na maofisa wengine wa serikali na wakazi wa Temeke.

Balozi Mushy katika risala yake ya kumkaribisha mgeni rasmi kufanya usafi aliitaka jamii kutambua kwamba usafi ni jukumu la kila mmoja wetu kwani bila usafi madhara yake ni makubwa ikiwamo ya kutunzwa kwa mazingira.

Alilitaka jiji la Dare s salaam ambalo linalinganishwa na majiji mengine duniani kama Nairobi, Kenya; Pretoria Afrika Kusini, Washinton DC na Paris kujifunza kuwa wasafi kwani hata mlipuko wa sasa wa Kipindupindu ni dalili tosha ya kukosekana kwa usafi.

Aidha alisema kwamba suala la usafi si lazima kwenda kujifunza nje kwani ipo miji na mikoa misafi ambayo inaweza kuulizwa wamefanikishaje jambo hilo. Aliitaja miji hiyo ni Moshi, Iringa na Mwanza.

Alisema katika kuadhimisha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa, wameamua kufanya usafi wa mazingira katika soko la Temeke kuonesha kwamba inawezekana kufanya usafi kwa kuwajibika kwa lengo la kufanya mazingira yawe masafi na ya uhakika.

Kwa kutekeleza usafi kwa maana nyingine kutasaidia kuondoa gharama zinazoambatana na uchafu wa mazingira.

Alitaka kila mmoja katika soko hilo kuanzia wakulima hadi wachuuzi kuwajibika kwa usafi ili mazingira yawe salama.
IMG_5301
Pichani juu na chini ni wafanyabiashara wa Soko la Temeke Stereo, wananchi na wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wa Wziara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia kwa umakini hotuba ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke (hayupo pichani).
IMG_5471
IMG_5299
IMG_5285
IMG_5554
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati) akikambidhi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (kushoto) vifaa vya kufanyia usafi katika Soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. Anayeshuhudia tukio hilo kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy.
IMG_5558
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akivaa 'gloves' tayari kushiriki zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
IMG_5569
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy wakifanya usafi katika maeneo ya wafanyabiashara katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5575
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akibeba taka katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5604
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema wakishiriki zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya kusheherekea maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
IMG_5649
Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakijumuika na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez wakiendelea na zoezi la usafi.
IMG_5643
IMG_5633
IMG_5787
Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Titus Osundina (kulia), Beatrice Mkiramweni pamoja na Jacqueline Namfua wakifanya usafi kwenye maeneo ya soko la Temeke Stereo.
IMG_5789
Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Titus Osundina akishiriki zoezi la kuzoa taka katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5801
IMG_5678
Umoja ni Nguvu: Wafanyabiashara wa soko la Temeke Stereo, wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje wakishirikiana kwa pamoja kufanya usafi katika soko hilo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
IMG_5695
Petra Karamagi na Nasser Ngenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa wakishikishiriki zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5704
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano alipomulikwa na kamera ya Modewjiblog
IMG_5683
IMG_5716
Zoezi likiendelea.
IMG_5721
Zoe Glorious katika ubora wake.
IMG_5723
#HapaKaziTu ......Usia Nkhoma Ledama akiwajibika katika zoezi la usafi soko la Temeke Stereo.
IMG_5726
Wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wafanyabiashara wakishirikiana katika zoezi hilo.
IMG_5741
IMG_5756
IMG_5290
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu (kulia) akiteta jambo na na baadhi ya maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walioshiriki kwenye zoezi la kufanya usafi wa mazingira katika soko la Temeke Stereo.

Sunday, August 30, 2015

WAHAMIAJI: NCHI ZA ULAYA ZAKOSOLEWA.


Waziri wa mashauri ya kigeni nchini Ufaransa Laurent Fabius ameelezea hisia za baadhi ya nchi za ulaya dhidi ya suala la uhamiji kuwa sawa na sakata.
Amezilaumu nchi za ulaya hasusan zilizo mashariki mwa ulaya kwa kukataa kuwaruhusu wahamiaji.
Bwana Fabius aliiilaumu Hungary kwq kujenga ua ulio na lengo la kuzuia watu wanaowasili wakipitia nchini Serbia akisema kuwa hatua hiyo haiendi sawa na maadili ya ulaya.

Ufaransa imejiunga na Uingezea pamoja na na Ujerumani katika kuitisha mkutano wa dharura na mawaziri wa nchi za ulaya kutafuta njia za kukabiliana idadi ya wahamiaji inayozidi kuongezeka.
Chanzo:-BBC Swahili

CHAMA CHA ACT-WAZALENDO CHAZINDUA KAMPENI ZAKE VIWANJA VYA MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM LEO

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira (kushoto), akihutubia katika uzinduzi wa kampeni ya chama hizo uliofanyika viwanja vya Zakhem Mbagala jijini Dar es Salaam leo.
 Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto akihutubia katika uzinduzi huo.
 Mshauri wa Chama cha ACT-Wazalendo, Profesa Kitila Mkumbo akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto (kushoto), akiteta jambo na  Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira.
 Viongozi mbalimbali wa chama hicho wakiimba wimbo wa taifa.
 Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto, akiwatambulisha wagombea ubunge wa majimbo yote ya Dar es Salaam.
  Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto, akigawa ilani ya chama hicho kwa mgombea urais na mwenza wake.
 Mgombea Mwenza, Hamad Mussa Yusuph akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Mwana muziki Bwana misosi, akitoa burudani katika uzinduzi wa kampeni wa Chama cha ACT-Wazalendo uliofanyika viwanja vya Zakhem Mbagala Dar es Salaam leo.
Umati wa Wananchi ukiwa katika uzinduzi wa kampeni wa Chama cha ACT-Wazalendo uliofanyika viwanja vya Zakhem Magala Dar es Salaam leo.