Pages

KAPIPI TV

Tuesday, November 25, 2014

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI BUSINDE WATUMIA CHOO KIMOJA NA WALIMU WAO -KIGOMA

BUSINDE KIGOMA
Na Magreth Magosso,Kigoma

ZAIDI ya wanafunzi 400 wanaosoma shule ya msingi ya Businde iliyopo manispaa ya kigoma ujiji Mkoa wa kigoma wamelazimika kutumia choo cha walimu ,baada ya choo cha wanafunzi kutitia kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha huku  uongozi wa shule wapiga marukuku  matumizi ya choo hicho.

Kufungwa kwa choo hicho imekuwa faraja kwa wanafunzi husika kuepuka na madhara mbalimbali hasa ya kiafya,ambapo kutitia kwa matundu nane imechangiwa na  uchakavu wa choo hicho kilichojengwa na ukoloni wa mjerumani tangu mwaka 1954.
 
Akifafanua hilo Diwani wa kata ya businde Mauridi Makala alisema lengo la kuzuia matumizi ya choo hicho ni faida ya kuepusha maafa kwa wanafunzi husika,ambapo kwa sasa wanatumia matundu mawili ambayo walimu wanayatumia.

“mvua zinazoendelea kunyesha imechangia kubomoka kwa choo,kaya mbili kubomoka na kaya tano kuezuliwa mabati sanjari na barabara ya businde ujiji kukatika na kupelekea adha kwa wananchi husika” alisema Diwani huyo.

Akithibitisha hilo mtendaji wa kata husika Richard Mgae alisema changamoto  ya kutitia kwa choo ilifikishwa kwa uongozi wa manispaa ya ujiji na wamedai kupitia bajeti ya  fedha ya mwaka  2014/15/ watahakikisha wanalifanyia kazi.

Naye mratibu wa elimu kata ya businde Noel  Joel alisema ni kweli wamewaruhusu wananfunzi watumie choo cha walimu kwa muda hadi hapo adha hiyo itakapofanyiwa kazi,kwa nia ya kuondokana na maafa yasiyo na lazima.

Baadhi ya wanafunzi kwa nyakati tofauti Amina Rashid na Josefu emanuel walisema walimu wamewaruhusu watumie choo chao,kwa kuwa choo cha wanafunzi kimetitia ambapo ni hatari kwa matumizi kwa kuhofiwa kutumbukia katika mashimo ya matundu hayo.

Mwandishi wetu alifika katika shule ya msingi ya businde na kushuhudia bango lenye ujumbe wa kuwataka wananfunzi wasikitumie choo hicho,sanjari na kumkuta mama mmoja Faida Luziga akiwa na watoto  tisa, mmoja wa mwezi mmoja amejibanza kwenye kibanda cha jiko baada ya nyumba kubomoka.

No comments: