Pages

KAPIPI TV

Sunday, May 24, 2015

JK AONGOZA KIKAO CHA NEC LEO TENA

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akishauriana jambo na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kabla ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kuanza leo, mjini Dodoma Nkoromo)
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, mjini Dodoma leo, May 24, 2015. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bara, Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. (Picha na Bashir Nkoromo)
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, wakiwa kwenye kikao hicho. mstari wa mbele kutoka kushoto ni, Dk. Salim Ahmed Salim, Shamsi Vuai Nahodha na Katibu Mkuu wa CCM, mstaafu, Wilson Mukama
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Mwigulu Nchemba na Spika wa Bunge Anna Makinda.
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM,  Bernard Membe na Nazir Kalamagi wakijadiliana jambo kabla ya kikao cha NEC kuanza.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Usi Yahya Haji kutoka Kaskazini Unguja, akimsalimia mjumbe mwenzake, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu wakati wakijiandaa kuingia ukumbini kwenye Kikao cha NEC mjini Dodma leo.
Katibu Mkuu wa UVCCM, Sixtus Mapunda akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Hamis Sadifa, kabla ya kikao kuanza. Kulia ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Wajumbe wakiwa ukumbini wakati wa mkutano huo









Saturday, May 23, 2015

NEED FOR INCLUSIVE QUALITY EDUCATION FOR ALL DOMINATES WORLD EDUCATION FORUM

WordEduForum-01-L
Opening of World Education Forum 2015, Seoul. UN Secretary-General Ban Ki-moon centre, at the opening of the World Education Forum 2015, in Seoul. He is flanked by Hwang Woo-yea (left), Deputy Prime Minister and Minister of Education of the Republic of Korea; and Irina Bokova, Director-General of the UN Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO). 19 May 2015. Seoul, Republic of Korea. (UN Photo/Evan Schneider).

Tanzania’s Minister for Education and Vocational Training (MoEVT), Honourable Dr. Jumanne Shukuru Kawambwa with a delegation of four most senior officials from Tanzania Mainland and Zanzibar and a representative from the Civil Society are attending the Third World Education Forum (WEF) from 19-22 May 2015 in Incheon, Republic of Korea. 

The 2015 WEF is the third after the Jomtien WEF of 1990 and the Dakar WEF of 2000. The 2015 forum takes stock of achievements and challenges since the Dakar WEF and deliberates on the education agenda for the next fifteen years (2015-2030).

Tanzania was represented by a high profile delegation that consisted of two the Permanent Secretaries (from the Ministry of Education and Vocational Training and from the Prime Minister’s Office-Regional Administration and Local Governments), the Commissioner for Education from MoEVT as well as the Deputy Principal Secretary from MoEVT Zanzibar. 

The Civil Society is represented by HakiElimu which is a member organization of the Tanzania Education Network (TEN/MET).

UNESCO is taking the lead in coordinating WEF with the collaboration of UNDP, UNHCR, UNFPA, UNICEF, UN Women and the World Bank (WB). 

The opening ceremony was attended by a number of high profile key speakers including Ms. Irina Bokova the Director General of UNESCO, representatives from the Government of the Republic of Korea and Mr Ban Ki-moon, the United Nations Secretary General, to mention but a few.

The 2015 WEF seeks to take stock of achievements and shortfalls in the implementation of the Millennium Development Goals since the year 2000. 

 The forum will also agree on a joint position for the education goal and targets in the post millennium development period (post 2015 development agenda). 

The agreements from the forum will be adopted by UN Member States at a Summit in September 2015;

The forum will further agree on a framework to support the implementation of the future education goal which focuses on equitable and inclusive quality education and lifelong learning for all by 2030.

UNESCO Dar es Salaam office, in collaboration with UNICEF, the WB and DFID are pleased to support the successful participation of the United Republic of Tanzania to the 2015 World education Forum

UNESCO WATOA MAFUNZO YA TEHAMA KWA WALIMU WA VYUO VYA UALIMU HAPA NCHINI

Washiriki wa mafunzo wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumaliza mafunzo ya matumizi ya Tehama katika ufundishaji kwenye vyuo vya ualimu.
Na Geofrey Adroph, Pamoja blog Shirika la Umoja wa Mataifa Elimu ya Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limejikita katika uboreshaji wa elimu kwa kuwapa mafunzo walimu katika somo la Teknnolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama). 

 Akizungumza leo katika Ufungaji wa Mafunzo yaliyoandaliwa na UNESCO wakishirikiana na China Funds in Trust Project (CFIT) yaliyofanyika kwa siku tano katika Ukumbi wa DIT, Jijini Dar es Salaam, Ofisa Miradi wa UNESCO, Faith Shayo amesema mafunzo waliopata walimu wa vyuo vya walimu mbalimbali nchini itawasaidia katika uboresha wa elimu ikiwa ni pamoja na kuwapa vifaa vitakavyotumika katika kufundishia somo hilo. 

 Faith amesema ufundishaji na uelimishaji namna ya matumizi ya Tehama hii inatokana na baada ya mkutano wa viongozi wa vyuo mbalimbali pamoja na wadau wa elimu wa hapa nchini kuona kuna mapungufu katika masuala la uelewa na matumizi ya Tehama katika vyuo vilivyopo nchini. Amesema katika kufikia malengo ya mradi wa UNESCO-China Funds in Trust Project (CFIT) wanaoshirikiana na vyuo vya elimu hapa nchini kwa malengo makuu matatu.  
Aliyataja malengo hayo ni kuboresha elimu kwa walimu wa vyuo vya ualimu, kuweka mafunzo ya walimu wanapofundisha katika somo la Tehama ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia pamoja na kuwanunulia vifaa vya Tehama ambavyo vitasaidia katika kufundishia.  

Faith amesema baada ya mafunzo hayo vyuo vitapata vifaa mbalimbali ambayo ni kompyuta, Projecta,ya na vifaa vya kuzalisha umeme wa jua (Solar Energy) kwa ajili ya kuondokana na tatizo umeme unaokatika katika mara kwa mara. Wakufunzi wa mafunzo hayo ni Mkuu wa idara ya maendeleo ya biashara kutoka (DIT), Daudi Mboma pamoja na Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria (OUT) Godfrey Haongo ambao wanajukumu la kuwafundisha walimu mbalimbali kutoka vyuo tofauti hapa .  

Waliopata mafunzo hayo Waalimu tisa wa Chuo cha Ualimu Tabora, na tisa wengine kutoka chuo cha ualimu Monduli , walimu wanne kutoka chuo cha ualimu Morogoro, na mmoja kutoka Shule direct, wawili kutoka Chuo kikuu cha Nelson Mandela, mmoja kutoka Ngorongoro Waso District. 

  Mafunzo hayo yametolewa kwa baadhi ya watumishi wa Wizara ya elimu ambao wana mchango mkubwa hasa katika ukuzaji wa Tehama wakishirikiana na wanafanya kazi wa UNESCO ili kuweza kufikia malengo ya mradi huo kwa vyuo vya elimu hapa nchini. 

Kutokana na kuwa na uelewa mdogo wa masuala ya Tehama UNESCO wamejipanga kuweza kupambana na kutoa mafunzo ya kiteknolojia ili kuweza kuboresha matumizi na upatikanaji wa huduma za kitehama katika taifa kwa kuanzisha mradi huo wa kutoa mafunzo kwa walimu nao walimu waweze kwenda kuutumia ujuzi huo katika ufundishaji kwenye vyuo wanavyofundisha ilikuweza kuwapa upeo mkubwa wanafunzi wa ualimu ambao ndio watakao kuwa kipaumbele katika kufanya nchi iwe katika mfumo mzuri wa Tehama.

REGISTRATION IS NOW OPEN FOR IMPACT ASSESSMENT EVALUATION SHORT COURSE

Untitled
Venue – ESRF Conference Hall
Date - 1st-5th June 2015
Course Objective:
This course on Impact Assessment Evaluation will provide researchers, project managers, policy makers, and practitioners of development with the necessary methodology and practical knowledge to meet the growing demand for rigorous evaluation of development programmes.
Learning Outcome
In this course you will learn how to design an impact evaluation of a development intervention employing both quantitative and qualitative methods. Some of the questions you will be able to answer include:
How do we frame the right evaluation questions and choose the right indicators?
What are the best impact evaluation methodologies?
How do we go beyond simple impact assessment by assessing spill-over effects, cost-effectiveness and impact on vulnerable groups?
What are cutting-edge qualitative and quantitative methods for impact assessment?
Should there be any interest from you or your organization email us on trainings@esrf.or.tz by Wednesday 27th May 2015.
Thank you for your valuable time it is much appreciated.

UNESCO IMEAHIDI KUWASAIDIA WATANZANIA KUKABILI DHULUMA DHIDI YA WANAOISHI NA ALBINISM

DSC_0349
Kiongozi wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake jijini Mwanza akiwa ameambatana na Mbunge wa Viti Maalum CCM, anayetetea maslahi ya watu wenye albinism, Mh. Al-Shaymaa Kwegyir (wa pili kulia) pamoja na Semeni Kingaru (wa tatu kulia).(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).

Na Mwandishi wetu, Mwanza
SHIRIKA la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) limeahidi kusaidia mapambano dhidi ya unyanyasaji na dhuluma zinazofanywa jamii dhidi ya watu wenye albinism.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Kiongozi wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues wakati akizungumza na mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo.

Mwakilishi huyo wa Unesco amesema hayo alipomtembelea Mkuu wa mkoa kumsalimia na kumweleza hatua zinazochukuliwana Unesco katika kukabiliana na ukatili dhidi ya watu wenye albinism.

Akifafanua zaidi alisema kwamba UNESCO haijatenga fedha zitakazotumika kuendesha kampeni mahsusi bali itatumia uwezo wa kiufundi uliopo kwa wataalamu walionao na kwamba wanakusudia kuona kwamba miaka 15 ijayo watoto wanaozaliwa nchini Tanzania wanakuwa huru pasipo na viashiria vya kuhatarisha maisha vinavyosababishwa na mauaji ya watu wenye albinism.

Akimkaribisha Bi Zulmira ofisini kwake, Mkuu wa mkoa Magesa Mulongo alisema kwamba ingawa kuna utulivu katika kipindi hiki mkoani Mwanza, bado mkoa wake unaendelea kukabiliana na viashiria vinavyosababisha ukatili kwa watu wenye albinism na wazee.

Bwana Magesa alisema imani potofu zilizopo zinazosadikika kufanikisha biashara za uvuvi wa samaki, uchimbaji wa madini na wanasiasa kuendelea na madaraka ni miongoni mwa sababu kubwa za mauaji hayo yaliyoitia doa jeusi jamii ya kitanzania nje ya mipaka.

Alisema kwamba jitihada zinafanywa kukabiliana na imani hizo potofu kwa kuihamasisha jamii kutoziamini na kwamba madaraka na utajiri unatokana na juhudi, kufanya kazi kwa bidii na si vinginevyo.

Aidha amesema mkoa wake umekuwa ukihakikisha kwamba makundi yanayotumika kuua watu wengine kwa kushirikisha jamii yanavunjwa na pia kuwachukulia hatua kali wote wanaobainika kushiriki kwa njia moja au nyingine.

Hata hivyo mwakilishi wa umoja wa mataifa alisema kwamba hali ya amani itatawala pale tu watu watakapobaini kwamba kuua ni ukiukwaji wa haki za binadamu na ni kosa la jinai.

Alisema pindi binadamu watakapokiri kwamba binadamu wote ni sawa na kuishi na albinism sio ‘mzimu’ watabadili mwelekeo mzima wa fikra potofu kimaisha na kuishi kwa amani na kuthaminiana.

Bi Zulmira alimwambia mkuu wa mkoa kwamba UNESCO kwa kushirikiana na wadau wengine wataendesha makongamano yenye lengo la kushirikisha jamii katika kuandaa na kutekeleza mikakati itakayo changia kuzuia na kutokomeza unyanyasaji na dhuluma zinazofanya dhidi ya watu wenye albinism.
DSC_0373
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo (kushoto) akizungumza na Kiongozi wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues (kushoto) aliyeambatana na Mbunge wa Viti Maalum CCM, anayetetea maslahi ya watu wenye albinism, Mh. Al-Shaymaa Kwegyir (wa pili kulia) pamoja na Semeni Kingaru (wa tatu kulia) alipomtembelea ofisini kwake jijini Mwanza. Wa pili kushoto ni Katibu Tawala wa mkoa wa Mwaza, Faisal Issa.

Warsha hizo zitafanyika kwa wakati tofauti katika kipindi cha wiki mbili wilayani Sengerema, Misungwi, Msalala na Bariadi. Warsha hizo zilizoanzia Sengerema Jumatano na kumalizika Ijumaa zitafuatiwa na Misungwi Mei 25 hadi 27, Msalala Mei 28 hadi 30 na Bariadi kuanzia Mei 28-30.

Katika warsha hiyo pamoja na kujadili mada mbalimbali, mijadala itahusisha viongozi wa serikali, wanasiasa, viongozi wa kidini na kimila na hoja kubwa itakayojadiliwa ni dhana ya kisayansi ya albinism, mitazamo ya jamii kuhusu dhana hiyo, makundi mbalimbali ndani ya jamii, tofauti kati ya utamaduni na asili.

Pia watajadili kubainisha na kuanisha matatizo, changamoto na hatari zinazowakabili watu wenye alibinism na kuchambua mambo yanayochangia uwepo wa changamoto na hatari kwa watu wenye alibinism.

Katika majadiliano hayo pia mikakati inayoweza kupunguza au kumaliza kabisa matatizo changamoto na hatari zinazowakabili watu wenye alibinism katika jamii yetu itatazamwa.

Watoa mada wanatarajiwa kutoka katika halmashauri, vyama vinavyotetea maslahi ya albinism, mbunge anayetetea maslahi ya watu wenye albinism Al-Shaymaa Kwegyir na mwakilishi kutoka baraza la taifa la dawa asilia.
DSC_0357
DSC_0369
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo akiendelea na maongezi na ugeni huo ofisini kwake jijini Mwanza.
DSC_0377
Kiongozi wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues (kulia), akielezea nia ya Shirika lake kusaidia mapambano dhidi ya unyanyasaji na dhuluma zinazofanywa jamii dhidi ya watu wenye albinism nchini alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo ofisini kwake jijini Mwanza.
DSC_0391

TAARIFA RASMI YA CCM KUHUSU KIKAO CHA KAMATI KUU

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kamati Kuu imepokea na kutafakari taarifa ya Kamati ya Usalama na Maadili ambayo ilipitia adhabu waliyopewa wanachama sita waliokiuka kanuni za Maadili na kupewa Onyo Kali, adhabu iliyodumu kwa kipindi kisichopungua miezi 12.

Wanachama hao sita ni;-
i. January Makamba
ii. Willium Ngeleja
iii. Steven Wasira
iv. Bernard Membe
v. Edward Lowassa
vi. Fredrick Sumaye

Kamati Kuu imepokea na kukubali pendekezo la Kamati ya Usalama na Maadili ya kumalizaka kwa kipindi cha adhabu kwa wanachama hawa. Kwahiyo adhabu hiyo kwa sasa imemalizika, na wanachama hao wameruhusiwa kuendelea na shughuli zao katika Chama.

Hata hivyo Kamati Kuu inawataka wanachama hawa na wale wengine wenye nia ya kugombea Urais kupitia CCM Kuzisoma , Kuziheshimu na Kuzizingatia Kanuni za Maadili za CCM na kanuni zingine zinazoongoza mchakato ndani ya Chama, ili wasikumbwe na adhabu itokanayo na kuzivunja kanuni hizo.

Wale wote wanaotaka kugombea, yaani waliokuwa kwenye adhabu na wengine watakaojiingiza kwenye kampeni mapema na hivyo kukiuka maadili na miiko ya Chama, taarifa za kukiuka kwao zitatumiwa wakati wa kuchuja majina ya wagombea utakapofika.

Taarifa hizo zitatumika katika kuwapima na kuamua iwapo wana sifa za kutosha na wanafaa au hawafai katika kupata uteuzi wa nafasi wanayoiomba.


Imetolewa na;-
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
22/05/2015

Nape Moses Nnauye
CCM Secretary for Ideology & Publicity

Friday, May 22, 2015

SKYLIGHT BAND YAREJESHA RATIBA YAKE YA BURUDANI KILA IJUMAA, SASA NI KIOTA KIPYA CHA LUCAS PUB MASAKI LEO

IMG-20150520-WA0074
Waimbaji wa Skylight Band wakiendelea kutoa burudani kwa wapenzi na mashabiki wa bendi hiyo (hawapo pichani).
Ashura Kitenge mwenye sauti ya kumtoa nyoka panoni akiimba kwa hisia kali huku akisindikizwa na Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK 47 Jumamosi iliyopita ndani ya Mzalendo Pub.
Waimbaji wa bendi ya Skylight wakiendelea kutoa burudani ndani ya kijiwe cha Mzalendo jumamosi iliyopita wa kwanza kushoto ni Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower, Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK 47(katikati) pamoja na Ashura Kitenge(kushoto)
Sam Mapenzi akitoa burudani huku akisindikizwa na wanamziki wenzake waliokuwa wakimpa support ya nguvu kwenye ngoma za Nigeria ambao ni Joniko Flower(wa kwanza kushoto), Ashura Kitenge(wa pili kutoka kulia) pamoja na Sony Masamba.
Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK 47 akiimba mmoja ya nyimbo yenye hisia kali sambamba na msanii mwenzake Sam Mapenzi kwenye kiota cha Mzalendo Pub wanapokinukisha kila siku za Jumamosi.
Waimbaji wa Skylight Band wakicheza moja ya nyimbo zao
Ashura Kitenge akiimba kwa pamoja na Sam Mapenzi mbele ya mashabiki wa Skylight Band(hawapo pichani)
Sony Masamba(kulia) akiendelea kutoa burudani huku akisindikizwa na wanamziki wenzake ambao ni Sam Mapenzia(katikati) pamoja na Joniko Flower (wa kwanza kushoto)
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akiimba kwa hisia huku akisindikizwa na mwimbaji mwenzake Ashura Kitenge
Sony Masamba(kushoto) akiendelea kutoa burudani huku akisindikizwa na wanamziki wenzake ambao ni Aneth Kushaba(katikati) pamoja na Sam Mapenzi(Kulia)
Ilikuwa noma sana jumamosi hii maana ilikuwa ni kubeneka mpaka kunakucha
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower huku akisindikizwa na Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK 47(katikati) pamoja na Ashura Kitenge
Waimbaji wa bendi ya Skylight Band wakiendelea kusebeneka ndani ya Mzalendo Pub
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akishusha mistari na kucheza huku waimbaji wenzake Aneth Kushaba (wa pili kutoka kushoto), Sony Masamba(wa pili kutoka kulia) pamoja na Ashura Kitenge wakisebeneka jumamosi iliyopita ndani ya Mzalendo Pub jijini Dar.

Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba akiendelea kuimba huku wapenzi wa bendi hiyo wakiendelea kukata mauno yaani ilikuwa noma sana.

Thursday, May 21, 2015

KIPINDUPINDU TISHIO KAMBI YA WAKIMBIZI WA BURUNDI NYARUGUSU, OXFAM YATOA


 Baadhi ya wakimbizi wakiwa wamewasili Kigoma
 Wakimbizi kutoka Burundi wakisubiri huduma mbalimbali za kijamii
 Mmoja wa wakimbizi akiwa anapata matibabu
 Hapa watoto wa wakimbizi wakijipikia Chakula , katika mazingira hatarishi
 Mamia ya wakimbizi wakiwa wanatafakari hatima yao
 Hii ndio hali halisi ya vyoo ambavyo vimechangia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu
Wafanyakazi wa Shirika la Oxfam wakishusha vifaa kwa ajili ya vifaa vya upatikanaji wa maji na vyoo ili kubabiliana na Kipindupindu. 
 Hiki ni moja ya chanzo cha maji
 Wakimbizi wakiwa ndani ya Meli

Ongezeko la wakimbizi kutoka nchi jirani ya Burundi pamoja na ukosefu wa huduma za msingi ikiwemo maji safi linamaanisha kuongezeka kwa hatari ya mlipuko wa magonjwa ya kuambukizwa hasa kwa wakimbizi takribani 40,000 walioko Kagunga mpakani mwa Tanzania. 

Tayari watu 20 wamethibitishwa kuwa na ugonjwa wa kipindupindu katika maeneo ya Kagunga na katika kambi ya Nyarugusu ambapo wakimbizi hupelekwa kwa ajili ya makazi.

Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) limeripoti uwepo wa watu 1057 wenye dalili za kuharisha waliopo Kagunga ambapo wakimbizi husubiria usafiri wa boti zinazowasafirisha kwenda Kigoma. 

Kuna uhitaji wa haraka sana wa huduma za msingi ikiwemo maji safi na vyoo. Shirika la Oxfam linafanya kazi na shirika la TWESA ili kutoa ufumbuzi wa haraka kukidhi mahitaji hayo kwani kuna uhitaji wa haraka sana wa maji safi, huduma za matibabu pamoja na vyoo. 

Shirika la Oxfam tayari limeanza maandalizi ya haraka ili kuongeza upatikanaji wa maji safi na kujenga vyoo vya dharura katika kambi ya Nyarugusu ili kukabiliana na ongezeko kubwa la wakimbizi. 

Inakadiriwa takribani wakimbizi 22,000 wamesafirishwa kutoka Kagunga kwenda katika kambi ya Nyarugusu ambapo wanapewa makazi ya muda mfupi katika shule na makanisa wakati mashirika mbalimbali ya misaada yakiendelea kutoa vifaa vya ujenzi wa makazi ya muda mrefu. 

Huduma za matibabu katika makambi ya wakimbizi zinasua sua kutokana na ongezeko kubwa la watu wenye magonjwa mbalimbali.

Uhitaji wa haraka wa huduma za msingi ni muhimu ili kuzuia ongezeko la magonjwa yanayosambaa kama kipindupindu. 


BALOZI WA PSPF FLAVIANA MATATA ATOA ELIMU YA FURSA MBALIMBALI ZINAZOPATIKANA KATIKA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF KWA WANAFUNZI WA VYUO MBALIMBALI JIJINI



 Balozi wa PSPF, Bi. Flaviana Matata akitoa elimu kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya juu (hawapo pichani) jijini Mwanza
 Afisa Mfawidhi Ofisi ya PSPF Mwanza, Bw. Salim Salim, akisalimiana na Balozi wa PSPF, Bi. Flaviana Matata, kabla ya kuanza semina ya siku moja kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya juu jijini Mwanza.
Baadhi ya wanafunzi wakisoma vipeperushi vyenye taarifa kuhusu Mfuko wa PSPF wakati wa semina juu ya Mfuko huo iliyotolewa na Balozi wa PSPF, Bi. Flaviana Matata hivi karibuni.
Mmoja wa wanafunzi waliohudhuria semina juu ya Mfuko huo iliyotolewa na Balozi wa PSPF, Bi. Flaviana Matata hivi karibuni akiuliza swali ili kapata ufafanuzi.
 Balozi wa PSPF, Bi. Flaviana Matata (mstari wa mbele katikati), katika picha ya pamoja na wanafunzi wa vyuo mbalimbali wa elimu ya juu jijini Mwanza baada ya kuotoa elimu kwa wanafunzi hao juu ya fursa mbalimbali zinazopatikana kwa kuwa mwanachama wa PSPF.