Pages

KAPIPI TV

Tuesday, November 25, 2014

MKOSAMALI APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUFANYA VURUGU KITUO CHA KUANDIKISHA WAPIGA KURA-KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

MBUNGE wa Jimbo la Muhambwe Wilaya ya Kibondo  Mkoa wa Kigoma,Felix Mkosamali amepandishwa kizimbani ( leo) katika Mahakama ya wilaya ya kibondo kujibu tuhuma dhidi ya kufanya vurugu katika kituo cha kuandikisha wapigakura .

Akisomewa jalada la kesi hiyo yenye namba 320/2014   mbele ya hakimu wa wilaya Erick Maley  mwendesha mashitaka wa mahakama ya wilaya ya kibondo Peter Makala alisema mbunge huyo alidaiwa kufanya fujo   katika kituo cha uandikishaji wa kupiga kura kilichopo kitongoji cha Nduta kijiji cha kumuhasha  kata ya Murungu  wilayani humo.

Alisema  Novemba,24,saa 9 alasiri mbunge huyo alitinga maeneo ya tukio na kudaiwa kumzuia karani  aliyekuwa akiandikisha wananchi waliofika hapo kwa kumnyang`anya vifaa husika kwa madai  waliofika kujiandikisha hapo ni wanachama wa chama tawala(CCM) huku vyama vya upinzani vikiachwa solemba.

Kitendo cha kumuinua karani na kuchukua  vitabu vyote na kuingia katika ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya kibondo  Mboya Judesadius na kumtupia makablasha husika,ikiwa ni sehemu ya kuonesha kutoridhishwa na utaratibu wa uandikishaji  katika kituo hicho.

Hakimu wa wilaya ya Kibondo Erick Malay alipomuliza mtuhumiwa juu ya shtaka lake ,mbunge huyo machachari awapo Bungeni alikana shtaka husika na kesi imeahirishwa na itasomwa tena Desemba,29,mwaka huu.

Awali Kamanda wa polisi mkoa wa kigoma Jafari Mohamed akiri mbunge huyo alifanya fujo  Novemba ,24,2014,saa 9,alasiri katika kitongoji cha nduta alikiuka sheria za malalamiko na kufanya fujo kituoni hapo, ilihali akijua ni kosa kisheria ambapo kwa raia yeyote bila kujali nyadhifa aliyonayo atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa katiba husika.

No comments: