Pages

KAPIPI TV

Wednesday, May 20, 2015

SERIKALI YAIAGIZA HALMASAHAURI YA WILAYA YA KALIUA KUWALIPIA KADI ZA CHF WALEMAVU NA WAZEE WASIOJIWEZA

Mkuu wa wilaya ya Kaliua Bw.Venas Mwamoto akizungumza na wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wilayani humo ambapo alitoa agizo la Serikali kwa Halmashauri kuanza utaratibu wa kuwalipia Kadi ya Mfuko wa Afya ya Jamii Walemavu na Wazee wasiojiweza fedha ambazo ameamuru zitoke kwenye mfuko wa maendeleo kuanzia ngazi za vijiji.
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kanda ya Magharibi Bw.Emmanuel Adina akisoma taarifa fupi ya uanzishwaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii wilayani Kaliua ambapo alihimiza Viongozi wa Serikali na Vyama vya Siasa kuifanya ajenda ya CHF ni muhimu kila wanapopata fursa ya kuzungumza na Wananchi katika mikutano mbalimbali hatua ambayo itasaidia kuihamasisha jamii kujiunga na CHF.
Dr.Gunini Kamba mganga mkuu mkoa wa Tabora akizungumzia umuhimu wa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii CHF,na kueleza mkakati mzima namna ambavyo mwananchi anaweza kunufaika atakapochangia Mfuko huo wa Afya ya Jamii.
Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wilayani Kaliua  wakipata elimu kuhusu faida za Mfuko wa Afya ya Jamii CHF.







No comments: