Pages

KAPIPI TV

Thursday, September 4, 2014

MKURUGENZI NHC ATEMBELEA ENEO LA MRADI WA NYUMBA ZA WATUMISHI HALMASHAURI YA BUSOKELO MBEYA

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Kyando Mchechu wa kwanza kulia mbele akitembelea eneo la ujenzi wa nyumba za gharama nafuu zitakazojengwa  katika Halmashauri ya Busekelo Mkoani Mbeya alipotembelea Halmashauri hiyo  Septemba 3 mwaka huu .Picha na Saguya wa NHC.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Mchechu akielezea mpango wa shirika wa kujenga nyumba za watumishi wa Halmashauri ya Busekelo alipotembelea Halmashauri hiyo jana .Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Busokelo Bw. Meshack Mwakipunga  na kulia  kwa Mkurugenzi Mkuu wa  NHC ni Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Busekelo Bw Saidi Mderu .
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Busokelo Bw,Meshack Mwakipunga akiutembeza ujembe wa shirika la Nyumba la Taifa  kwenye eneo la viwanja vitakavyojengwa  nyumba  na NHC hivi karibuni.
Ujumbe wa NHC na Halmashauri ya Busokelo ukiendelea kutambua  viwanja vitakavyojengwa Nyumba na NHC hivi karibuni
 
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Mchechu akitoa maelezo ya kuridhia eneo walilopewa na Halmashauri ya Busekelo ili kujenga nyumba hivi karibuni.
Ujumbe ukikagua kazi ya kutengeneza matofali kwa ajili ya kujengea nyumba katika Halmashauri ya Busokelo.
Mhandisi wa  miradi ya nyumba wa NHC Kanda ya Mbeya Bw.Mtili akitoa maelezo ya hatua iliyofikiwa ya ufyatuaji wa matofali ya  kujengea nyumba katika Halmashauri hiyo.
 
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC  ulipata fursa ya kutembelea shamba la mwekezaji wa Kilimo cha Maparachichi baada ya kumaliza ziara yake katika Halmashauri ya Busokelo,ambapo kupitia uwekezaji huo wananchi wa busokelo na maeneo mengine wamepata fursa ya ajira.
Ujembe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC ukipewa maelezo na Meya wa Jiji la Mbeya Bw.Athanas Kapunga yanayohusu fursa za uwekezaji ambazo NHC inaweza kuzitumia kukuza uchumi wa jiji hilo.

MGODI WA NORTH MARA WACHANGIA BILIONI 7.5 KATIKA SHUGHULI ZA JAMII


Picha Na 2Mwenyekiti wa Jopo la Majaji kwa ajili ya kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji Prof. Samwel Wangwe (kushoto) akisalimiana na Afisa Mahusiano wa Mgodi wa North Mara Bw. Zakayo Kalebo (kulia) mara baada ya jopo hilo kuwasili kwenye mgodi huo.
Picha Na 3Meneja Mahusiano wa Mgodi wa North Mara Bi Fatuma Mssumi (mbele) akielezea shughuli za mgodi wa North Mara mbele ya jopo la majaji waliotembelea mgodi huo ili kuendelea na zoezi lake la kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji.
Picha Na 5Afisa Uhusiano wa Kijiji cha Matongo Bw. Magesa Wanjara akionesha jinsi ya kutumia bomba la kisima cha maji kilichofadhiliwa na mgodi wa North Mara mbele ya timu ya majaji, sekretarieti na wajumbe wengine.
Picha Na 7Mwenyekiti wa Umoja wa Kikundi cha Vijana cha Nyakegema Bw. Zacharia Mwita ( wa pili kutoka kulia) akitoa maelezo mbele ya timu ya majaji na wajumbe wengine kuhusu mchango wa mgodi wa North Mara kwa kikundi hicho kupitia mradi wake wa mboga za majani. Kikundi hicho kina jumla ya vijana 578 kutoka katika vijiji saba vinavyouzunguka mgodi huo.
Picha Na 9Mwenyekiti wa Jopo la Majaji kwa ajili ya kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji Prof. Samwel Wangwe (kushoto) akisalimiana na Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ingwe Bw. Alfred Joseph mara timu hiyo ilipofanya ziara kwenye shule hiyo iliyofadhiliwa na mgodi wa North Mara.
……………………………………………

Na Greyson Mwase, Tarime
Imeelezwa kuwa mgodi wa North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara umechangia jumla ya shilingi bilioni 7.5 katika kipindi cha mwaka 2013 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo   katika vijiji saba vinavyouzunguka mgodi huo.

Akizungumza mbele ya timu ya majaji kwa ajili ya kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji chini ya mwenyekiti wake Prof. Samwel Wangwe Meneja Mahusiano wa Mgodi huyo Bi Fatuma Mssumi alitaja vijiji hivyo kuwa ni pamoja na Nyangoto, Nyamwaga, Nyakunguru, Kerende, Kewanja, Genkuru na Matongo.

Bi Mssumi alisema kuwa kupitia sekta ya elimu, mgodi ulichangia madawati 2700 yenye thamani ya shilingi milioni 251.9 kwa ajili ya shule mbalimbali za msingi na sekondari na kuongeza kuwa mgodi ulijenga shule ya sekondari ya Ingwe kwa shilingi bilioni 1.1 miradi ambayo imekamilika.

Alisema kuwa mgodi ulifanya ukarabati pamoja na ujenzi wa shule ya sekondari ya Kemambo kwa gharama ya shilingi milioni 905.5, na shule ya msingi ya Bong’eng’e kwa gharama ya shiligi milioni 827.

Aliongeza kuwa mgodi huo katika awamu yake ya kwanza ulichangia shilingi milioni 605. 8 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Nyamwaga mradi ambao bado unaendelea.

“ Pia   mgodi uligharamia shilingi milioni 12.7 kwa ajili ya wanafunzi waliofanya vizuri kusoma katika shule na vyuo mbalimbali”, alisema Bi Mssumi

Aliongeza kuwa nia ya kuwekeza katika elimu katika wilaya ya Tarime ni kuhakikisha wanajenga msingi utakaopelekea kupatikana wataalamu kwa ajili ya kufanya kazi katika mgodi huo.

Akielezea mchango wa mgodi huo katika sekta ya afya Bi Mssumi alitaja miradi mingine kuwa ni pamoja na ukarabati na ujenzi wa zahanati ya Genkuru uliogharimu shilingi milioni 61.2, upimaji wa macho kwa wanakijiji 3,000 kwa shilingi milioni 19 pamoja na upimaji wa virusi vya Ukimwi kwa wanakijiji 1067 uliogharimu shilingi milioni tano.

Aliendelea kusema kuwa mgodi huo ulitoa msaada kwaajili ya upasuaji kwa wanakijiji 11 ambapo jumla ya shilingi milioni 12.2 zilitumika

Akielezea sekta ya maji Bi. Mssumi alisema kuwa mgodi ulichimba visima katika vijiji sita kwa thamani ya shilingi milioni 888.3 pamoja na usambazaji wa maji katika vijiji vya Nyangoto, Kewanja, Matongo na Kerende uliogharimu shilingi bilioni 1.2

Alisema kuwa mgodi pia ulifanya ukarabati katika kituo cha afya cha Nyangoto kwa gharama ya shilingi milioni 481.7 pamoja na usafi katika vijiji vya Nyangoto, Kerende, Kewanja na Nyamwaga uliogharimu shilingi milioni 544.4

Alisisitiza kuwa ili kuhakikisha kuwa wachimbaji wadogo wananufaika na sekta ya madini kupitia kujiajiri mgodi huo ulichangia shilingi milioni 91.4 kwa kikundi cha wachimbaji wadogo Tarime kwa ajili ya ununuzi wa mashine kwa ajili ya kusaga kokoto.

Bi Mssumi aliongeza kuwa hatua iliyofikiwa sasa ni mkandarasi kufanya kazi ya kutoa umeme kutoka mgodi wa North Mara hadi mashine ilipo ili ianze kazi mara moja.

Alisema kuwa mgodi pia ulifadhili   miradi mbalimbali kwa gharama ya shilingi milioni 252.5 pamoja na vikundi vya kijamii/kidini kwa gharama ya shilingi bilioni 1.8

Akizungumzia mchango wa mgodi huo katika sekta ya miundombinu Bi Mssumi alisema kuwa mgodi huo ulikarabati barabara yenye urefu wa kilomita 47.9 kwa gharama ya shilingi milioni 469 pamoja na uunganishaji wa umeme kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) katika vijiji vya Kerende na Matongo kwa gharama ya shilingi milioni 472

Alitaja miradi mingine kuwa ni pamoja na ujenzi wa kituo cha polisi uliogharimu shilingi milioni 555.5 na ujenzi wa mahakama ya mwanzo Nyamongo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za wafanyakazi wa mahakama hiyo kwa shilingi milioni 182.9 mradi ambao haujakamilika bado.

Akizungumzia changamoto katika   utekelezaji wa miradi hiyo, Bi. Mssumi alisema kuwa kumekuwepo na tatizo la wanavijiji kuhujumu miundombinu ya maji iliyowekwa hali inayopelekea mgodi huo kuingia gharama kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu hiyo.

“Wapo wanakijiji wasio waaminifu ambao huharibu miundombinu ya maji kwa makusudi ili kufanya biashara ya maji jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya vijiji hivyo” Alisisitiza Bi. Mssumi.

MAJAMBAZI WATANORAIA WA BURUNDI WAUWAWA KIGOMA WAKUTWA NA MABOMU 3 SILAHA 2 RISASI 64

Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma Kamishina Msaidizi Japhari Muhamed akionyesha siraha walizokuwa nazo majambazi waliouwawa leo alfajiri.
Mabomu, bunduki na vyakula vyenye nembo ya kutoka nchi ya Burundi walivyokutwa navyo majambazi
Silaha walizokuwa nazo majambazi katika eneo la tukio Kigoma


Na Magreth Magosso,Kigoma

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma limefanikiwa kuyauwa Majambazi watano raia kutoka nchi ya Burundi leo(jana) alfajiri katika   Barabara Kuu ya Kasulu Kibondo eneo la pori la malagarasi wakiwa tayari kuteka mabasi ya abiria mbalimbali yaendayo mikoani.
 
Pia walikuta mfuko wa salfeti uliokuwa na mabonu matatu ya kutupa kwa mkono,silaha za moto  mbili moja aina ya AK 47 yenye namba UA40501997,SMG namba 691220 ,magazine tatu  pamoja na risasi 64.
 
Akifafanua hilo jana ofisini kwake kigoma Ujiji Kamishna Msaidizi wa polisi Jaffari Mohamed  alisema  Septemba ,3,mwaka huu  saa 11.45 alfajiri  askari polisi wakiwa wamejipanga katika eneo la tukio hilo waliwakuta wakiandaa silaha zao tayari kufanya mashambulizi kwa walengwa.
 
“tulibaini njama  hizo kutoka kwa wadau wetu,askari walipofika eneo hilo walishuhudia harakati zao badae nao walibaini  askari wetu na walianza kufyatua risasi bila mpangilio mungu ni mwema tumeyauwa  na maiti zipo hospitali ya wilaya ya kasulu”alianisha Mohamed.

Alisema  wananchi kwa kushirkiana na wajumbe wa vikao vya kamati ndogo na kubwa za ulinzi hasa polisi jamii zimechangia kufanikisha hayo ambapo hivi karibuni wilaya ya buhigwe majambazi watano  raia wa nchi hiyo waliua watu wanne na kujeruhi saba kwa kutupa bomu katika basi la abiria.
 
Kwa upande wa Naibu kamishna idara ya uhamiaji wa hapa Ebrosy Mwanguku alibainisha kuwa,changamoto ya matukio ya uhalifu katika mkoa huo ni kutokana na uhalisia wa mipaka ambayo ina vipenyo vingi visivyo na vituo vya uhamiaji na askari polisi hali inayochangia wahalifu kutoka huko kushambulia raia wa hapa.
 
Naye Mkuu wa wilaya ya kasulu Danny Makanga alisema kupitia vikao vya ujirani mwema unaoshirikisha  nchi  tatu ambazo zinapakana na kigoma(Drc Kongo,Burundi ) wahakikishe wanakusanya silaha zilizozagaa nchini kwao ili kuheshimu madhimio 12 yaliyoadhimiwa katika kikao cha Agost,15,mwaka huu.  
 
Ubalozi mdogo wa Burundi Johnbosco Ngayikengurukiye alipoulizwa kwa nini raia wa Burundi hukutwa katika matukio yasiyorasmi hasa uhamiaji haramu na uhalifu akiri changamoto hiyo inamumiza kichwa na kubainisha ukosefu wa ardhi na ajira chachu ya hayo.

Jamboleo limebaini bidhaa zilizokutwa katika kiroba cha majambazi hayo ni mikate iliyookwa kiasili na juisi iliyosindikwa  `Zaam Zam Orange'ambayo ni moja yakinywaji kiwanda  cha  Mona`s,ambavyo huvila pale wanapohisi njaa katika safari ya kuja hapa.

Hivyo changamoto ya mipaka mikubwa  isiyokuwa na idara nyeti za ulinzi  kuingia kinyemela usiku kwa usiku na kufanya uhalifuambapo hitaji  la vituo  ni 14 ni chachu ya  kuimarisha ulinzi lakini  kwa sasa kigoma ina vituo  viwili tu venye  huduma hiyo hali inayochangia majanga ya uhalifu kushamiri kila kukicha.

Wednesday, September 3, 2014

UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU HAPA NCHINI UNAANZIA PALE MTU ANAPOKAMATWA NA VYOMBO VYA DOLA


DSC_0478SULEIMAN MSUYA
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHGG) imesema asilimia kubwa ya ukiukwaji wa haki za binadamu hapa nchini unaanzia pale mtu anapokamatwa na vyombo vya dola kwenye mahojiano pamoja na mahabusu.
 
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Kisheria (CHGG) Nabor Assey wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
 
Assey alisema utafiti unaonyesha kuwa wengi wao wanakamatwa pasipo utaratibu, kudhalilishwa, kuteswa, kubambikiwa kesi, kuwekwa muda mrefu bila kufikishwa mahakamani na kuwepo mazingira magumu ya dhamana jambo linalokiuka haki za binadamu zilizoainishwa katika ibara ya12 mpaka 24 ya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na sheria zingine za nchi na mikataba ya kimataifa iliyoridhiwa.
 
Mkurugenzi huyo utafiti huo unaonyesha kuwa asilimia 50 ya watu wanaoshikiliwa maeneo mbalimbali nchini ni mahabusu ambao ama wanasubiri kufikishwa mahakani au kesi zao zinaendelea katika mahakama mbalimbali bado hawajahukumiwa.
 
“Napenda kuweka wazi kuwa hii ni Idara huru ya Serikali tunachokisema hapa ni katika juhudi za kusaidia serikali kutatua changamoto ambazo zinaikabili jamii yake hasa katika masuala ya haki za binadamu” alisema.
 
Assey alisema ni wazi kuwa vyombo vya dola hasa jeshi la polisi limekuwa likishutumiwa kwa ukiukwaji wa haki za binadamu hali ambayo inahitaji elimu zaidi ambayo inaweza kusaidia kutatua tatizo hilo.
 
Alisema ni vema dhana halisi ya jina la polisi (Police Force) kubadishwa na kuwa (Police Service) ili kuwapatia uelewa kuwa wanapaswa kutoa huduma na sio kutumia nguvu zaidi kama njia ya kukabiliana na tatizo.
 
Mkurugenzi huyo alisema pia kuna mapungufu katika mfumo wa sheria za jina za Tanzania akitolea mfano ibara ya 13(6) (e) ya Katiba ya Tanzania ya 1977  inakataza utesaji kwa watuhumiwa na kuelekeza mamlaka za nchi kutunga sheria kwa minajili hiyo.
 
Alisema bado kuna  upungufu katika sheria kwani kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi  sura ya 6 ya sheria za Tanzania kinakata ushahidi uliopatikana kwa shinikizo la aina yoyote kutumika kama ushahidi halali mbele ya mahakama.
 
Assey alisema pamoja na sheria hizo kuonyesha ukatazo bado hazijaonyesha ni hatua gani atachukuliwa mtumishi yeyote ambaye atabainika kufanya vitengo vinavyokiuka haki za binadamu.
 
Alisema Tume yao ipo katika mchakato wa kuhakikisha kuwa vyombo vya usalama vinapatiwa elimu yakutosha juu ya nini majukumu yao pale ambapo wanamshikilia mtu ambaye amefanya kosa.
 
Mkurugenzi huyo alisema jitihada hizo zinatakuwa zikishirikisha wananchi hasa kwa kudai haki zao ambazo hazipo kisheria ambao wanaonekana kuwa waathirika wakubwa kutokana na vyombo vya dola hasa Jeshi la Polisi

Tuesday, September 2, 2014

NISHATI NA MADINI WAIMARISHA MKAKATI WA UTUNZAJI MAZINGIRA

day 2 - pic 1Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Emmanuel Shija akiwasilisha mada kuhusu ‘Uchimbaji mdogo wa Madini na Mazingira’ wakati wa semina ya mafunzo kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa. Semina hiyo ya siku nne inafanyika jijini Mwanza (Septemba 1-4, 2014) na imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara husika.
day 2 - pic 2Katibu Mtendaji wa TAREA (Tanzania Renewable Energy Association) Tawi la Kanda ya Ziwa, Bw. Jacob Ruhonyora akizungumzia uzoefu wake kuhusu faida za matumizi ya nishati jadidifu,kwa Wajumbe wa semina ya mafunzo ya mambo ya mazingira inayoendelea jijini Mwanza kuanzia Septemba 1, 2014. Semina hiyo ya siku nne imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara ya Nshati na Madini.
day 2 - pic 3Afisa Misitu Mkuu kutoka Kitengo cha Mazingira – Wizara ya Nishati na Madini (Kulia), Theodory Silinge akitoa ufafanuzi kuhusu umuhimu wa kuhimiza jamii kutumia nishati mbadala wakati wa semina ya mafunzo kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza, Septemba 1 – 4, 2014 day 2 - pic 4Afisa Sheria kutoka Wizara ya Nishati na Madini Renatus Damian, akiwasilisha mada kuhusu masuala ya sheria katika utunzaji mazingira wakati wa semina kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza Septemba 1 – 4, 2014.
day 2 - pic 5Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Nassor Abdullatif (Kushoto), akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa kufanya Tathmini ya Mazingira (Environmental Impact Assessment – EIA) kabla ya kuanza utekelezaji wa mradi wowote katika siku ya pili ya semina kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza Septemba 1 – 4, 2014.

AMERICAN SENATORS VISIT SERENGETI NATIONAL PARK

3US Senators heading to the vehicles ready for their game drive at Serengeti National Park
5Supporting staff of the US Senates delegation busy taking pictures.
7Zebras were also there to give US Senators maximum satisfaction of the beauty of Serengeti
9 
A cheetah hunting in the bush of Serengeti
Five American Senators have started a two days visit in Serengeti National Park as part of the official program in the country. The delegation led by the Senator of Michigan Ms. Debbie Stabenow who is also the Chairperson of the US Senate Committee on Agriculture, Nutrition and Forestry will have an opportunity to witness firsthand the vital role of conservation and good natural resources management in promoting sustainable economic development.

The US Senate delegation will also specifically demonstrate the challenges of combating the Wildlife Trafficking Crisis and methods for mitigation at the local, regional, national and the international level.

While in Serengeti, the delegation will visit sites of local conservation projects, view elephants and rhinos in their natural habitats, meet with leaders on the front lines in the war on poaching, and visit community projects that are working to preserve their natural resources, including threatened species. They will also learn about human-wildlife conflict and other issues of importance to local people.

Other Senators in the delegation includes Ms. Cantwell (Washington); Ms. Amy Klobuchar (Minnesota); Ms. Heidi Heitkamp (North Dakota) and Ms. Maize Hirono (Hawaii).

LADY JAYDEE AUNGANA NA MARIE STOPES TANZANIA KWENYE KAMPENI YA UZAZI WA MPANGO


IMG_2966Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marie Stopes Tanzania (MST), Uller Muller (kulia) akikabidhi kisanduku chenye vifaa vinavyohusika na masuala ya  uzazi wa mpango kwa  Balozi mpya wa Marie Stopes ambaye pia ni msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura ‘Lady jaydee’ katika hafla ya utiaji sahihi makubaliano  hayo katika ofisi za MST, jijiji Dar es Salaam jana.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Lady Jaydee, mwana muziki mashuhuri wa kizazi kipya nchini Tanzania, aliibua shangwe na chereko kwenye hospitali ya uzazi Marie Stopes iliyopo Mwenge, Dar es Salaam.  
 
Uwepo wa Jaydee ulitokana na kuungana kwa nyota huyu na Marie Stopes kwenye kampeni ya “Chagua Maisha” ambayo inalenga  kuboresha upatikanaji wa huduma za uzazi wa mpango katika jamii.
 
Akiongea na waandishi wa habari punde baada ya mazungumzo na Mkurugenzi Msimamizi wa MST nchini Tanzania, Bi Uller Muller, Lady Jaydee aliwaambia waandishi : “Nina furaha kubwa kuchukuka nafasi hii ya kipekee kama Balozi wa Marie Stopes kwa sababu wanafanya mengi kuwawezesha wakina mama kusimama na kujitegemea. 
 
Lengo kuu la Kampeni hii ya Chagua Maisha nikuhakikisha kila Mtanzania ana haki ya kuchagua mfumo wa uzazi wa mpango ili kulinda afya zao na kutimiza malengo yao ya kimaisha, hususan mabinti wadogo”.
 
Akitafakari sababu zilizompeleka kuungana na kampeni hii, Lady Jaydee alieleza: “siku zote nilikuwa naamini kuwa wanawake wana uwezo wa kubadilisha Tanzania kimaendeleo. Hivyo niliumizwa moyo sana nilipoambiwa hivi leo kuwa Wanawake wengi hupoteza maisha, na wasichana wengi wanalazimishwa kuacha masomo kutoka na ujauzito. 
 
Mimi nimeamua kusaidiana na Marie Stopes kuelimisha jamii nzima wanaweza kubalili fikra na hatima zao, kwa kutumia uzazi wa mpango”.
Continue reading →

RAIS KIKWETE AFUNGUA RASMI NYUMBA ZA MAKAZI ZA MEDELI LEO HII

1Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma wenye nyumba 150, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Rehema Nchimbi (wa kwanza kushoto) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene. Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Christopher Kangoye. (Picha zote kwa hisani ya Shirika la Nyumba la Taifa)
2Rais Jakaya Kikwete akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma wengine wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC, Nehemia Mchechu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji.
3 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma wenye nyumba 150, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene. Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Christopher Kangoye. 4 Majengo ya Nyumba za Makazi za Medeli Mjini Dodoma kama yanavyoonekana pichani. 5 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji huku Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Christopher Kangoye na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene wakishuhudia wakati wa ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma. Mradi una jumla ya nyumba 150. (Picha zote kwa hisani ya Shirika la Nyumba la Taifa) 6 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Meneja wa NHC katika Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu, Bulla Boma wakati wa ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma. 7 Rais Jakaya Kikwete katika picha ya pamoja na Watendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mara baada ya ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma.

STAR WA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) 2014, MWANAAFA MWINZAGO AWA KIVUTIO MITAA YA KARIAKOO

Mshindi wa Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 Mwanaafa Mwinzago (Katikati) akisindikizwa na Matron pamoja na Mfanyakazi wa TMT huku akilindwa na Mabaunsa wakati alipopelekwa Katika Mitaa ya Kariakoo kwaajili ya kununua zawadi Kwaajili ya Wazazi wake.
Mfanyakazi wa TMT, Happy Ngatunga (Kushoto) akitoa maelekezo kwa Mabaunsa na Mshindi wa TMT aliyejinyakulia Kitita Cha Shilingi milioni 50 katika fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Mlimani City Mwanaafa Mwinzago wakati walipokuwa katika matembezi Kariakoo.
Baadhi ya wafanyabiashara wa Kariakoo wakimpungia Mikono kama ishara ya kumpongeza kwa kuibuka mshindi wa fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) Star wa TMT 2014 kutoka Mtwara, Mwanaafa Mwinzago Wakati alipokatiza kwenye mitaa ya Kariakoo pindi alipokwenda kununua zawadi kwaajili ya wazazi wake
Star Wa TMT 2014, Mwanaafa Mwinzago (katikati) akiwa na furaha mara baada ya kupongezwa na mashabiki waliopata nafasi ya Kumsalimia na kumpongeza wakati akikatiza mitaa ya Kariakoo pindi alipokwenda kununua Zawadi kwaajili ya Wazazi wake
Wanafunzi wa Shule ya Msingi wakimpongeza Star Wa TMT 2014, Mwanaafa Mwinzago kwa kuweza kuibuka mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 kwa kuwabwaga mwenzake 9 na kuondoka na Kitita Cha Shilingi Milioni 50 za kitanzania wakati walipomuona katika moja ya mitaa ya Kariakoo wakati Star Huyo wa TMT 2014 alipokwenda Kununua Zawadi kwaajili ya kuwapatia wazazi wake ikiwa kama ishara ya Upendo na shukrani kwao.
Matron wa Kambi ya TMT 2014, Kemmy akichagua baadhi ya vitenge kwa Niaba ya Star Wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago wakati alipopelekwa Kariakoo kwaajili ya Kununua Vitenge kama zawadi kwa wazazi wake.

SIDO KUZINDUA MRADI WA MCHIKICHI

Na Magreth Magosso,Kigoma

SHIRIKA la kuhudumia viwanda vidogovidogo Mkoa wa Kigoma (Sido)  watazindua  Mradi wa Local Investment Climate ifikapo mosi, Octoba mwaka huu ,ukiwa na lengo la  kuboresha mazingira  ya  uchakataji wa bidhaa   za wajasiliamali  hasa zao la Mchikichi.
 
Akielezea hilo jana kwenye kufunga maonyesho ya wajasiliamali Kanda ya kati  ambapo mwaka huu yamefanyika  kigoma ujiji Meneja wa Sido wa hapa  Mackdonald  Maganga  alisema,mradi utaanza na zao moja muhimu katika mkoa na kulifanyia utafiti wa kina.
 
Pia watajenga kiwanda kidogo cha usindikaji wa zao husika,ambapo kwa hapa zao la mchikichi litapewa kipaumbele katika mradi mtambukwa kwa lengo la kuboresha zao hilo na kuteka soko  nchi za Afrika Mashariki.

“mchikichi   zao kuu na asili ,  kwenye maonyesho hayakuwepo mafuta ya mawese unajua kwa nini  kutokana na mazingira ya uandaaji wa mafuta hayo ni duni , ukiona wanavyofanya huwezi kuyatumia ,ingawa mawese yanafaida mwilini” alibainisha  Maganga.

Mradi huo unasimamiwa na shirika la Danida  ambapo watatumia shamba darasa kwa  walengwa wachache wenye vigezo, ili kulinyanyua zao hilo kutoka kwenye kiwango duni hadi ubora wa kimataifa .
 
Alisema mashirika ya usajili (Brela) ubora wa bidhaa na chakula (Tfda),(Tbs  waweke  ofisi  kigoma ili kupunguza  umbali  na urasimu katika utendaji kazi kwa wadau na kutoa wito kwa umma watumie fursa  zilizopo kujikwamua na umaskini.
 
Kwa upande wa Meneja wa Mfuko wa hifadhi wa Nssf Josephat Komba alisema  wajasiliamali wa wilaya ya kigoma wanakabiliwa na bidhaa duni walizonazo ukilinganisha na  wilaya ya kasulu na mikoa  mingine.
 
Alisema jamii  itumie fursa za Asasi za kifedha ili kupanua wigo wa ubunifu,elimu  ili kuhodhi soko la mipakani hasa nchi jirani  na kuongeza ajira kwa wakazi ambapo kwa mwaka 2014 januari -agust wamekopesha bilioni 4 kwa  vikundi  Vinne  kikiwemo cha wakulima.

Monday, September 1, 2014

NAIBU IGP AKUTAKA NA MAKAMISHINA WA POLISI KUTOKA NAMIBIA

1Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi,Abdulrahman Kaniki akimkabidhi zawadi Kamishna wa Polisi wa Namibia Bw.Schalk Meuwesen ofisini kwake jana.Kamishna huyo yupo nchini kwa ziara ya siku tatu akiwa na maafisa wengine kutoka Namibia kujifunza jinsi Jeshi la Polisi Tanzania lilivyofanikiwa katika kutekeleza Maboresho yake.(Picha na Frank Geofray wa Jeshi la Polisi).
2Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi,Abdulrahman Kaniki akimfafanulia namna maboresho ya Polisi yalivyoanza Kamishna wa Polisi wa Namibia Bw.Schalk Meuwesen ofisini kwake jana.Kamishna huyo yupo nchini kwa ziara ya siku tatu akiwa na maafisa wengine kutoka Namibia kujifunza jinsi Jeshi la Polisi Tanzania lilivyofanikiwa katika kutekeleza Maboresho yake.(Picha na Frank Geofray wa Jeshi la Polisi).
3Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi,Abdulrahman Kaniki akiwafafanulia namna maboresho ya Polisi yalivyoanza Makamishna wa Polisi kutoka Jeshi la Polisi la nchini Namibia Bw.Schalk Meuwesen na Bw.Abed Kashihakumwa ofisini kwake jana.makamishna hao pamoja maafisa wengine wapo nchini kwa ziara ya siku tatu kujifunza jinsi Jeshi la Polisi Tanzania lilivyofanikiwa katika kutekeleza Maboresho yake.(Picha na Frank Geofray wa Jeshi la Polisi).

CHADEMA TABORA WAPATA MWENYEKITI MPYA

Na Allan Ntana, Tabora

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Tabora kimepata safu mpya ya uongozi baada ya kufanya uchaguzi wake mkuu katika ngazi ya mkoa hapo jana katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Ualimu Tabora.

Katika mkutano huo wa uchaguzi nafasi zilizokuwa zinagombewa ni Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa na Katibu wa Mkoa na Mwenyekiti na Katibu wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA), Baraza la Wanawake (BAWACHA) na Baraza la Wazee.

Aliyeibuka kidedea katika nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Tabora ni Bw. Francis William Msyuka aliyepata kura 46 na kumshinda mgombea mwenzake Bw.Hassan Said aliyepata kura 17 kati ya kura zote 66 zilizopigwa huku kura 3 zikiharibika.

Na aliyeibuka kidedea katika nafasi ya Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Tabora ni Bw.Alinanuswe Mwakilima ambaye alipigiwa kura za ndio 57 na hapana 2 kati ya kura zote 61 baada ya kukosa mpinzani katika wajumbe wote waliohudhuria mkutano huo.

Waliochaguliwa kuongoza mabaraza ya chama hicho katika ngazi ya mkoa ni, BAVICHA, Mwenyekiti ni Lazaro Damson na Katibu wake ni Daud Ndelwa, BAWACHA Mwenyekiti ni Sada Kabezi na Katibu wake ni Anna Nyawacha na Baraza la WAZEE Mwenyekiti ni Joseph Tanganyika na Katibu wake ni Vicent Ndeuka.

 Msimamizi wa Uchaguzi huo Christopher Nyamwanji ambaye ni Mratibu wa chama hicho Kanda ya Magharibi aliwapongeza wajumbe wote waliohudhuria mkutano huo kwa kufanikisha zoezi hilo la kikatiba ndani ya chama kwa utulivu na amani huku akiwataka kukitumika chama hicho kwa moyo mmoja pasipo kuruhusu roho za usaliti kama walivyofanya viongozi waliokuwepo.

Naye diwani wa kata ya Bukene wilaya ya Nzega Omar Shehe kupitia chama hicho ambaye alikuwa Mwenyekiti wa mkutano huo wa Uchaguzi aliwataka viongozi hao kudumisha amani, mshikamano na uzalendo ndani ya chama hicho na kujiepusha na makundi ili kuwaunganisha vizuri wanachama katika mkoa huo hasa ikizingatiwa kuwa uchaguzi mkuu hauko mbali sana huku akiwaasa kutogopa changamoto za hapa na pale.

Akitoa shukrani zake Mwenyekiti mpya wa chama hicho Mkoa wa Tabora Francis William Msyuka alisema kazi kubwa iliyoko mbele yake ni kutengeneza mshikamano mzuri kwa viongozi wote na wanachama wa chama hicho kuanzia ngazi ya shina, wilaya, jimbo na mkoa na kuhamasisha maendeleo katika kila eneo husika sambamba na kukutana na wananchi ili kusikiliza kero zao.