Pages

KAPIPI TV

Tuesday, April 21, 2015

CHADEMA YAPATA MRITHI WA JIMBO LA KIGOMA KASKAZINI 2015

 
Na Magreth Magosso, Kigoma
 
Mgombea Ubunge  Jimbo  la Kigoma Kaskazini  2015 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) Mkoa wa Kigoma,Dr.Yared Fubusa amesema kuwa,wananchi waishio vijijini watashindwa kujikwamua na kipato duni,ikiwa watadumisha siasa za upepo kwa kuchagua mgombea asiyejali kero zinazowakabili, ilihali mkoa una rasilimali za kutosha zitakazowanufaisha wakazi wake.
 
Akifafanua kauli hiyo Dr.Fubusa alisema kwamba,wananchi wanapaswa kutathimini uwajibikaji wa mgombea katika jimbo husika kwa kigezo cha mahusiano bora yenye maslai kwa jamii hiyo ,ili kuepuka viongozi wanaokimbia kuishi katika majimbo yao baada ya kuukwaa  ubunge kwa hadaa za mjini na kuonya  wasikubali kufanywa madaraja ya wagombea wenye maslai binafsi.
 
Alitaja sifa za mgombea bora ni pamoja na kuwekeza rasilimali mkoani mwake na kuishi jimboni humo  baada ya kumaliza vikao vya Bunge sanjari kutafuta wahisani wa kufadhili miradi mbalimbali ambayo ni chachu ya  kuboresha kero kadhaa ikiwemo ajira , afya,elimu,  miundombinu ya barabara  na nishati kwa lengo la kuondoa  kamba ya umaskini na ufakiri.
 
Alibainisha kuwa,ushirikishwaji wa wananchi katika usimamizi wa maliasili,uchumi na mazingira ni chanzo cha kupunguza adha ya ukosefu wa ajira kwa jamii, kwa kuwa watakuwa na uwezo wa kutumia fursa hizo ili kujikwamua katika tope la  umaskini  na dhana ya utegemezi wa kipato unatoka serikalini.
 
Dr.Fubusa alisema kipaumbele cha awali ni kuboresha zahanati ya bitale kuwa na hadhi ya hospitali ya wilaya ambapo kwa sasa wilaya haina ,  ujenzi wa sekondari katika  kata 14 , ujenzi wa soko   katika mji mdogo wa mwandiga,sanjari na ujenzi wa viwanda  vya uchakataji wa matunda(nanasi),kahawa na mchikichi ili kuongeza thamani ya bidhaa na kupunguza kero ya ajira .
 
Alisema ahadi hizo si za kubahatisha kwa kuwa anawafadhili kutoka watu wa marekani na kuwasihi wakazi wa vijiji vilivoporwa ardhi na hifadhi ya Gombe mwaka 1968 kufidiwa haki zao ambazo waliondolewa bila kufidiwa na kuongeza chanzo cha mapato katika mwalo wa kijiji cha Kalalangabo kwa kujengwa  forodha ili kuongeza mapato kwa halmashauri.
 
Mbali na hayo alisema kitendo cha halmashauri ya kijijini kutoa huduma katika jimbo la kigoma mjini ni fedheha na chanzo cha kushindwa kutoa huduma bora kwa wananchi wa jimbo la kigoma kaskazini na kushauri  majengo  yanastahili yawepo mji mdogo wa mwandiga.
 
“Raisi Jakaya kikwete ni kiongozi anayeunga mkono uthubutu wa Dr.Fubusa kuwa ni kijana pekee mzalendo ,jasiri na mwenye uchungu wa kuwaondoa watu wa eneo lake katika janga la umaskini kwa kuwa ametoa ajira zaidi ya watu 50 katika shule ya  sekondari Gombe na timu ya Mvuvumwa”alisema Mgombea huyo mwenye Phd ya uchumi,maliasili na mazingira.
 
Mwandishi wetu amezungumza na mkazi wa jimbo hilo Fadhili Hamisi juu ya mgombea huyo,alisema ni kijana pekee mwenye uthubutu wa kuishi kijijini na kuwekeza rasilimali kwa jamii ya kijiji cha kiganza anjari na kusogeza huduma ya elimu ya chuo kikuu mkoani humo na kutaka aongeze jitihada za makusudi kumaliza mgogoro wa ardhi baina yake na walengwa.
 
 Aidha hivi sasa anakabiliwa na  miradi mbalimbali ya elimu hususani ujenzi wa   vyumba  viwili vya madarasa ya kuanzia  na ofisi ya walimu  shule ya msingi mpya kijiji cha Mkabogo ,shule ya Luhobe na buhagala kata ya mkongoro   .Huku shule ya sekondari Gombe ikishika nafasi ya kwanza  kimkoa katika ufaulu kwa  wananfunzi waliomaliza kidato cha sita na Nnne mwaka jana.

No comments: