Pages

KAPIPI TV

Thursday, July 23, 2015

UN YAKANUSHA UZUSHI WA JAMII FORUM NA INDIAN OCEAN NEWSLETTER

IMG_7871
Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mipango ya maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez.
UMOJA wa Mataifa umetaka vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa kuhakikisha vinatoa taarifa zao kwa usahihi kuhusu maandalizi ya uchaguzi na uchaguzi wenyewe.
Kauli hiyo imetolewa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa Dar es salaam, kufuatia taarifa iliyochapishwa na jarida moja kwamba UN inataka kujitoa katika kusaidia mandalizi ya uchaguzi nchini Tanzania.
Aidha alisema kwamba si kweli kuwa Umoja wa Mataifa haujaridhishwa na mwenendo wa maandalizi ya uchaguzi nchini Tanzania na kwamba Umoja huo utaendelea kushirikiana na serikali na vyombo vingine vya uchaguzi kuhakikisha uchaguzi unakwenda vyema.
Indian Ocean Newsletter ya Julai 10 mwaka huu ilichapisha habari iliyoandikwa na kichwa cha habari “State is facing electoral commissions negligence” na kusema kwamba Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mipango ya maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez, haridhishwi na mwenendo wa maandalizi ya uchaguzi na uchaguzi wenyewe na kutishia kuondoa msaada wa mamilioni unaoratibiwa na UNDP kutoka kwa wahisani mbalimbali.
Aidha Julai 15, 2015, mtandao wa Jamii Forum ilitafsiri habari hiyo kwa Kiswahili na kuitawanya kwa wasomaji wake.
Ukweli ulivyo
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini hajawahi kukutana wala kuzungumza na watu wa Indian Ocean Newsletter .
Aidha taarifa zilizotolewa na kijarida hicho na tafsiri yake iliyowekwa mtandao wa kijamii wa Jamii Forums hazikujengwa katika ukweli.
Pia Umoja wa Mataifa utaendelea kufanyakazi na mamlaka za Tanzania na wananchi wake na kuwa Uhusiano kati ya Umoja wa Mataifa na mamlaka za uchaguzi nchini Tanzania na Jumuiya ya kimataifa inayofadhili mradi wa DEP unawasilisha mahusiano muhimu miongoni mwa wadau mbalimbali wanaotaka kuwapo na uchaguzi huru na wa amani.
Alisema katika makubaliano kuna kamati ya mradi inayojumuisha wadau wote na ina wajibu kuongoza na kutoa mwongozo wa utekelezaji mradi huo kimkakati.
Maamuzi ya mradi huo hufanywa na kamati hiyo na kamati ya ufundi ya mradi iliyopo Bara na Zanzibar.
Kutokana na ukweli huo Umoja wa Mataifa unavitaka vyombo vya habari vya kitaifa na Kimataifa kuhakikisha kwamba inatoa taarifa za ukweli na za usahihi kipindi hiki cha maandalizi na uchaguzi wenyewe.
[caption id="attachment_141105" align="aligncenter" width="595"]Biometric Voter Registration (BVR)   Machines operator, Kheri Mkali attends Rebeca Kimu at Bunju A in Dar es Salaam yesterday during the trial registration. PHOTO|VENANCE NESTORY Biometric Voter Registration (BVR) Machines operator, Kheri Mkali attends Rebeca Kimu at Bunju A in Dar es Salaam yesterday during the trial registration. (LIBRARY PHOTO|VENANCE NESTORY).[/caption]
Background
The Democratic Empowerment Project is a three year project launched on the 12th of March 2013 and is directly executed by UNDP with UN Women and UNESCO through a donor basket fund. It follows two previous electoral support projects in Tanzania: the Electoral Assistance Project of 2005 and the Election Support Project of 2010. The USD 25m project has four main components, namely, a) supporting legal and institutional reforms; b) support improvement of Electoral Management body’s capacities(NEC and ZEC); c) promote inclusive participation in political and electoral processes, and d) support national peace infrastructures. More specifically, the project has been supporting both NEC and ZEC to improve their institutional capacity both in the context of the conduct of the voter registration process (but not the provision of the BVR kits which is the government’s responsibility) and the preparations for the 2015 general elections. DEP’s support has included technical and advisory services, staff training, voter education and stakeholder engagement. Such stakeholders include the Office of the Registrar of Political Parties, political parties, media, civil society and groups representing women, youth and people with disabilities. So far DEP has supported and implemented most of these activities either directly or via cooperation agreements with the electoral management bodies who execute specific activities directly in line with their mandate.
Issued by: The Office of the UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative – Mr. Alvaro Rodriguez
For more information, please contactHoyce Temu-UN Communications Specialist at hoyce.temu@one.un.org or Aine Mushi, UN Coordination Specialist at aine.mushi@one.un.org
Below is the Indian Newsletter article in French

UZINDUZI WA KAMPENI YA AWAMU YA PILI YA WAZAZI NIPENDENI WAFANYIKA DAR ES SALAAM

 Mkurugenzi wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ali Mohamed Ali (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa tamko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Donan Mmbando katika uzinduzi wa kampeni ya awamu ya pili ya wazazi nipendeni uliofanyika Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Georgina Msemo na Mshauri wa Kiufundi wa Malaria kutoka  Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID)
 Ofisa Uzazi Salama,  Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Heavengton Mshiu (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mshauri wa Masuala ya Afya ya Uzazi wa Taasisi ya Center for Comminication Programs Johnns HopKins University, Dk,.Rosemarie Madinda (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo. Taasisi hiyo ndiyo inayoendesha kampeni hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Georgina Msemo (kulia), akizungumza kwenye uzinduzi huo.
 Mwongozaji wa uzinduzi huo akiendelea na kazi.

Wanahabari wakiwa kwenye shughuli hiyo.
  Ofisa Uzazi Salama,  Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Heavengton Mshiu (kushoto), akimpongeza  Mkurugenzi wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ali Mohamed Ali, baada ya kutoa tamko la Wizara hiyo katika uzinduzi huo.
Mwanamuziki Nyoshi Al-Saadat wa Bendi ya Muziki wa Dansi ya FM Academia "Wana wa Ngwasuma" itakayotoa burudani katika maonyesho mbalimbali yatakayokwenda sanjari na uzinduzi huo yatakayofanyika kuanzia kesho viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam kuanzia kesho, akizungumza katika uzinduzi huo utakaopambwa na burudani za kumwaga.

Na Dotto Mwaibale

SERIKALI imesema imepiga hatua katika kupunguza vifo vya watoto waliochini ya miaka mitano toka 157 mwaka 1990 hadi kufikia 54 kwa mwaka 2013.

Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ali Mohamed Ali wakati akitoa tamko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Donan Mmbando katika uzinduzi wa kampeni ya awamu ya pili ya wazazi nipendeni uliofanyika Dar es Salaam leo

Alisema kati yua watoto hai 1,000 wanaozaliwa na kufikia lengo la Melenia (MDG) 4 waliojiwekea kufikia mwisho wa mwaka huu Disemba 2015.

"Pamoja na mafanikio hayo bado hari si shwari kwa upande wa vifo vinavyotokana na uzazi kwani vimepungua kutoka 770 mwaka 1990 na kufikia 410 kwa mwaka 2014 kwa kila vizazi hai 100,000 tofauti na lengo tulilojiwekea kufikia Disema 2015 kuwa vipungue kufikia 193 kwa kila vizazi hai 100,000" alisema Dk.Ali.

Alisema Kampeni ya Wazazi Nipendeni awamu ya kwanza ilitengenezwa na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na msaada toka watu wa Marekani kupitia taasisi ya USAID, Mfuko wa Malaria wa Rais wa Marekani na taasisi ya Kukinga na kuzuia Magonjwa.

Dk. Ali alisema programu hiyo ilihusisha kutuma ujumbe uliolenga kuimarisha afya ya mjamzito na mtoto na kuwa ilizinduliwa hapa nchini jijini Mwanza kwa mara ya kwanza mwezi Novemba, 2012.

Alisema katika kampeni hiyo ya masuala ya afya na ustawi wa jamii vyombo vyote vya habari ni muhimu zaidi kuhabarisha na kuwa ujumbe mfupi wa simu za kiganjani wenye taarifa anwai zitakuwa zinatumwa wakati wowote wa ujauzito mpaka mwaka mmoja baada ya kujifungua.

Aliongeza kuwa ili kujiunga mhusika, ndugu, jirani au rafiki atatuma ujumbe "mtoto" kwenda namba 15001 jambo litakalosaidia kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, mtoto mchanga na mtoto alie chini ya miaka mitano.

Alisema uzinduzi wa kampeni hiyo unakwenda sanjari na maonyesho mbalimbali, upimaji wa damu, masuala ya huduma ya VVU na Ukimwi yatakayoanza leo asubuhi viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam.

Dk. Ali alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam na mingine hasa wanaume na wanawake kufika kwenye maonyesho hayo kupata huduma za afya ya uzazi ambayo yataambatana na burudani za muziki kutoka bendi za Wanaume Familia, Ngwasuma, Wanaume Halisi na nyingine nyingi.



Tuesday, July 21, 2015

KAMANDA WA POLISI MKOA WA PWANI JAFARI IBRAHIMU AZUNGUMZIA JUU YA SILAHA ZILIZOKAMATWA


ki1
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina mwandamizi Jafari Ibrahimu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari ofisini kwake kuhusina na watuumiwa wa ujamabzi waliokamatwa pamoja na siraha ambazo wamezikamata baada ya kufanya operesheni katika mapori(Picha na Victor Masangu)
ki2
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina mwandamizi Jafari Ibrahimu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari ofisini kwake kuhusina na watuumiwa wa ujamabzi waliokamatwa pamoja na siraha ambazo wamezikamata baada ya kufanya operesheni katika mapori(Picha na Victor Masangu)
………………………………………………….
VICTOR MASANGU, PWANI
 
KUFUATIA kukithiri kwa wimbi la matukio ya uharifu pamoja na kuvamia vituo vya polisi  Jeshi la polisi Mkoa wa Pwani  limefanya msako mkali katika mapori mbali mbali  na  kufanikiwa kuwanasa watuhumiwa  wa ujambazi  27 pamoja na   risasi 153,bunduki 2  mabomu 3  ambavyo  walikuwa wakivitumia katika matukio ya uharifu.
 
Akizungumza na wa waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina mwandamizi Jafari Ibrahimu amesema kwamba watuhumiwa hao wamekamatwa baada ya kufanyika operesheni katika magenge yaliyopo vichakani na kuwakuta watuhumiwa hao wakiwa wamejificha.
 
 Kamanda amesema kwamba  wameamua kufanya  operesheni  hiyo  kutokana na kuongezeka kwa uharifu katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani na kuwakamata watuhumiwa hao  ambao wengine walikutwa na vifaa mbali mbali ikiwemo visu mapanga,pamoja na nyaya tatu za milipuko ya mabomu.
 
Aidha Kamanda huyo amebainisha kwamba katika zoezi hilo pia waliweza  kukamata madawa ya kulevya aina aya bangi gunia 18 na mirungi kilo 124,lita 88 za pombe ya moshi pamoja na mitambo yake mitatu ya kutengenezea noti bandia 370 na meno ya tembo.
 
 Katika hatua nyingine Kamanda huyo amesema kwamba wanafunzi wawili  wa familia moja katika shule ya msingi mgogodo  iliyopo Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani wamepoteza maisha  baada ya chumba chao walichokuwa wamelala kuteketea kwa moto na kwamba chanzo cha moto huo ni kibatali.
 
 Mkoa wa pwani umekuwa na matukio ya uharifu mbali mbali ikiwemo kuvamiwa kwa vituo vya polisi ikiwemo kituo cha  Kimazichana Wilayani mkuranga ,Ikiwiriri ,kituo kidogo cha mloka,pamoja na tukio la kufanya  jaribio la kutaka kuvamia kituo cha polisi Kibiti vyote vilivyopo Wilayani Rufiji.

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA LASAIDIA MASHINE KWA VIJANA WALIOACHA KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA


 Vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga, Jijini Dar es Salaam  wakishangilia baada ya Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC, Bw. Muungano Saguya alipokabidhi msaada wa mashine tatu za kufyatulia matofali kwa Mlezi wao, Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani Luhanga, Rev. Richard Hananje anayelea  takribani vijana 150 hivi. Shirika limetoa msaada wa mashine hizo tatu za kufyatulia matofali ya kufungamana zenye thamani ya shilingi milioni moja na nusu kwa vijana hao na mtaji  ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato na kusahau utumiaji wa madawa ya kulevya.

Vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam  wakishangilia kwa pamoja na Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC, Bw. Muungano Saguya na Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani Luhanga, Richard Hananje ambaye ni Mlezi wa kikundi hicho chenye vijana takribani 150 hivi. Shirika limetoa msaada wa mashine ili kuunga mkono juhudi za Kituo hicho za kuokoa maisha ya vijana wanaojihusisha na madawa ya kulevya. 
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw. Muungano Saguya akikabidhiana mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana na Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani Luhanga, Richard Hananje  kwa ajili ya kuwapatia vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam. Shirika hilo limetoa msaada wa mashine hizo za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
Afisa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Edith Nguruwe akijadiliana jambo na baadhi ya vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam, baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
Vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam wakimsikiliza Meneja wa Huduma kwa Jamii, Muungano Saguya (hayupo Pichani) baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya akizungumza na vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam, baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
  Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya akizungumza na vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam, baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya akijadiliana jambo na mmoja wa vijana waathirika wa madawa ya kulevya ambao wamebadilika kabisa tabia na sasa wanafanya shughuli mbalimbali za kujipatia kipato.
  Vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam wakimsikiliza Meneja wa Huduma kwa Jamii, Muungano Saguya  baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
  Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya akizungumza na vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam, baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
  Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya akimkabidhi kiasi cha pesa kwa Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani Luhanga, Richard Hananje kwaajili ya kuwasaidia vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam, baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
 Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani Luhanga, Richard Hananje akizungumza na vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam, baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.
Afisa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Edith Nguruwe akijadiliana jambo na baadhi ya vijana walioacha kutumia dawa za kulevya katika eneo la Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam, baada ya Shirika hilo kutoa msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana kwa vijana hao ili waweze kujishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.

"MKUFYA ATANGAZA NIA YA UBUNGE JIMBO LA TABORA MJINI KUPITIA CHADEMA"


WARSHA YA KUPUNGUZA VIFO NA MAJERUHI WA AJALI ZA BARABARANI YAFANYIKA JIJINI DAR-ES-SALAAM

????????????????????????????????????
Kamishina Msaidizi wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Johansen Kahatano akifungua rasmi warsha ya waandishi wa habari ya kupunguza ajali na vifo vinavyotokana na ajali za barabarani iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la AMEND na kufadhiliwa na Jumuiya ya Umoja wa Ulaya EU warsha hiyo imefanyika kwenye jengo la Umoja House jijini Dar es salaam.
????????????????????????????????????
Gianluca Azzon Mwakilishi wa EU Nchini Tanzania akiwasilisha mada katika warsha ya waandishi wa habari ya kupunguza ajali na vifo vinavyotokana na ajali za barabarani iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la AMEND na kufadhiliwa na Jumuiya ya Umoja wa Ulaya EU warsha hiyo imefanyika kwenye jengo la Umoja House jijini Dar es salaam.
????????????????????????????????????
Tom Bishop kutoka shirika lisilo la Kiserikali la AMEND akiwasilisha mada katika warsha ya waandishi wa habari ya kupunguza ajali na vifo vinavyotokana na ajali za barabarani iliyoandaliwa na shirika hilo na kufadhiliwa na Jumuiya ya umoja wa Ulaya EU warsha hiyo imefanyika kwenye jengo la Umoja House jijini Dar es salaam.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wataalamu na taasisi mbalimbali za serikali, Umoja wa Ulaya na Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na waandishi wa habari wakifuatilia mada mbalimbali katika warsha hiyo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wataalamu na taasisi mbalimbali za serikali, Umoja wa Ulaya na Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na waandishi wa habari wakifuatilia mada mbalimbali katika warsha hiyo.
????????????????????????????????????
Kamishina Msaidizi wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Johansen Kahatano akimkabidhi cheti cha ushiriki wa warsha hiyo Mkurugenzi wa mtandao wa Fullshangweblog Bw. John Bukuku.
????????????????????????????????????
Kamishina Msaidizi wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Johansen Kahatano akimkabidhi cheti cha ushiriki wa warsha hiyo Kibuda Chalila Mwandishi mwandamizi wa Michuzi Media.
????????????????????????????????????
Kamishina Msaidizi wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Johansen Kahatano akimkabidhi cheti cha ushiriki wa warsha hiyo Mwandishi wa habari wa magazeti ya serikali TSN Bi. Regina Kumba.
????????????????????????????????????
Washiriki wa Warsha hiyo wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika warsha hiyo
????????????????????????????????????
Na Mwandishi Wetu
Imeelezwa kuwa suala la usalama barabarani ni ni jukumu la kikosi cha usalama barabarani hali ambayo jamii imejengeka na utamaduni huo na kusahau suala hilo ni jamii nzima katika mapambano ya kupunguza ajali za barabarani.

Hayo ameyasema leo Kamishina Msaidizi wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Johansen Kahatano wakati wa mafunzo kwa waandishi habari juu ya kuhabarisha jamii katika suala la usalama barabarani iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU)
Kahatano amesema kuwa kikosi cha usalama barabarani kimekuwa kikitoa elimu juu ya usalama barabarani kwa wananchi pamoja na madereva katika kuzingatia sheria zilizowekwa katika kuondokana na ajali zinazotokana na makosa ya kibinadamu.

Amesema jamii ikipata mwamko wa katika kutambua sheria za usalama barabarani kuna uwezekano wa kuondokana na ajali ambazo zinapoteza watu pamoja na kuacha watu wengine wakiwa na ulemavu wa kudumu.

“Kikosi cha usalama barabani pekee yake hakiwezi ni wakati umefika kwa jamii kuweka suala hili kwenye vichwa vyao kuwa wanamchango katika wa kusukuma gurudumu katika kupambana na ajali katika sehemu zao”amesema Kahatano.

Katika kuhamasisha masuala ya Usalama Barabarani ,Mwandishi wa Citizeni Mkinga Mkinga amesema ni wakati umefika kwa waandishi kutambua umuhimu wetu wa kutoa taarifa za kuelimisha wananchi juu ya usalama barabarani.

Umoja wa Ulaya utaendelea kushirikiana na Tanzania katika mradi wa uboreshaji wa miundombinu katika mashule ili kuweza kuondokana na ajali za wanafunzi katika maeneo ya karibu na barabara.

"LEMBELI AITOSA CCM,AJIUNGA RASMI CHADEMA"


Aliyekuwa Mbunge wa Kahama kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), James David Lembeli (kushoto) akiingia ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Dar es Salaam leo asubuhi akiwa ameongozana na mtoto wake, Wizilya Lembeli wakati akienda kutangaza kuondoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kahama mkoani Shinyanga, James David Lembeli, akizungumza na waandishi wa habari Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Dar es Salaam leo asubuhi wakati akitangaza kuondoka katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pamoja na kutangaza nia ya kugombea ubunge kupitia chama hicho.
 Lembeli akizungumza na wanahabari.
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.

Wanahabari wakimsikiliza Lembeli. Suleiman Msuya

Na Mwandishi Wetu

ALIYEKUWA Mbunge wa Kahama James Lembeli, amehamia rasmi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akitokea Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tukio hilo la kuhama lilifanyika jijini Dar es Salaam leo asubuhi katika Hoteli ya Blue Pearl, Ubungo Plaza ambapo aliambatana na mwanae ambaye alijitambulisha kwa jina Wizilya James.

Akizungumzia uamuzi wake huo Lembeli alisema amekuwa ndani ya CCM kwa miaka yake yote lakini kutokana na vitendo vinavyofanyika ndani ya chama hicho ameaona akae pembeni.

Lembeli alisema, ndani ya CCM ili ufanikiwe kupita michakato yote sahihi ni lazima utoe rushwa au kuiba kura jambo ambalo yeye analipiga vita hivyo kutofautiana na viongozi wa chama ngazi ya Wilaya.

"Ndani ya CCM rushwa imekuwa ibada inasumu kali kuliko ukimwi hivyo nimeshindwa kuvumilia naona Chadema wana viashiria vinavyofanana na mimi ngoja tukafanye kazi," alisema Lembeli.

Alisema katika harakati za kupata wagombea katika jimbo la Kahama kila mwaka ni lazima rushwa itumike lakini chama kimekuwa kimya na kuwabeba wale watoa rushwa.

Mbunge huyo alisema ushahidi wa watu kutoa rushwa hasa katika kipindi hiki umeonekana lakini wahusika wameendelea na hatua zingine bila kukemewa.

"Mimi mwaka 2010 nilikuwa nimekatwa lakini huruma ya Rais Jakaya Kikwete nilirejeshwa sasa nimeona hakuna sababu ya kuendelea kulazimisha kama viongozi hawakutaki," alisema.

Alisema iwapo angechukua fomu CCM mkakati ambao ulikuwepo ni kumkata kwa kile ambacho wanaamini kuwa amekuwa akisimamia misimamo ambayo ina madhara kwa Serikali.

Lembele alisema kutokana na dhana hiyo ni vema aende katika chama ambacho kinaonekana kuwa wabunge wake wanauchungu na nchi yao na sio kubebana kusiko na sababu.

"Kufanya kosa sio kosa lakini kurudia kosa ni kosa kubwa sana hivyo siwezi kurudia kosa la 2010 hivyo huku Chadema ndiko sahihi," alisema.

Alisema ukiona mwenzako ananyolewa ni vema kujiandaa kwa kutia maji nywele jambo ambalo ameliona na ameamua kufanya hivyo.

"Siwezi kutoa rushwa kwa sababu sijafunzwa hivyo na hata wananchi wa Kahama wanajua kuwa mimi sio mtoa rushwa hivyo ukiwa hutoi rushwa CCM ni ngumu kukubalika jambo ambalo linafanya kuwa rushwa iwe mbaya kuliko ukimwi," aliongezea.

Akizungumzia kugombea ubunge kupitia Chadema, alisema atafanya hivyo kwani ukweli ni kuwa anakubalika kwa wananchi wote kutokana na misingi yake ya utumishi.

Alisema mpaka anafanya uamuzi huo ameshafanya utafiti ambapo anaamini kuwa atashinda tena kwa kishindo kwani wananchi wa jimbo hilo wanamkubali.

Lembeli alisema kimsingi jimbo la Kahama wapinzani wapo tangu yeye akiwa Mbunge, hivyo anaamini kuwa iwapo atafanikiwa kushinda hatapata wakati mgumu kufanya kazi.

"CCM imefanya mambo mengi ambayo kimsingi hayana afya ndani ya chama ukiwa wa kwanza kwa kura ndani ya CCM unakuwa wa mwisho hali ambayo inakatisha tamaa na hilo lilitokea 2010 na Chadema wakapata ushindi," alisema

Pia alisema amepokea simu na meseji nyingi ambazo kutoka kwa wananchi zinamtaka agombee kupitia chama Chadema hivyo pamoja na ukweli kuwa ni uamuzi mgumu ila hawezi kula matapishi.

Alisema ilimchukua masaa 10 kumuelezea mama yake juu ya uamuzi huo lakini baadae alielewa hivyo kwa sasa ana baraka zote za mama na familia kwa ujumla.

Kuhusu uhusiano na 4U Movement

Akizungumzia kuhusu uamuzi huo kuhusishwa na kundi la 4u Movement, alisema kimsingi kundi hilo analiona kupitia mitandoa ya kijamii ila hana uhusiano nalo na hahitaji kuwa katika hao.

Lembeli alisema wananchi wa Kahama ni watu makini wanajua nini cha kufanya hivyo uamuzi ambao watafanya utakuwa ni kwa uelewa wao na sio kwa msukumo wa kundi hilo linalotajwa kuwa ni wafuasi wa Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa.

Kuhusu Katiba iliyopendekezwa Lembeli alisema yeye ni muumini wa Serikali tatu na alionesha hilo katika vikoa vyote vya bunge lile ambapo alikuwa katika kamati namba moja.

Alisema kutokana na ukweli huo ni dhahiri kuwa ameenda chama ambacho wanafanana kifra kwani bila Serikali tatu hatma ya Tanzania itakuwa mashakani.

"Kwa hili siwezi kubadilika mimi msimamo wangu hadi leo ni Serikali tatu ambapo pia ni msimamo wa Chadema hivyo wengi ndio walishinda lakini mimi sio mmojawapo," alisema.

Aidha Lembeli alitumia muda huo kufafanua ni kwanini alitoa hoja ya kutaka Lowassa na wengine ambao wamekutana na majanga ndani ya bunge wasafishwe ambapo alisema haki haikutendeka kusafisha watu baadhi na wengine kuachwa.

Lembeli alisema katika taarifa ya Operasheni Tokomeza haikusema mawaziri fulani wanamakosa ila iliweka bayana kuwa kulinga na nafasi zao wanapaswa kuwajibika kisiasa.

Alisema mfumo wa kusafisha watu fulani na wengine kuwaacha sio mzuri kwani hauendani na misingi ya haki za binadamu ni ubaguzi.


Kwa upande wa mtoto wake wa pili Wizilya James Lembeli alisema wanamuunga mkono baba yao kwa uamuzi huo na kuwa wako nyuma yake.

Alisema uamuzi ambao amechukua baba yake ni mgumu hasa ukilinganisha na kipindi husika lakini hakuwa na njia nyingine kwani ni mtu wa siasa.

Akizungumzia ujio huo Ofisa Habari wa Chadema ambaye ndiye alimpokea Lembeli alisema kimsingi mwanachama huyo mpya alikiwa ni mpinzani kiroho hivyo hawana shaka naye.

Makene alisema wanaamini kuwa wamepata mtu ambaye anapenda mabadiliko kwani alionekana ndani ya bunge na nje kwa kusimamia rasilimali za nchi bila uoga.

Alisema Chadema itaendelea kupokea wanachama wapya kutoa CCM na vyama vingine hadi Julai 25 kwani lengo lao ni kuhakikisha kuwa nchi inafikia kwenye mabadiliko chanya.

Lembeli amekuwa Mbunge wa jimbo la Kahama, tangu mwaka 2005 hadi 2015 ambapo awali alikuwa  mwandishi na mtumishi katika shirika la Hifashi ya Taifa (Tanapa).

NEW MUSIC VIDEO : EMANUEL AUSTIN FEAT. BEN POL -RUKA JUU


MFAHAMU EMANUEL AUSTIN MTANZANIA MWANAMUZIKI AISHIYE UJERUMANI.

Emanuel  Austin alizaliwa 27.10.1990 Jijini Dar es salaam Tanzania, na ilipofika mwaka 1996  alihamia Ujerumani Kuishi na wazazi wake, Kipaji chake cha kucheza na kuimba kilianza kuonekana mapema.
Akiwa na Miaka mitano Emanuel Austin alianza kuigiza kama anacheza movie pamoja na rafiki zake wa Kiafrika akiwemo Gregory Msuya na Michael Jackson.  Alipofika umri wa Miaka 15 alianza kupenda na kuimba muziki wa Kugani yani ‘Hip hop’
Baadaye alitafuta baadhi ya wenzake ambao aliona wanaweza kuingia studio na kufanya muziki wa Kughani yaani Rap baadhi ya marafiki zake walikuwa ni pamoja na Miguel Amil Matos, Bernado Ernest na Patrick Kitchens ambapo kwa Mara ya kwanza walifanya vizuri.
Mnamo mwaka 2002 wazazi wake na Emanuel walianzisha Mradi mkubwa wa shule kwa ajili ya kufundisha Salsa huko Großkrotzenburg  jirani na  Frankfurt , ambapo yeye binafsi alijifunza Salsa na sasa amekuwa ni mwalimu mzuri wa Mtindo huo. Na kuanzia mwaka 2005 Emanuel  na baba yake wamekuwa wakiendesha programu ya kuwafundisha watoto salsa.
Kipaji cha nyota Mwanamuziki Emanuel Austin kilianza kuonekana wakati ameanza kuimba Lebo ya MarciRecords moja ya sehemu ambayo inawaunganisha wanamuziki mbalimbali na vijana ambao wanavipaji katika sanaa ya Muziki, akiwa huko Emanuel alishinda tuzo ya Msanii anayechipukia ndani ya Mji wa Hanau, Ujerumani  mwaka 2006.
Mwaka 2007 Emanuel alifanya video yake ya kwanza kupitia wimbo wake wa Put your hands up wimbo uliotoka katika album yake ya Put your Hands up, Album hiyo ilitengenezwa na Muandaaji wa Muziki Dj Verde.
Mwaka 2008 Emanuel alifanya ngoma nyengine ambapo alitoa audio pamoja na video , ngoma hiyo ilikwenda kwa jina la Master of the Game, chini ya usimamizi wa mwandaaji wa Muziki Axel Breitung hii ilikuwa ni nyimbo ambayo ilimuongezea umaarufu zaidi na kusikika katika chanel maarufu za Televisheni kama VIVA na MTV.
Kutokana na mafanikio hayo makubwa Emanuel alianza kuandaa matukio mbalimbali ikiwa ni pamoja na matamasha ya muziki , Mwaka 2008 Emanuel aliamua kufungua darasa la mafunzo ambapo ilikuwa ni Shule ya Muziki inayoitwa Tanzschule Weiss iliyopo Offenbach, ambapo wanafundisha Hip hop, Kuwafundisha watoto kucheza na Salsa Cubana na anampango wa kuanzisha shule ya Muziki Nchini Tanzania.
Kwa sasa Emanuel Austin anafanya kazi katika moja ya shule kubwa ya Muziki wa Dance nchini  Ujerumani  ambapo wachezaji maarufu wa Dance kama Don Omar wapo humo , hata hivyo Emanuel huja nyumbani Tanzania kila mwaka  na sasa Amekuja na ngoma mpya ambayo amemshirikisha Ben Pol inaitwa ruka juu.

Kufahamu zaidi juu ya Emanuel Austin   Mfuate hapa
.
www.instagram.com/emanuelaustinofficial 
www.facebook.com/emanuelaustin 
YouTube : Emanuel Austin 
Twitter: emanuelaustin27 

www.twitter.com/emanuelaustin27

"DOGO" AJITOSA UDIWANI KUPITIA CHADEMA KATA YA KORONGONI MJINI MOSHI.

Mpambanaji aliyejitambulisha kwa mwandishi wa blog hii kwa jina la Liberatus Oba Mawalla "Dogo" (pichani juu) amechukua na kurudisha fomu za kugombea udiwani kata ya Korongoni wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Amesema endapo atapata ridhaa hatapenda wamuite mheshimiwa na badala yake anataka wapiga kura wake wamuite ndugu. Angalia picha zaidi hapa chini

Dogo akiwa na wanachama hicho

Msafara kuelekea kurudisha fomu ukijipanga.

Hapa ni furaha tupu.

Dogo akiwa na vijana wa chama hicho.

Akisaini wakati akichukua fomu.

Hapa ni ushindi tu.


Msafara huo kurudisha fomu.

Ni alama ya vidole viwili chadema .



Ni furaha tu kwa kwenda mbele.




Dogo ndani ya mchuma akienda kurudisha fomu.

Ni kama wanasema ushindi ni lazima.

Msafara huo wa kwenda kurudisha fomu.

Dogo akipongezwa na vijana wenzake.