Pages

KAPIPI TV

Tuesday, September 22, 2015

WAKAZI WA KIGOMA KUNUFAIKA NA UJENZI WA CHUO KIKUU -KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma
MGOMBEA Ubunge   Jimbo la kigoma Kaskazini Mkoa wa Kigoma kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Dkt,Yared Fubusa amesema ataendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kujenga Chuo kikuu ili kuongeza tija kwa wakazi wa hapo.

Akitoa kauli hiyo mbele ya wananchi wa Kata ya Kagongo  kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni anaoendelea kuzifanya katika kata na vijiji vilivyopo katika Jimbo hilo kwa kusihi wananchi wachague kiongozi mwenye makazi ya kudumu ambaye atashiriki kikamilifu katika mchakato wa kutatua kero zinazowakabili.

Dkt,Fubusa alisema hivi sasa anamiliki  Shule ya `Gombe school of Environment and Society’(GOSESO)na mwanzilishi wa ujenzi wa Chuo kikuu ,Gombe University of Tanzania(GUTA) na msimamizi wa tafiti za wanafunzi wa vyuo vikuu ndani na nje ya Nchi na  mwaka huu shule hiyo  imeshika nafasi ya kwanza kwa ufaulu wa wanafunzi kwa Kanda Magharibi na kitaifa imenyakua nafasi ya 11.

Alisema maendeleo hayaangalii vyama ,bali yanahitaji kiongozi mwenye utu,uzalendo na ubunifu wa kutumia uwezo alionao sambamba na elimu na kunufaisha  jamii, na yalete mabadiliko chanya kwa  kuondoa hali ngumu za maisha zinazochangiwa na mfumo mbovu wa serikali husika kushindwa kuwajibika kwa umma.

Dkt,Fubusa alianisha kuwa changamoto kubwa iliyopo kwenye Serikali ya Chama tawala (CCM) ni mfumo mbovu katika usimamizi wa rasilimali watu na mali ,ambapo wachache hunufaika na rasilimali za taifa,Hivyo hushindwa kudhibiti na kuwawajibisha kwa wakati wanaotuhumiwa na skendo za ubadhirifu wa mali za umma.

Dkt,Fubusa alieleza kuwa,kijiji cha Kagongo ni miongoni mwa vijiji vilivyopo pembezoni mwa Ziwa Tanganyika ,ambapo ni walinzi wa hifadhi ya Gombe,ambapo haifaidishi wakazi husika katika kuboresha kero zilizo ndani ya uwezo wao.

Alisema kisheria hifadhi hiyo inapaswa asilimia ya mapato yake kwa mwaka ili kutatua kero mbalimbali za kijamii kwa  mujibu wa sheria ya maliasili hasa misitu yenye hifadhi za wanyama na kuahidi akipewa ridhaa hapo ,Octoba,25, mwaka huu atasimamia hilo ili kuondoa kero ya madawati,vitabu vya ziada na kiada ili kustawisha jamii lengwa.

Aidha alisema anauhakika wananchi wana uelewa mpana wa elimu ya uraia kwa kuchagua kiongozi bora na sio bora kiongozi ,ambao wanadiriki kuhama familia zao na kwenda kupanga katika familia ya kaya nyingine,ilhali kaya yake inatabika na kero ya nishati ya kuzalisha viwanda,kilimo cha kisasa kupitia mabonde mtambukwa .

Kwa upande wa Kampeni meneja wa mgombea huyo Alhaji Salum Ndama alisema,wananchi wa jimbo la kigoma kaskazini hawana budi kufanya mabadiliko , kwa kuchagua mgombea mwenye vigezo muhimu na kwa Dkt,Fubusa anatosha kwa kuwa ni msomi pekee aliyewekeza katika sekta ya elimu na anasomesha watoto  wenye mazingira magumu 38 kila mwaka.

No comments: