Wanafuzi 16 wa kike katika shule ya sekondari ya
Mugombe wilaya ya Kibondo Mkoani hapa,wameshindwa kufanya mtihani wa majaribio wa kidato cha Nne baada ya kupatwa
na hali ya kuchanganyikiwa akili ghafla katika mazingira ya kutatanisha.
Wakizungumzia hilo kwa nyakati tofauti mbele ya waandishi wa
habari shuleni hapo, Tilifania Jonathan na Suzana Charles walisema Septemba 23,2014 majira ya mchana baada ya kumaliza mtihani wa tano walihisi maumivu makali ya
kichwa pamoja na kukosa nguvu mwilini kwa ghafla na kujikuta wanaanza kukimbiakimbia
hovyo.
Akielezea hilo Mkuu wa shule hiyo Tanu Selemani alikiri kuwepo kwa tukio hilo kwa wanafunzi wa kike tu,ambapo rasmi walianza wanafunzi
wawili mnamo 17,septemba mwaka huu na hali
kuwa mbaya zaidi tarehe 26,septemba na kusabaisha baadhi yao kurudishwa nyumbani kwao hatua iliyofanya pia kukosa kufanya baadhi ya mitihani.
“Tulidhani ni mzaha lakini muda ulivyozidi hali ilikuwa
mbaya zaidi ,tuliwafunga kamba za mikono na miguu ili kudhibiti kukimbia holela
na wengine kumi hawajarudi shuleni hadi leo wapo majumbani kwao na wazazi hawajarudisha
mrejesho juu ya afya zao aah ni tukio la kwanza” alisema Seleman.
Hata hivyo wanafunzi wapatao kumi kati yao bado wapo majumbani na watano
walifanyiwa maombi na mchungaji wa kanisa moja la kilokole la wilayani humo
Mwamko Lutego ambapo alidai walikutwa na nguvu za pepo na kufanikiwa kuyafukuza
kwa mujibu wa imani ya dini yao huku ikithibitika kuwa hali zao zimeanza kuimarika.
Diwani wa kata ya Kumsenga Simoni Kanguye ambaye alifuatana na timu ya wauguzi na mganga wa wilaya
pamoja na mchungaji huyo katika kufuatilia hali na kutathimini uhalisia wa chanzo cha maradhi
hayo ya aina yake,alisema hali hiyo imewashangaza sana kwakuwa baada ya kuwapima wanafunzi hao walikuwa hawana ugonjwa wa aina hiyo.
Aidha shule hiyo ni ya mchanganyiko pia ina mabweni ya wanafunzi wa jinsia zote,lakini adha hiyo huwakumba wanafunzi wa kike pekee.
No comments:
Post a Comment