Pages

KAPIPI TV

Thursday, December 4, 2014

WAHAMIAJI WATAMBULIKA KISHERIA

Na Magreth Magosso,Kigoma

Zaidi ya wahamiaji walowezi 6,000 katika manispaa ya kigoma ujiji mkoani kigoma,wamefanikiwa kupata hati ya utambulisho wa kuishi  kisheria ,kutokana na juhudi ya serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la wakimbizi (IOM na U.K AIDS) kuwezesha  zoezi la kuwatambua na kuandikisha wageni,linaloendelea mkoani humo.

Hayo yalibainishwa na Mkuu wa idara ya uhamiaji  kigoma Ebrosy Mwanguku  kigoma ujiji juzi katika uwanja wa Lake Tanganyika  kwenye  uzinduzi rasmi wa kuandikisha raia walowezi,wakimbizi waliopewa uraia 1980,watoto wa waliopewa uraia,waliooa/kuolewa na watanzania .
 
Lengo la kufanya hivyo,ni kutambua uwepo wao na taarifa  kuhifadhiwa  katika `Kanzi data’ ili kubaini wahalifu wa matukio ya ujambazi sanjari na kuepusha migogoro ya uraia katika kipindi cha chaguzi  za kugombea  nyadhifa mbalimbali za madaraka kama ubunge,udiwani,uenyeviti wa mitaa na  urais.
 
Alisema zoezi lipo katika mkoa wa kigoma,Kagera na Geita kutokana na mikoa hiyo kuwa na changamoto kubwa ya kuwa karibu na nchi jirani husika,ambapo kwamakundi mtambukwa wanapewa fursa ya kujiandikisha ili waepukane na adha ya operesheni ya kamatakamata (uhamiaji usio rasmi).
 
Kamishna wa uhamiaji na udhibiti wa mipaka Abdallah Khamis  akiri walowezi wapo wengi nchini ,ambapo kipindi cha mwezi uliopita baada ya kutangaza zaidi ya kaya 6000 wamejitokeza ambapo ni miongoni mwa makundi mtambukwa,na kwa wilaya ya kigoma watu 1050 washapata vitambulisho husika.
 
Pia walowezi watapaiwa huduma za msingi ndani ya nchi na kudai kigoma ni chachu ya mafanikio ya mpango huo,ambao ni tija ya kubaini wahalifu na wanaovamia jukwaa la siasa kinyume cha vigezo vya kufanya hivyo na kuishukuru( IOM),Uk ,aids kwa kuwezesha zoezi hilo endelevu nchini.
 
Kwa upande  wa Mwakilishi wa shirika la kimataifa la wakimbizi ( IOM ) Tamara Keating alisema wahamiaji walowezi na waliopewa uraia mwaka 1980 sanjari na waliooa na kuolewa na raia wa hapa wakitaka kurudi kwenye asili ya nchi yao watasaidia kuwasafirisha na mtaji wa kuanzia maisha ya huko.
 
“fursa hii ni  ya kipekee ambapo mhanga ataandaliwa mazingira mazuri ya kuishi kwenye nchi yake kwa kuwezeshwa huduma zote za msingi ikiwemo malazi,chakula na fedha za kuanzia maisha ili wapate yote wanahitajika wajiandikishe kwa muda uliopo wakipuuza wasilaumiwe” alisema Keating.
 
Kaimu mkurugenzi idara ya wakimbizi mambo ya ndani Philo Nondo aliwahimiza walengwa watumie fursa waliyopatiwa na serikali kwa kushirikiana na( IOM ,Uk.Aids)  kufanikisha mchakato huo,ambao ni chachu ya kuondoa operesheni tokomeza zilizoweka majeraha kwa baadhi ya wahanga.
 
Mchungaji wa kanisa la (PEFA) Mwananzambe Bugondo  alisema serikali inathamini maisha ya wahamiaji wasio rasmi,awali waliishi kwa woga hali iliyochangia ashindwe kuwekeza kwa moyo mkunjufu na kushauri walengwa wa kigoma watumie fursa hiyo.

No comments: